Nyerere huko uliko!!!

Kizito

Member
Feb 23, 2008
69
2
Kama huko uliko baba yetu wa Taifa unasoma mawazo haya ya watoto wako uliotuacha huku tukiwa na amani na utulivu uliotukuka, basi naomba usome hapa kwa umakini mkubwa. Yule kijana ambae ulituambia bado mdogo na sasa amekuwa na akapanga kwenye lile jumba jeupe pale magogoni anawanyanyasa wafanyakazi. Hataki kuwasikiliza anawakejeli kama vile wakimbizi katika Ardhi yao uliyoikomboa toka kwa wakoroni.
Habari iko hivi: Mwezi wa kumi mwaka jana walitangaza nia ya kutaka kugoma baada ya kuona wamemuamba awaongezee kimshahara kiduchu tu hakuwasikiliza hadi ilipofika muda wa kugoma mwaka huu tare 3/5/2010 ndio anatoa majibu ya kejeli ya maswali ya mwezi wa kumi. toka huo mwezi wa kumi mwaka jana ameenda kwa jirani zaidi ya mala kumi na kaongeza posho ya kaka zetu walioko mjengoni zaidi ya asilimia kumi , vilevile kanunua mgari ya kifahali V8 kwa idadi isiyohesabika kila wizara inayo zaidi ya kumi haya hayakuwepo wakati wewe upo na hata zile wizara ambazo wewe uliziweka 13 na baadae 18 na mawaziri wako hawakuzidi 20 yeye mawaziri wako 57 na wakianza kwenda mjengoni wanafunga wizara nzima wanaondoka wote.

Tunaomba mwongozo tufanya nini je tumnyime kura kama alivyosema kura zetu hazina UDHU! hata tukimnyima atashinda tu ? Yaani Baba ukituona utatushangaa! TUPE MWONGOZO.
 
Jana nilikuwa nasikia radio TBC mwalimu alipikuwa Rais wafanyakazi walikuwa wakidai mishahara zaidi wakati ule aliwajibu serikali haina uwezo wa wa kuwalipa pesa hizo kama hawataki wache kazi !Ilikuwa hotuba kali sana kwa wafanyakazi wafuate TBC watakutafutia hotuba hiyo
 
Mwacheni mzee wa watu alale pema peponi, hili la Kikwete liko ndani ya uwezo wenu sio mungu wala Nyerere ndio wanaohusika.

Nivyema mkakubali wajibu wenu na kusimamia ya kwenu bila kumtegemea yeyote, sio mzungu wala mchina. Mnashindwa nini kumfata Kikwete na kuzungumza nae uso kwa uso kwanza kabla ya kuanza kulalamika. Mmelalamika sana kwa miaka yote ndio mfahamu pia inawezekana njia mnazotumia kutatua matatizo yenu sio sahihi.

Ipo njia nyingine ya kumaliza matatizo yenu sio kulalamika wala mgomo hizi ni za muda mfupi tu, umizeni vichwa kutafuta njia sahihi na sio kulalamika kila kukicha, mmelalamika sana inatosha.

Nyelele wakati wake umepita, huu ni wakati wenu goma liko uwanjani timbwilikeni. Kulalamika ni dalili za woga kama Kikwete sio basi atafutwe na achanwe live uso kwa uso, sio kujificha na kutupa maneno na kusingizia Nyerere. Mliambiwa kuweni myaone, sasa mnayaona sio magorofa ni Maisha.

Majibu ya matatizo yenu mnayo wenyewe, Nyerere keshamaliza ya kwake haya yenu. Manake dunia ilikuwepo kabla ya Nyerere na itaendelea kuwepo baada ya Nyerere.
 
Jana nilikuwa nasikia radio TBC mwalimu alipikuwa Rais wafanyakazi walikuwa wakidai mishahara zaidi wakati ule aliwajibu serikali haina uwezo wa wa kuwalipa pesa hizo kama hawataki wache kazi !Ilikuwa hotuba kali sana kwa wafanyakazi wafuate TBC watakutafutia hotuba hiyo

I think we need to be objective here wakuu. Well ni kweli Nyerere alikuwa mkali by then lakini je kulikuwa na matumizi ya kufuru ya serikali kama ya sasa? Mashangingi yasiyo na idadi? Safari na vikao visivyokwisha na posho ni almost 600,000 per day, Furniture majumbani kila mwaka, mishahara ya mpaka 25m kwa mtu mmoja na mengineyo kibao.
 
Kwa hali ya viongozi wetu wa nchi angefufuka na kuona ufisadi, udikteta, vitisho na manyanayaso wanayo wananchi basi angezimia na kufa tena.Tumuache mzee wa watu apunzike kwa raha zetu, sisi tulio hai tupambane kung'oa viongozi wasio waadilifu madarakani, hapo tutapona bila shida.
 
Jana nilikuwa nasikia radio TBC mwalimu alipikuwa Rais wafanyakazi walikuwa wakidai mishahara zaidi wakati ule aliwajibu serikali haina uwezo wa wa kuwalipa pesa hizo kama hawataki wache kazi !Ilikuwa hotuba kali sana kwa wafanyakazi wafuate TBC watakutafutia hotuba hiyo

Kwa hiyo unataka kutuambia nini? Kwamba kwa kuwa Mwalimu aliwaambia wafanyakazi wakati huo Serikali haina uwezo wa kuwalipa pesa hizo na Rais wa sasa naye anayo haki ya kuwaambia hivyo wafanyakazi bila kuangalia kwa dhati na ukweli kwamba Serikali ina uwezo au la?

Hata kama Mwalimu aliyasema maneno hayo, wakati huo gharama za kuishi hazikuwa kubwa kama ilivyo sasa. Watoto walikuwa wanasomeshwa bure; ukienda hospitali unapata huduma bure, hakuna mgonjwa aliyeambiwa akanunue dawa kwenye famasia!

Kwa nini hao TBC hawatoi hotuba za Mwalimu alizotoa kuelezea jinsi ambavyo uwiano mbaya wa vipato vya watu wa chini na wa juu na kusababisha matabaka ya walionacho na wasionacho kunavyoweza kuleta migogoro na kuondoa amani na utulivu nchini?
 
Tatizo la TBC Boramaisha ni kuwa wako pale kuwakilisha serekali bila kujali ya kuwa kodi zetu ndio zinawafanya wawe hewani.
 
Back
Top Bottom