NYARAKA: Watoto wa Magufuli, Dotto James na mke wa Makonda na viwanja huko Ununio, Dar

Status
Not open for further replies.
Labda ungetupa tip hiyo ardhi iliyoporwa ni kiasi gani na je wamepewa hao hao watatu ardhi yote au kuna watanzania wengine wamepewa ili hata tukipiga kelele au kusambaza ujumbe huu kuwe na mashiko maana tukumbuke hata viongozi na familia zao nao ni Watanzania wana haki ya kumilki ardhi kikubwa utaratibu ufuatwe
 
Sasa hivi kuna vijinyumba kuanzia za udongo mpaka tofali vimeandikwa CCM Block wanadai ni maeneo yao yaliyovamiwa.

Najaribu kujiuliza inakuwaje CCM waweze kurudisha maeneo yao lakini yale maeneo ya wazi ya wananchi yaliyouzwa kinyamela hayarudi? Je, CCM wana nguvu kuliko serikali zetu kiasi kwamba CCM wanaweza lakini serikali isirudishe maeneo ya wananchi?

Sizungumzii yale mashamba makubwa kama ya akina Sumaye? najua Sumaye asingeenda CHADEMA wasingeweza kuchukua hata eka moja
 
Hii ardhi iliporwa kutoka kwa nani? Maana ukisema kutoka kwa wananchi Dar kidogo haileweki. Hao wamiliki wa hiyo ardhi walikuwa wakina nani?
Subiri nitakapoleta uzi wenye heading 'wananchi dar waporwa ardhi' hapo ndo nitawataja hao wananchi walioporwa, lakin hii inahusu hao waliogawiwa ardhi iliyoporwa na nimewataja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yesu na maria!

Ufisadi katika sura mpya!Kweli hawa watu wameivana,mpaka viwanja wanagawiana sehemu moja!
Hii ni viwanja tu,deal gani nyingine wamepiga pamoja!
Halafu kuna mtu anahisi Makonda atakuja kutumbuliwa,mtasubiri sana!
Ukiona JPM yuko radhi nchi ikose matrilion ya misaada au mikopo ilimradi tu kumlinda Makonda basi ujue kuna binding force kubwa sana baina yao!
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…