WAKAZI wa Msangamkuu, Mtwara Mjini mkoani Mtwara na vitongoji vyake, jana walimiminika katika pwani ya Bahari ya Hindi kumshangaa samaki aina ya Nyangumi mwenye urefu wa futi 48 na tani zaidi ya 30.
Mbali na mshangao huo nyangumi huyo alikuwa kivutio kwa waliomwona huku ikielezwa kwamba mara ya mwisho samaki huyo alionekana zaidi ya miaka 25 iliyopita.
Akizungumza na Tanzania Daima, mvuvi wa samaki huyo Saidi Hassani ‘Ngassa' alisema Septemba 3 akiwa katika shughuli zake alizivuta nyavu na kubaini kuna uzito usio wa kawaida uliosababisha chombo chake kuvutwa na samaki huyo.
"Baada ya kuona anaweza kuniletea shida nilimuacha samaki huyo akiwa kwenye nyavu nilirudi nyumbani kuwaita watu wengine ili wanisaidie kuvuta nyavu… lakini siku ya kwanza na ya pili ilishindikana hadi siku ya tatu tulimvuta mpaka pwani," alisema Ngassa.
Ofisa Uvivu Manispaa ya Mtwara-Mikindani, Saidi Abdallah aliwataka wakazi wa Msangamkuu kutomla samaki huyo kwa kuwa ni sumu, badala yake watumie mafuta yake ambayo ni dawa ya misuli.
Chanzo: Tanzania Daima
wanasema nyangumi anatemaga kitu kinaitwa "ambari" hebu ichekino hyo ina thamani sana
Kaka usishangae sana hii ndo nchi yetu TZYou can see why some us get irritated with the government idea of promoting the nation seasonal blessing to boost tourism internal and abroad; hivi inakuaje wakazi wa Mtwara tu awajui kama kipindi hiki Nyangumi wanakusanyika kwa wingi mafia kwa sababu za uzazi?
Kwa baraka za Tanzania madini ni bonus tu ukubwa wake, urefu wa bahari na mazingira yanaweza toa another perspective of exotic holiday should the government choose to invest, ukijumlisha na ardhi yenye rutuba, vivutio vyawanyama second to none in the world you dont need a magician to tell you what is wrong with this nation its simply a matter of lacking ideas.
mzungu huyo akiogelea na nyangumi Mafia Ireland.
Mtu unakuja kujua vitu vingi kwa google maana shuleni amfundishwi mambo hayo; kwa mfano didn't know either Tuna wanapatikana Tanzania kwa wingi na wanapenda kuja kuzalia kwenye maji ya mipaka yetu sasa why on earth are we still obsessed with dagaa, hivi tuna mmoja wanakula watu wangapi or how many ways a tuna can be eaten plus business opportunity if you chose to package it for starters it is a favourite fish when it comes to sandwiches, yaani sielewi kwanini tumekazana na habari za katiba badala ya kupigania maendeleo.
Wabongo walivyo wa ajabu mnyama wamekuta amekufa wanakimbilia kukata nya kwa ajili ya kitoeo bila kajua sababu zilizomuua.
You can see why some us get irritated with the government idea of promoting the nation seasonal blessing to boost tourism internal and abroad; hivi inakuaje wakazi wa Mtwara tu awajui kama kipindi hiki Nyangumi wanakusanyika kwa wingi mafia kwa sababu za uzazi?
Kwa baraka za Tanzania madini ni bonus tu ukubwa wake, urefu wa bahari na mazingira yanaweza toa another perspective of exotic holiday should the government choose to invest, ukijumlisha na ardhi yenye rutuba, vivutio vyawanyama second to none in the world you dont need a magician to tell you what is wrong with this nation its simply a matter of lacking ideas.
mzungu huyo akiogelea na nyangumi Mafia Ireland.
Mtu unakuja kujua vitu vingi kwa google maana shuleni amfundishwi mambo hayo; kwa mfano didn't know either Tuna wanapatikana Tanzania kwa wingi na wanapenda kuja kuzalia kwenye maji ya mipaka yetu sasa why on earth are we still obsessed with dagaa, hivi tuna mmoja wanakula watu wangapi or how many ways a tuna can be eaten plus business opportunity if you chose to package it for starters it is a favourite fish when it comes to sandwiches, yaani sielewi kwanini tumekazana na habari za katiba badala ya kupigania maendeleo.
Dah kitoweo hicho,,,inapendeza unadaka kilo nyingi tia kwenye friji.
Dah! Bado tuna safari ndefu, yaani unakuta kitu kimejifia unakimbilia kitoeo.
Katika hicho kisiwa cha msangamkuu ambacho kinapakana na bandari ya mtwara na ndipo kuna mlango bahari wenye kina kirefu sana cha maji Afrika mashariki na kati ndio mana huyo nyangumi kapatikana kwenye hayo maji mrefu