Nukuu kumi (10) fikirishi za Katibu Mkuu wa CCM, Dkt Bashiru

Kwa bahati mbaya Bashiru hajui kuwa ndani ya ccm kuna ccm mbili. Ccm dola na ccm chama cha siasa. Ccm dola ndio inaamua nchi iendeshwe vipi na hiyo ndio inayoratibu nani awe kiongozi. Ccm dola ndio inayopora kura na kutoheshimu box la kura. Ccm dola inaundwa na viongozi wote wastaafu hasa wenye kumiliki mali walizochukua kwa wizi. Kundi hili la ccm dola linashirikisha viongozi wote wastaafu wa serikali na wa vyombo vya dola na taasisi nyingine. Hawa wanatumia ccm chama cha siasa kuhadaa umma kwamba ccm ni chama cha siasa. Ccm dola ndio yenye wazee wanaoamini kwenye mambo ya matambiko ya nchi hii kama mwenge wa uhuru na muungano. Kundi hili linaamini kwenye ushirikina sana, kulinda mali zao na madaraka. Wako radhi damu imwagike lakini ccm isitokee madarakani

Kuna ccm chama cha siasa chini ya Bashiru, hawa ni wale wanaomini kwenye kufanya siasa za ushindani lakini wana uwezo mdogo kwenye siasa za hoja. Hawana maamuzi yoyote ndani ya chama kwani hawajui chama na nchi inaendeshwaje. Kwenye kundi hili ndio kulipojaa watu wanaojipendekeza, wanafiki, wafanya fitina, wasaka tonge, wazinzi nk. Hawa ndio huvalishwa nguo za chama kwenye kila jambo kutokana na kuwa na viherehere ili wapate mlo wa siku. Hawa ndio hutumika kuiba kura, kuratibu vikundi vya kihalafu kufanya ukatili wakati wa uchaguzi na hushirikiana kwa karibu na vyombo vya dola baada ya kuchukua maagizo toka ndani ya ccm dola. Huyu Bashiri anajitahidi kuifanya ccm ikubalike lakini inakuwa ngumu ndio maana unaona anakuwa mkweli japo anahofia usalama wake, huku akiona ccm ikishinda kwa mbinu ovu ambazo yeye hashirikishwi. Isipokiwa anajua dhahiri ccm haiko madarakani kwa ridhaa ya wananchi bali kwa utashi wa kundi la ccm dola.
Kweli mkuu umechambua vizuri.Hayo mambo ni ya inner circle. Ni wale wabobezi ndio wanaelewa haya!
 
Kwa bahati mbaya Bashiru hajui kuwa ndani ya ccm kuna ccm mbili. Ccm dola na ccm chama cha siasa. Ccm dola ndio inaamua nchi iendeshwe vipi na hiyo ndio inayoratibu nani awe kiongozi. Ccm dola ndio inayopora kura na kutoheshimu box la kura. Ccm dola inaundwa na viongozi wote wastaafu hasa wenye kumiliki mali walizochukua kwa wizi. Kundi hili la ccm dola linashirikisha viongozi wote wastaafu wa serikali na wa vyombo vya dola na taasisi nyingine. Hawa wanatumia ccm chama cha siasa kuhadaa umma kwamba ccm ni chama cha siasa. Ccm dola ndio yenye wazee wanaoamini kwenye mambo ya matambiko ya nchi hii kama mwenge wa uhuru na muungano. Kundi hili linaamini kwenye ushirikina sana, kulinda mali zao na madaraka. Wako radhi damu imwagike lakini ccm isitokee madarakani

