NYERERE ni 'MSANII' kwanza mzalendo

Hapa unapotosha. Ni madarasa gani hayo "maalum" unayozungumzia? Tupo wengi tuliokuwepo enzi hizo!

Ilikuwa si rahisi kupata kadi za CCM kama mnavyozipata siku hizi kwa kununua tu.

Zamani kulikuwa na mafunzo maalum ambayo kila alietaka kupata kadi hiyo ilikubidi kuhudhulia mafunzo hayo kwa miezi mitatu ambayo yalikuwa yanaratibiwa na CCM yenyewe na kuendeshwa na makada wa CCM wengi wao walikuwa wanatoka Chuo cha Chama kivukoni. Na siku ya kupewa kadi hizo mlikuwa mnakula kiapo maalum kabla kukadhibiwa KADI Hiyo.

Na kwa kukufahamisha haikuwezekana kabisa mtu kuweza kujiunga na Chuo kikuu bila kuwa na Kadi ya Chama CCM na ilikuwa ni moja ya kigezo kuweza kuchaguliwa kujiunga hapo UDSM. Na kukujuza zaidi ulikuwa huwezi pata Passport au hata kazi Serikalini bila kuwa na Kadi za CCM. na kubwa zaidi hata maofisini au katika majeshi na mashirika yote kulikuwa na tawila CCM n viongozi wake walikuwa na nguvu kuliko hata Mkurugenzi mkuu.

Enzi hizo huko Tanzania ilikuwa na Sera kuwa Chama kimeshika hatamu za uongozi.

nafikiri nimekupa mwanga nafikiri waliowahi kupitia JKT nafikiri wanalijua hilo Pale RUVU JKT PEO alikuwa anaitwa WO II Nassari.

 
Kwa maelezo yako, unajaribu kutetea uongo kwa kusema uongo hapo kwenye red.

Na kama hilo ndilo lilikuwa dhumuni lake, tukubaliane kama lilimshinda kwa sababu kuanzia 1964 mpaka mwaka 1985 ni kama miaka 21 ilipita tokea muungano ambapo bado zilikuwa ni nchi mbili ambazo zinazoshughulikia mambo 17 ya muungano tu na mengine yalikuwa yanashughulikiwa na nchi mbili bila kutegemeana.

Tusizunguke zunguke, Muungano ulifanyika mahsusi tu siyo kwa manufaa ya nchi hizi mbili bali ilikuwa ni njama za kibeberu za kudhibiti ushawishi wa siasa za kimapinduzi za Chama cha Umma na viongozi wake ndani ya Baraza la Mapinduzi Zanzibar la wakati huo (rejea wikileaks cable) ndiyo maana hata ukweli mpaka leo unakuwa umefichwa ndani ya serikali ya TANU na sasa CCM

Kama ni hivyo unavyodai, mbona mikoa mingine haikuachwa ishughulikie mambo yake kama mkoa wa "zanzibar" ulivyoachwa?.


Watu wengi wamepotosha nakupindisha ukweli, dhumuni la mwalimu na waambata wake lilikuwa kuwa na NCHI moja tu ambayo ni Tanzania,

Zanzibar ulisimama kama mkoa tu baada ya Muungano.

Wapinga muungano wametufikisha hapa tulipo na mwisho watauvunja kabisa.
 
We kijana maswali magumu namna hiyo humu huwa hayaulizwi,,,,,,we waulize wazanzibar watakujibu lakini hawa vijana wagonjwa wa chademaliasis wanaugonnjwa wa kupenda chongo huita kengeza

hapo ndipo busara inapomuacha mtu kama wewe,mimi sijaona uhusiano wowote kati ya chadema na hoja iliyoletwa, hoja iko too general sasa wewe sijui umetumia kiungo gani cha mwili wako tofauti na ubongo ndani ya kichwa chako kufikiria hivyo!!
 
Ilikuwa si rahisi kupata kadi za CCM kama mnavyozipata siku hizi kwa kununua tu.

Zamani kulikuwa na mafunzo maalum ambayo kila alietaka kupata kadi hiyo ilikubidi kuhudhulia mafunzo hayo kwa miezi mitatu ambayo yalikuwa yanaratibiwa na CCM yenyewe na kuendeshwa na makada wa CCM wengi wao walikuwa wanatoka Chuo cha Chama kivukoni. Na siku ya kupewa kadi hizo mlikuwa mnakula kiapo maalum kabla kukadhibiwa KADI Hiyo.

Na kwa kukufahamisha haikuwezekana kabisa mtu kuweza kujiunga na Chuo kikuu bila kuwa na Kadi ya Chama CCM na ilikuwa ni moja ya kigezo kuweza kuchaguliwa kujiunga hapo UDSM. Na kukujuza zaidi ulikuwa huwezi pata Passport au hata kazi Serikalini bila kuwa na Kadi za CCM. na kubwa zaidi hata maofisini au katika majeshi na mashirika yote kulikuwa na tawila CCM n viongozi wake walikuwa na nguvu kuliko hata Mkurugenzi mkuu.

Enzi hizo huko Tanzania ilikuwa na Sera kuwa Chama kimeshika hatamu za uongozi.

nafikiri nimekupa mwanga nafikiri waliowahi kupitia JKT nafikiri wanalijua hilo Pale RUVU JKT PEO alikuwa anaitwa WO II Nassari.

