Nyerere na Karume walikagua gwaride kwa pamoja wakati wa sherehe za Muungano

Jamhuri ya Zanzibar

Senior Member
Jul 17, 2012
126
195
Picha ya Kwanza:

attachment.php


Rais Abeid Amani Karume wa Zanzibar akiwa na Rais Gamal Abdel Nasser wa Misri mara baada ya kiongozi huyo kuwasili Zanzibar kwa ziara rasmi tarehe 24 Septemba, 1966 ndani ya Muungano. Kushoto kwa Mzee Karume anaonekana Brigadier General Yussuf Himid. Leo hii sio tu Rais wa Zanzibar hana hadhi ya kukagua gwaride na kiongozi wa kigeni nchini lakini pia Zanzibar haina hata hadhi ya kufikiwa na mgeni huyo. Hayo ndio yaliyokuwa wakati wa Rais Obama na wakati wa ziara ya Mwai Kibaki ya kuwaaga watanzania. Rais wa Zanzibar alilazimika kwenda kupanga foleni na kushangilia mizinga uwanja wa ndege wa Dar es Salaam.

Picha ya Pili:

attachment.php



Malkia Elizabeth II wa Uingereza akiwa ameambatana na mwenyeji wake Rais wa Zanzibar Sheikh Aboud Jumbe mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Zanzibar kwa ziara rasmi katika visiwa hivi mwaka 1979.

Hadi wakati huo zilibakia angalau alama kama hizo za Muungano wenye heshima, haki na usawa kati ya Zanzibar na Tanganyika.

Sasa mambo yamegeuka. Badala ya Wakuu wa Madola ya kigeni kutembelea Zanzibar, kupokelewa rasmi kwa gwaride na kupigiwa mizinga 21 huku Wimbo wa Taifa wa Zanzibar na ule wa nchi ya Mkuu anayetutembelea zikipigwa kwa heshima, sasa Rais wa Zanzibar na wasaidizi wake hufunga safari kwenda Tanganyika kuwapokea Wakuu wa Nchi za Nje na kufanya nao mazungumzo yanayoihusu Zanzibar huko huko.

Hatuwezi tena kukubali udhalilishaji huu kuendelea. Hatuwezi tena kuwaachia Tanganyika udhibiti wa Mambo ya Nje yanayoihusu nchi yetu. Tumewaamini kwa miaka 50 sasa lakini wameshindwa kuonesha uaminifu.

Tunataka kuona suala la Mambo ya Nje linaondolewa katika orodha ya mambo ya Muungano na linasimamiwa na nchi washirika wenyewe kila nchi kati ya Zanzibar na Tanganyika kwa upande wake.

Picha ya Tatu:

attachment.php

Tofauti kati ya Serikali mbili za Karume na zilizopo sasa ambazo zimeipora Zanzibar hadhi yake. Nyerere na Karume walikagua gwaride kwa pamoja wakati wa sherehe za Muungano na sio peke yake. Hivi sasa mwenye hadhi hiyo ya kukagua jeshi wakati wa sherehe za Muungano ni Rais wa Jamhuri ya Muungano pekee.
 

Attachments

  • KARUME.jpg
    KARUME.jpg
    35.1 KB · Views: 3,403
  • karume1.jpg
    karume1.jpg
    29.9 KB · Views: 3,355
  • Mbili kwenda moja.jpg
    Mbili kwenda moja.jpg
    116.7 KB · Views: 3,420
CCM wanadai watanzania wanachohitaji ni barabara bora, huduma bora za afya, elimu bora, kipato bora n.k na wala si usawa katika muungano. Kama watanzania watapata vitu hivi, hawana shida yeyote na usawa wa kumuungano, wala watanganyika hawada haja na Identity yao kama nchi maadam wana vitu hivyo. Hayo ndiyo mawazo ya CCM.
 
Huwezi kuwa na marais wawili sawa katika nchi moja! Pengine hapo ilikuwa mwanzo tu kabla hatujaweka mifumo mixture na Katiba iliyokuwa inamtambulisha amiri jeshi mkuu.
 
we mchochezi. Badala udai mambo ya msingi ya maendeleo kama umeme,maji,barabara,ajira nk unadai haki ya kukagua gwaride!

mbinu ya CCM ya kipropaganda ya kuwaondoa watu kwenye hoja! Maji na barabara ni matokeo ya siasa makini!
 