Kuna ccm chama cha siasa chini ya Bashiru, hawa ni wale wanaomini kwenye kufanya siasa za ushindani lakini wana uwezo mdogo kwenye siasa za hoja. Hawana maamuzi yoyote ndani ya chama kwani hawajui chama na nchi inaendeshwaje. Kwenye kundi hili ndio kulipojaa watu wanaojipendekeza, wanafiki, wafanya fitina, wasaka tonge, wazinzi nk. Hawa ndio huvalishwa nguo za chama kwenye kila jambo kutokana na kuwa na viherehere ili wapate mlo wa siku. Hawa ndio hutumika kuiba kura, kuratibu vikundi vya kihalafu kufanya ukatili wakati wa uchaguzi na hushirikiana kwa karibu na vyombo vya dola baada ya kuchukua maagizo toka ndani ya ccm dola. Huyu Bashiri anajitahidi kuifanya ccm ikubalike lakini inakuwa ngumu ndio maana unaona anakuwa mkweli japo anahofia usalama wake, huku akiona ccm ikishinda kwa mbinu ovu ambazo yeye hashirikishwi. Isipokiwa anajua dhahiri ccm haiko madarakani kwa ridhaa ya wananchi bali kwa utashi wa kundi la ccm dola.

HABARI,
"tindo,
Mimi nadhani na rudi mimi nadhani ni heri kuongozwa na CCM kwa sasa mpaka kitakapotokea chama kipya cha siasa kisicho na muamuzi mmoja.Leo kuna watu wameunda vyama vyao sasa kama katiba ya Nchi ndio inampa Rais guvu kubwa ya kuamua mambo Nchi ikichukuliwa na chadema ambacho ndio chama kikubwa Hivi nani atanzuiya mbowe kuweka watu wa kabila lake kila nafasi nyeti?Nasema hivyo chunguzeni wenyeviti wa matawi ya chadema vyuoni na mitaani utaona majina yao mbona vitu viko wazi?Kama chadema viti maalumu wanapeana ndugu itakuwaje?.Ni heri CCM ambapo hata Rais akiyeleza hawa wazee wastaafu wananguvu ya kumrekebisha sasa Vyama tawala wana wazee gani wa kuwatuliza.
Mimi napenda upinzani ila wasiwasi wangu uko hapo tu Mimi binafsi.


LUMUMBA
 
HABARI,
"tindo,
Mimi nadhani na rudi mimi nadhani ni heri kuongozwa na CCM kwa sasa mpaka kitakapotokea chama kipya cha siasa kisicho na muamuzi mmoja.Leo kuna watu wameunda vyama vyao sasa kama katiba ya Nchi ndio inampa Rais guvu kubwa ya kuamua mambo Nchi ikichukuliwa na chadema ambacho ndio chama kikubwa Hivi nani atanzuiya mbowe kuweka watu wa kabila lake kila nafasi nyeti?Nasema hivyo chunguzeni wenyeviti wa matawi ya chadema vyuoni na mitaani utaona majina yao mbona vitu viko wazi?Kama chadema viti maalumu wanapeana ndugu itakuwaje?.Ni heri CCM ambapo hata Rais akiyeleza hawa wazee wastaafu wananguvu ya kumrekebisha sasa Vyama tawala wana wazee gani wa kuwatuliza.
Mimi napenda upinzani ila wasiwasi wangu uko hapo tu Mimi binafsi.


LUMUMBA

Hapa ulichoongea ni habari ya mwamba ngozi.
 
Nukuu ni maneno mazuri ya misplaced msomi mzuri na mhadhiri wa Chuo Kikuu anayefundisha Chekechea ambao masafa yao ni ya chini mno kwamba ni muda tu ataachia ngazi au atatupiliwa mbali arudi Chuoni kwa wenzake. Hilo likitokea ni kwa manufaa take na wanafunzi wake.
 
