Nukuu ya Heche John

Nukuu ya Heche John

mbinguni

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2013
Posts
2,767
Reaction score
1,068
“Kama tutashindwa kuwajibishana wenyewe kwa wenyewe katika makosa yenye ushahidi kama huu basi tutakuwa hatuna sababu ya kupewa nchi mwaka 2015 kwa kuwa hawa wasaliti hawawaathiri Wanachadema tu bali kila Mtanzania mpenda mabadiliko,” alisema.Tafakari nukuu hii.
 
Kwa hiyo ndio akaamua wengine awafukuze uanachama na mwingine ampongeze na kumsifia kuwa ni mtu maarufu?
 
kuwajibika au kuwajibisha limekuwa ni jambo dogo sana hapa kwetu na ndio maana wengi wamegeuza taasisi za umma kama vijiwe vya kahawa. Ni bora kuanzia hapa ili naye akitoka kwenye msitari historia itumike hivyo hivyo
 
Kuwajibika maana yake nini? Neno hili linatoholewa kutoka kwenye misingi utawala bora. Pillars of good governance. One of these pillars is Responsible/ acountable. It means being answerable for ones actions. Hii ndiyo kuwajibika kwa watu tunaowaongoza au kwa matendo yako binafsi. Ni tofauti na jinsi wengi wanavyolichukulia neno kuwajibika kama vile kuachia ngazi au kufukuzwa kazi. Hii si tafsiri halisiilnayokusudiwa kwenye utawala bora. Heche anaposema "tusipowajibishana wenyewe kwa wenyewe ana maanisha tusipofukuzana wenyewe kwa wenyewe, jambo ambalo ni upotofu wa dhana ya utawala bora. Lakini pia mtu anapotoa majibu kwa matendo/ makosa yake si lazima afukuzwe chama au kazi ili chama kionekane mbele ya jamii kuwa kinataka mabadiliko. Sidhani kama kona adhabu moja kwa kila kosa. Tukifanya hivyo tutakuwa wavivu wa kufikiri kwa kutoa jibu moja kwa kila swali.
"Kama tutashindwa kuwajibishana wenyewe kwa wenyewe katika makosa yenye ushahidi kama huu basi tutakuwa hatuna sababu ya kupewa nchi mwaka 2015 kwa kuwa hawa wasaliti hawawaathiri Wanachadema tu bali kila Mtanzania mpenda mabadiliko," alisema.Tafakari nukuu hii.
 
Nadhani ndiyo ukomavu WA misuses ningekuwa Mimi LAZIMA ningewapeleka polis wKachapwe na fimbo.
 
[h=2]
icon1.png
Tafakari ya Mwanakijiji leo...[/h] Uongozi ni ushawishi. Uongozi siyo kutegeana, kutegeshana, kunyemeleana na kufukuzana. Na uongozi siyo vitisho au mikwara. Kiongozi anayeishi kwa vitisho ni kiongozi aliyeshindwa hoja. Hili ni kweli kwa vyama vile vile; chama kinachoishi kwa vitisho kimeshindwa hoja. Tafakari

"Kama tutashindwa kuwajibishana wenyewe kwa wenyewe katika makosa yenye ushahidi kama huu basi tutakuwa hatuna sababu ya kupewa nchi mwaka 2015 kwa kuwa hawa wasaliti hawawaathiri Wanachadema tu bali kila Mtanzania mpenda mabadiliko," alisema.Tafakari nukuu hii.

- Dih! Kidumu chama tawala CCM! CCM Hoyeeeeee!!

le mutuz
 
Kwa hiyo ndio akaamua wengine awafukuze uanachama na mwingine ampongeze na kumsifia kuwa ni mtu maarufu?

Hayakuhusu; ebu fukuzeni mafisadi wanaojulikana hata na watoto wadogo mtaani.
 
Sidhani kama kona adhabu moja kwa kila kosa. Tukifanya hivyo tutakuwa wavivu wa kufikiri kwa kutoa jibu moja kwa kila swali.

Wamekwisha fukuzwa watakwenda kwenye chama kinachowajibika chenye utawala bora machoni penu. Mimi nawaona CCM ni cha mafisadi wanaoendesha bora utawala ndiyo maana wanakuwa na mamluki kwenye vyama vingine kwa hofu.
 
Kwa hiyo ndio akaamua wengine awafukuze uanachama na mwingine ampongeze na kumsifia kuwa ni mtu maarufu?

Heche hakuwafukuza bali kiako kiliamua kuwa hawafai, maamuzi hayakuwa ya Heche, yalikuwa ya Kamati ya Utendaji!!!
 
Kuna kuawjibika,na kuwajibishana,na sio kuwajibishana kwa shinikizo na kile tu cha mtaji wa kitu fulani bali kuwe ni jambo mtambuka kwa wale wote ambao kwao makosa na kutotimiza wajibu ni kawaida.
 
Kwa hiyo ndio akaamua wengine awafukuze uanachama na mwingine ampongeze na kumsifia kuwa ni mtu maarufu?

JULIANA aka SILIMU SASA UKIMWI NI HATARI SANA, YEYE NA WENZIE WALIKUWA WANAKATA TAWI SOTE TULOKALIA ULITEGEMEA NINI KIFANYIKE? KUWACHAPISHA LAPA, THATS ALL
 
"Kama tutashindwa kuwajibishana wenyewe kwa wenyewe katika makosa yenye ushahidi kama huu basi tutakuwa hatuna sababu ya kupewa nchi mwaka 2015 kwa kuwa hawa wasaliti hawawaathiri Wanachadema tu bali kila Mtanzania mpenda mabadiliko," alisema.Tafakari nukuu hii.

Bwanaeee, utakaaje na adui ndani? Atakuua ukiwa umelala, muasi aende out
 
Kama ni kweli walichokuwa wanaongea akina Juliana,Mwampamba basi naamini ujumbe umefika kwa jamii na kazi ya jamii ni kuchambua pumba na mahindi kwani kuwafukuza watu watano c chochote katika nchi yenye watu mil 44,lakini kama walikuwa wametumwa na ccm basi walaniwe maisha yao yote ya siasa.mungu ibariki chadema, mungu ibariki tanzania, mungu ibariki afrika."AMEN"
 
Kuwajibika maana yake nini? Neno hili linatoholewa kutoka kwenye misingi utawala bora. Pillars of good governance. One of these pillars is Responsible/ acountable. It means being answerable for ones actions. Hii ndiyo kuwajibika kwa watu tunaowaongoza au kwa matendo yako binafsi. Ni tofauti na jinsi wengi wanavyolichukulia neno kuwajibika kama vile kuachia ngazi au kufukuzwa kazi. Hii si tafsiri halisiilnayokusudiwa kwenye utawala bora. Heche anaposema "tusipowajibishana wenyewe kwa wenyewe ana maanisha tusipofukuzana wenyewe kwa wenyewe, jambo ambalo ni upotofu wa dhana ya utawala bora. Lakini pia mtu anapotoa majibu kwa matendo/ makosa
yake si lazima afukuzwe chama au kazi ili chama kionekane mbele ya jamii kuwa kinataka mabadiliko. Sidhani kama kona

dhabu moja kwa kila kosa. Tukifanya hivyo tutakuwa wavivu wa kufikiri kwa kutoa jibu moja kwa kila swali.


kwani mkuu, kuwajibishwa unaelewaje?Kufukuzwa sio kuwajibishwa?
 
Back
Top Bottom