Ukimuuliza maswali haya Asha Bakar mjumbe wa BMK kutokea Zanzibar atakujibu hivi.
ImageUploadedByJamiiForums1398704101.977581.jpg


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Huwezi kuwa na marais wawili sawa katika nchi moja! Pengine hapo ilikuwa mwanzo tu kabla hatujaweka mifumo mixture na Katiba iliyokuwa inamtambulisha amiri jeshi mkuu.

Kumbe mfumo mlijiwekea nyinyi sio alichokubali Karume kwa niaba ya wazanzibari? Mambo hadharani! Na Lukuvi anasema sababu yake ni asilimia 99 ya waislamu, wataanzisha dola ya kiislamu tusipoendelea kuwatawala. Wapi! Fararasi keshatoka bandani!
 
Kumbe mfumo mlijiwekea nyinyi sio alichokubali Karume kwa niaba ya wazanzibari? Mambo hadharani! Na Lukuvi anasema sababu yake ni asilimia 99 ya waislamu, wataanzisha dola ya kiislamu tusipoendelea kuwatawala. Wapi! Fararasi keshatoka bandani!
Duh! Kwani amiri jeshi mkuu ilianza lini. Marehemu Karume alikuwepo wakati Nyerere anakuwa amiri jeshi.
 
we mchochezi. Badala udai mambo ya msingi ya maendeleo kama umeme,maji,barabara,ajira nk unadai haki ya kukagua gwaride!

Hayo yoote Zanzibar yalikuwepo kwa burdan hata kabla ya Muungano, jibu hoja usipoteze muelekeo..
 
Huwezi kuwa na marais wawili sawa katika nchi moja! Pengine hapo ilikuwa mwanzo tu kabla hatujaweka mifumo mixture na Katiba iliyokuwa inamtambulisha amiri jeshi mkuu.

Wewe vp ni muungano wa nchi mbili,zanzibar na tanganyika,usawa ni lazima
 
we mchochezi. Badala udai mambo ya msingi ya maendeleo kama umeme,maji,barabara,ajira nk unadai haki ya kukagua gwaride!

mtu akizungumza ukweli, mchochezi, uamsho, alshabaab na majina mengine tele. hayo unayodai maendeleo pelekeni kwanza kwenye vijiji vyenu huko Tanganyika, tuacheni tupumue hamtufahamu
 
Wewe vp ni muungano wa nchi mbili,zanzibar na tanganyika,usawa ni lazima
Sasa vitu viwili vinavyofanana vikiungana si kinakuwa kinakuwa kitu kimoja! Sasa kama nchi mbili zilizosawa zimeungana matokeo ni nchi moja. Zikiwa ki nchi mbili zinakuwa hazijaungana bali zinashitikiana tu!
 
we mchochezi. Badala udai mambo ya msingi ya maendeleo kama umeme,maji,barabara,ajira nk unadai haki ya kukagua gwaride!

ukiondoa ajira, mambo yote ulioyataja sio mambo ya muungano, na hii ni kwa mujibu wa katiba ya sasa na hata rasimu ya warioba.......


kua makini usiburuzwe na ma ccm!!
 
Baada ya Jaribio la Mapinduzi au Uhaini la Rais Aboud Jumbe wa Zanzibar ambae cheo chake cha kwanza kilikuwa Makamu wa Rais wa Tanzania, baada ya uhaini katiba ilibadilishwa.
Sasa Makamu wa Rais wa Tanzania atakuwa huku huku Daressalaam na atoke upande wa pili wa Muungano.
Rais wa Visiwa amebaki kama Waziri asiye na Wizara Maalum na Gavana wa Visiwa ambavyo ni sehemu ya Tanzania.
mengine ni Udaku.
 
Zanzibar tunawabeba sana na ndio wanaofaidika na Muungano huu wa serikali 2. Tanganyika haifaidiki hata kidogo na Muungano. Angalia sherehe za Muungano, zanzibar hawakutoa hata sh 5.
 
Back
Top Bottom