Dr. BASHIRU ALLY KAKURWA aliteuliwa na Mwenyekiti wa CCM, Mh. Dr. JOHN JOSEPH POMBE MAGUFULI na kisha kuidhinishwa na NEC ya CCM kuwa Katibu Mkuu wa CCM tarehe 29 Mei 2018. Zifuatazo ni nukuu za Mwanazuoni huyu nguli na Mpenda mijadala ambazo amezitoa nyakati mbalimbali akitekeleza majukumu yake mapya ndani ya CCM:


1. *"Nimekuta wizi wa kutisha kwenye chama chetu na wengine nikiwataja hamtanielewa. Wanajifanya ni waheshimiwa kumbe ni wezi, wameiba magari, wameiba ardhi. Ukiwaskia nje wanabwatuka unawezakudhani ni wazalendo kumbe ni mijizi na kwenye vikao mkikaa hata kabla hamjafikia maamuzi, mijizi hiyo inatoka nje"*.

2. *"Mijadala ndio namna ya kuendeleza nchi yetu, mijadala ndiyo inatufanya tujisahihishe. Hatuwezi kusonga mbele bila mijadala. Tumekosea sana katika nchi yetu, tumepotea sana katika nchi yetu. Mbaya zaidi tumeanza kuogopa kusema ukweli, lazma tubadilike"*.

3. *"Tuambizane ukweli; kuanzia sasa CCM haitachukua tena wanamuziki kwaajili ya kampeni za chaguzi. Hivi wananchi mkiishapewa kofia na fulana halafu nyimbo za "mbele kwa mbele" zikapigwa, huwa mnapata nafasi ya kuhoji sifa za mnayetaka kumchagua? Wanamuziki wanakichaji chama fedha nyingi na wanafaidika wao na matumbo yao. Hivyo, kuanzia sasa hakuna tena kitu kama hicho"*;

4. *"Wapigakura wajanja wameanza tabia ya kudharau chaguzi. Wanabaki nyumbani kwani wanaona chaguzi ni kituko, ni mchezo wa kuigiza. Ndio maana leo kupata watu wa kwenda kupiga kura imekuwa shida. Note CCM tunakoshinda ni chini ya 30%, chini ya 40% . Hakuna mahali ambako wapigakura wamejitokeza kwa 50%. Na mwaka 2010 ulitia fora. Watu wengi walijiandikisha kumbe walikuwa wanataka kile kiparata (kitambulisho cha mpigakura) kwasababu huwa kinatumika polisi kumwekea mtu dhamana. Wakiishakipata wanaingia mitini. Kwa mara ya kwanza katika historia nchini, mwaka 2010 tukapata serikali ambayo haina uhalali wa kisiasa kwasababu 50% ya wapigakura walibaki nyumbani"*.

5. *"Msimu wa uchaguzi umekuwa msimu wa rushwa. Imefika mahali wagombea wanauza adi nyumba. Wengine wanaomba sana michango. Usipomchangia anakuwa mkali na kununua uso utadhani anakwenda kutibiwa. Akiishazikusanya fedha anakwenda kuwanunua mawakala, nao wanawanunua wananchi. Wananchi mnachotakiwa kufanya ni kubomoa soko la kura"*.

6. *"Napenda kuwafahamisha kwamba HUSSEIN BASHE sio mkorofi bali ni miongoni mwa wabunge wa CCM wadadisi. Kuna tofauti kubwa kati ya mdadisi na mkorofi. BASHE na NAPE NNAUYE ni miongoni mwa wanachama wetu wadadisi na wanasaidia kulichangamsha bunge ila wanatofautiana katika udadisi wao. NAPE kidogo ana joto zaidi kuliko BASHE. Wote nawafahamu vizuri hivyo msidanganywe kuwa NAPE na BASHE ni watukutu. Sio watukutu, ni wadadisi na wamewezesha mawaziri kufikiri kabla ya kutenda. Kutenda kila mmoja anawezakutenda, hata mwendawazimu anaweza kutenda lakini ili uweze kutenda kwa ufanisi na tija lazma ufikiri. Michango ya BASHE bungeni inafikirisha"*.

7. *"Mimi ninachosisitiza ni nidhamu na si kunyamazisha watu. Tutapata wapi fikra mpya bila kuhojiana, bila kujadiliana na bila kudadisi? Tusipofanya hivyo, Chama Chetu cha Mapinduzi kitakuwa chama mfu"*.

