Nusura nijiunge CCM

Nusura nijiunge CCM

Topic nzuri sana ILA vichaa wa CCM wanaiharibu, nawachukia sana sana
 
Aiseeee nilitaka nikushukue mkuu kwa maneno makali lakn baada ya kutulia na kuielewa thread, sina neno..

Pa1 kamanda.
 
My point kujiunga na chama is not a single event issue leo maselle kasema hivi najiunga kesho fulani kasema hivi najitoa nadhani ni more that that thus why democracy is not flourishing in Africa

"Nusura nijiunge na CCM" - ndo kichwa cha thread, nashawishika kuamini u-duni katika fasihi. Kusema " nusura..........." Kunaonyesha kiu au shauku aliyokwishakuwa nayo, ni lugha inay'onyesha jinsi gani mtu amekuwa katika kutafiti jambo kwa karibu. Ni dhahiri kuna ufatiliaji una'onekana kufanywa kwa mda mrefu pasipo hitimisho kwa sababu fulani na katika ufatialiaji huo kidogo afikie hitima yake lakini bado akagundua sivyo alivyodhani.

There is always a single event that becomes a turning point in a life cycle for every body or everything ....i.e. you only make a decision at one moment not many moments although the research may have gone over many.
 
Pole sana kaka kama unahitaji kujiunga na chama cha siasa na unatafuta mahali ambapo pana viongozi wenye UTHUBUTU basi kwa Afrika bada hawajazaliwa,hivyo chama hicho pia bado hakijazaliwa.

Kwanza kwa Maselle kumrukia Balozi wa Uingereza alionyesha UWOGA wa hali ya juu,maana Balozi yue wala hana hatia na Maselle anajua Balozi hana hatia ila anafanya kazi yake vyema ya kuhakikisha pesa za wapipa kodi wake zinafanya kazi iliyokuwa programmed na siyo kutajirisha mifuko ya wachache.

Ili kuitetea hoja yake akamrukia kamnyama kadogo ambako hakawezi kutosha mlo wa jioni.Maselle ameonyesha UWOGA wa wazi,angekuwa JASIRI na mwenye UTHUBUTU angetuambia ukweli bila kutikisa macho nani yupo behind IPTL SAGA.

Kwa heri na usiku mwema,ila pole sana maana chama ukitakacho utasubiri sana.
 
Alhamis tutamuuliza waziri mkuu juu ya kauli ya Masele bungeni ili ifutwe kwenye hansard, spika chonde chonde usimkingie kifua pinda nitakapouliza swali hili alhamis hii.
 
Subiri ukisha muuliza nita muuliza na mimi Mh. Benard Membe alienda kuongea nini na huyo balozi pale Serena Hotel baada ya week ya bunge.
 
Kwakuwa bado nipo kwenye utafiti na kutafuta chama cha kujiunga nacho,mwisho wa juma hili nilitaka kufanya uamuzi. Uamuzi wa kujiunga na CCM. Mimi nataka chama ambacho wanachama na viongozi wake wanaweza kusema ukweli bila ya kuangalia ukweli huo unaelekezwa kwa nani. Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Stephen Masele 'alipomkoromea' Balozi wa Uingereza kwa kuingilia mambo ya ndani ya nchi yetu nilifurahi na kuvutiwa.

Nikajua kuwa Balozi wa Uingereza 'atakiona cha moto' kidiplomasia na kinchi kwakuwa Serikali ya CCM haiwezi kuvumilia mambo yasiyo mazuri kwa mustakabali kwa Taifa. Nikajua kuwa CCM inaundwa na viongozi wathubutu na ambao wanaweza kuuelekeza uthubutu wao kwa yeyote na popote pale alipo. Nikajua ya kuwa kauli ya Masele ilifuatia utafiti wa kutosha na hilo lilikuwa 'onyo' tosha kwa Balozi wa Uingereza.

Kumbe wapi. Ilikuwa ni 'mikwara' yenye lengo la kisiasa tu. Lengo kuu lilikuwa ni kupitisha Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini na mambo mengine yaendelee. Ukweli umejidhihiri pale ambapo Katibu Mkuu Kiongozi,Balozi Ombeni Yohana Sefue amenukuliwa na vyombo vya habari kuwa kauli ya Masele si ya Serikali na ni ya kwake. Kurukwa kwa Masele kuna maana kubwa kisiasa. Kwamba, usanii hutumika kupata jambo fulani.

Kanusho la Balozi Sefue limenikumbusha sakata la Balozi wa China. Balozi huyu wa China alivaa kofia ya CCM na kuhutubia pamoja na kushiriki ipasavyo mikutano ya CCM kule Kanda ya Ziwa. Balozi huyu wa China,baada ya kukosolewa na wapinzani,alitetewa kila kona ya chama tawala na Serikali hadi sakata hilo lilipopoa. Sasa ninaamini kuwa, kuna Mabalozi wa aina mbili: wanaopendwa kwa matendo yao na 'wanaopondwa' kisanii.

Kabla ya kanusho la leo, nilitumaini kuwa nasi twaweza kuutetea utaifa wetu kama auteteavyo Rais Mugabe wa Zimbabwe. Rais Mugabe anapambana na yeyote kwa lolote.Hajawahi kurudi nyuma katika mapambano yake kwa anachokiamini na kukisimamia. Hata Uingereza inamfahamu vyema Rais Mugabe! Sisi bado sana kwa jambo hilo. Labda tukapate mafunzo toka kwake.

Baada ya kadhia hii ya Balozi wa Uingereza, nimerudi hatua nyingi mno kujiunga na CCM. Imani yangu imeshuka kwa kasi kama joto la jangwani wakati wa usiku. Mimi sipendi sanaa na usanii.
Una miaka mingapi?
 
Back
Top Bottom