Hizo chumvi unazoongezea wadanganye wajukuu wetu. Kwa kukufahamisha mimi ni kizazi cha enzi za mkoloni. Yote hayo unayoongelea nimeyapitia kwa hiyo huwezi kunidanganya. Hebu nieleze hayo "madarasa ya miezi mitatu" unayoongelea yalikuwa wapi kwanza!
 
Hizo chumvi unazoongezea wadanganye wajukuu wetu. Kwa kukufahamisha mimi ni kizazi cha enzi za mkoloni. Yote hayo unayoongelea nimeyapitia kwa hiyo huwezi kunidanganya. Hebu nieleze hayo "madarasa ya miezi mitatu" unayoongelea yalikuwa wapi kwanza!

Mzee wa enzi za ukoloni

Naona ima hujasoma Chuo kikuu wakti wa Chama kimoja cha Siasa CCM na wala hujawahi kufanya kazi Tanzania wakti wa chama kimoja cha Siasa.

1. Lakin kifupi kwa tuliopitia JKT kulikuwa na somo la Siasa likifundishwa na PEO kwa makuruta wote kujua Katiba ya CCM na miongozo yake na Mkimaliza masomo hayo mnatunukiwa Kadi za CCM.

2. Ilikuwa huwezi pata admission UDSM kama wewe ni Mtanzania chini ya ufadhwili wa Serikali bila kuwa na Kadi ya CCM.

3. Ilikuwa huwezi kupata kazi Serikalini bila kuwa na kadi ya CCM

4. Ilikuwa huwezi kupata Passport ya Tz bila kuwa na Kadi ya CCM.

5.Kwa watu wasiobahatika kwenda JKT kulikuwa na mafunzo yaliyokuwa yanaandaliwa na matawi ya CCM ili kuwawezesha kuweza kujua Katiba na miongozo ya CCM mitaani. Na kabla kukabidhiwa kadi hiyo ilikuwa mnakula kiapo.

6. Kulikuwa na matawi ya CCM katika mashirika ya umma, majeshi na hata wizara za Serikali. Na wenyeviti wake walikuwa na sauti sana kulika hata watendaji wakuu wa taasisi hizo

Sasa labda nijuze katika point hizo hapo juu ni ipi si sahihi kwako?

 
Mzee wa enzi za ukoloni

Naona ima hujasoma Chuo kikuu wakti wa Chama kimoja cha Siasa CCM na wala hujawahi kufanya kazi Tanzania wakti wa chama kimoja cha Siasa.

1. Lakin kifupi kwa tuliopitia JKT kulikuwa na somo la Siasa likifundishwa na PEO kwa makuruta wote kujua Katiba ya CCM na miongozo yake na Mkimaliza masomo hayo mnatunukiwa Kadi za CCM.

2. Ilikuwa huwezi pata admission UDSM kama wewe ni Mtanzania chini ya ufadhwili wa Serikali bila kuwa na Kadi ya CCM.

3. Ilikuwa huwezi kupata kazi Serikalini bila kuwa na kadi ya CCM

4. Ilikuwa huwezi kupata Passport ya Tz bila kuwa na Kadi ya CCM.

5.Kwa watu wasiobahatika kwenda JKT kulikuwa na mafunzo yaliyokuwa yanaandaliwa na matawi ya CCM ili kuwawezesha kuweza kujua Katiba na miongozo ya CCM mitaani. Na kabla kukabidhiwa kadi hiyo ilikuwa mnakula kiapo.

6. Kulikuwa na matawi ya CCM katika mashirika ya umma, majeshi na hata wizara za Serikali. Na wenyeviti wake walikuwa na sauti sana kulika hata watendaji wakuu wa taasisi hizo

Sasa labda nijuze katika point hizo hapo juu ni ipi si sahihi kwako?

Aisee usijifanye mjuaji sana. JKT nimepitia (Oljoro, Mgulani, Pugu) na hata Chuo Kikuu UDSM nimehitimu, na shahada ya kwanza nilivalishwa na Mwl. Nyerere. Nilichokuuliza bado hujajibu. Hayo "madarasa maalum ya miezi mitatu" yalikuwa wapi? Hebu jibu hilo kwanza.
 
We kijana maswali magumu namna hiyo humu huwa hayaulizwi,,,,,,we waulize wazanzibar watakujibu lakini hawa vijana wagonjwa wa chademaliasis wanaugonnjwa wa kupenda chongo huita kengeza


Chademaliasis ndio nini? Huyu bwana ameleta maswali yenye kuchallenge muundo wa muungano wetu. Challenge za muundo wa muungano zinaathiri kila mtu bila kujali mrengo/unazi wa vyama vya siasa

Sasa wewe sijui umeamka na mood gani kwa Chadema kwa sababu sioni Chademaliasis inakujaje kwenye kuchambua swali zuri la kusugua vichwa. Nafikiri tuwe objective wakati mwingine ili tu-analyse mambo haya na tupate points za kutoa michango mahala pake yaani kwenye tume ya katiba mpya.

Hata kama tunalipwa kwa kazi tunayofanya humu, I think kutumia opportunity ya kila thread kukipaka chama usichokipenda si kielelezo cha weledi kwenye masuala ya nchi. Ni utoto. Anzisha thread yako kukiponda Chadema utapata wachaingiaji tu. Ila acha objectives za thread zingine zitimie
 
Back
Top Bottom