8. *"Nilikuwa Morogoro na akatajwa Waziri kuwa anamiliki hekari 1000. Watu wanatakakujua amezipataje na mi ntamwita waziri huyo nimuulize kusudi nikawajibu walioniuliza. Hatuwezi kuwa na viongozi ndani ya chama kinachojitambulisha kama chama cha wanyonge halafu baadhi yetu tunapora ardhi ya wanyonge. Ni suala la kuchagua kati ya kuwa Kiongozi wa CCM au kuwa Mporaji wa ardhi"*.

9. *"Na hii habari ya "Dar Es Salaam ya MAKONDA" sio sahihi. Hakuna "Dar es Salaam ya MAKONDA" ni "Dar we Salaam chini ya Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam, MAKONDA". Kuna wakati huwa namsikia MAKONDA akasema "Wananchi wangu", nani kamwambia ana wananchi wake? Hakuna wananchi wako. Hakuna kiongozi anamiliki wananchi, ni "wananchi wenzangu". Mwalimu Nyerere aliwahi kuonya juu ya ubinafsi .."mkianza kusema- mimi, wewe, sisi au wao hamfiki". Vongozi vijana mnapaswa kuwa wanyenyekevu na kuacha papara. Vinginevyo mtapotea kama walivyopotea viongozi wengine vijana waliopewa madaraka wakakosa unyenyekevu"* .

10. *"Nawashukuru sana watanzania. Nawashukuru watanzania kwa kunisomesha kwa kodi zao na hatimaye nikaweza kupata shahada zote tatu, kamwe sitawasahau watanzania. Nina deni kubwa la kulipa utumishi uliotukuka. Kazi niliyopewa ya kuwa Mtendaji Mkuu katika chama ni kubwa mno"*.

KWA hakika, nukuu hizi kuntu zinamtanabaisha Mh. BASHIRU kuwa ni mwanadamu wa aina gani, amedhamiria kuifanya CCM iwe chama cha aina gani na pia viongozi wa serikali ya CCM waweje.

KANYAGA TWENDE, MH. KATIBU MKUU
 
Hahah dude man. As if hakuna intelligent people from tanzania zaid ya bashiru pekee ?
Ndani ya muda mfupi eti kishakuwa presidential material. I say nope.
Apewe cheo serikalin tuone jinsi gani ana behave kwe madaraka. Kwa sasa ni too early
Kwa nini asiweze kuongoza nchi?He is intelligent,rational and committed to saving his country and Tanzanians.These are the type of people which our country needs as Presidents.Mnataka marais mazuzu?
 
Hahah dude man. As if hakuna intelligent people from tanzania zaid ya bashiru pekee ?
Ndani ya muda mfupi eti kishakuwa presidential material. I say nope.
Apewe cheo serikalin tuone jinsi gani ana behave kwe madaraka. Kwa sasa ni too early

On point...👍
 
Hahah dude man. As if hakuna intelligent people from tanzania zaid ya bashiru pekee ?
Ndani ya muda mfupi eti kishakuwa presidential material. I say nope.
Apewe cheo serikalin tuone jinsi gani ana behave kwe madaraka. Kwa sasa ni too early
Kijana inaelekea kimombo kwako ni shida,nimesema "these are the type of people." Hapa sijam-singleout Bashiru kwamba ndio the only intelligent person in Tanzania.It means wako wengi,lakini watu wa aina hiyo ndio tunaotaka waiongoze nchi at least for now while sanity still prevails.Subirini wakati wenu(kwenye utawala wa Shetani) you will be in charge,mkanyagane weee, hadi basi.
 
Kijana inaelekea kimombo kwako ni shida,nimesema "these are the type of people." Hapa sijam-singleout Bashiru kwamba ndio the only intelligent person in Tanzania.It means wako wengi,lakini watu wa aina hiyo ndio tunaotaka waiongoze nchi at least for now while sanity still prevails.Subirini wakati wenu(kwenye utawala wa Shetani) you will be in charge,mkanyagane weee, hadi basi.
Hahaha boy please. They way umejib as if niko upinzan. Sio kila mtu anaen oppose serikal ni mpinzan.. wengine ni raia wa kawaida wasio na mfangamano na chama au itakadi yoyote ile. They umejib ni as if mko wengi mnaotaka bashiru awe president... lakin kumbe ni ww mwenyewe.

Bashiru is a good person. But i doesnt mean lazima awe rais why? Because ccm kuna matabaka mazito. Kuwa president is not easy kama unavyodhani.
Kuna the system hawa ndio hupendekeza nani awe rais.. na si wanachama. Ukiwajua ao members basi utajua kwann ni ngumu.
 
Hahaha boy please. They way umejib as if niko upinzan. Sio kila mtu anaen oppose serikal ni mpinzan.. wengine ni raia wa kawaida wasio na mfangamano na chama au itakadi yoyote ile. They umejib ni as if mko wengi mnaotaka bashiru awe president... lakin kumbe ni ww mwenyewe.

Bashiru is a good person. But i doesnt mean lazima awe rais why? Because ccm kuna matabaka mazito. Kuwa president is not easy kama unavyodhani.
Kuna the system hawa ndio hupendekeza nani awe rais.. na si wanachama. Ukiwajua ao members basi utajua kwann ni ngumu.
Jamani hayo yote nayajua,ila in an
ideal situation,meaning mazingira ambayo hakuna kubebana bebana au huyu ni mwenzetu,Bashiru would be the best candidate,in the next election and beyond.Sioni anybody in CCM as bright as him.
 
Yes but umeshasema kubebana. Na ccm kubeban a kwingi. Angalia teuzi za wakuu wa mikoa wilaya.. kama haukuwa karib na mzee cheo huna.
Kwenye fair ground yes.. lakin kwenye ground ya sasa nope. He maybe a good candidate but kwa mfumo wa sasa hiyo nafas hawatampa.
Jamani hayo yote nayajua,ila in an
ideal situation,meaning mazingira ambayo hakuna kubebana bebana kwa maslahi fulani fulani,Bashiru would be the best candidate,in the next election and beyond.Sioni anybody in CCM as bright as him.
 
Yes but umeshasema kubebana. Na ccm kubeban a kwingi. Angalia teuzi za wakuu wa mikoa wilaya.. kama haukuwa karib na mzee cheo huna.
Kwenye fair ground yes.. lakin kwenye ground ya sasa nope. He maybe a good candidate but kwa mfumo wa sasa hiyo nafas hawatampa.
Hilo nalijua mkuu.All in all,thankyou for sharing.
 
Leo nimejikuta nafuatilia matamko ya wanasiasa.

Huyu Dr Bashiru huyu sijui kama anaeleweka.

Tumtazame hapa.

NUKUU KUMI MUJARAB ZA KATIBU MKUU WA CCM DR. BASHIRU !!!


Dr. BASHIRU ALLY KAKURWA aliteuliwa na Mwenyekiti wa CCM, Mh. Dr. JOHN JOSEPH POMBE MAGUFULI na kisha kuidhinishwa na NEC ya CCM kuwa Katibu Mkuu wa CCM tarehe 29 Mei 2018. Zifuatazo ni nukuu za Mwanazuoni huyu nguli na Mpenda mijadala ambazo amezitoa nyakati mbalimbali akitekeleza majukumu yake mapya ndani ya CCM:


1. "Nimekuta wizi wa kutisha kwenye chama chetu na wengine nikiwataja hamtanielewa. Wanajifanya ni waheshimiwa kumbe ni wezi, wameiba magari, wameiba ardhi. Ukiwaskia nje wanabwatuka unawezakudhani ni wazalendo kumbe ni mijizi na kwenye vikao mkikaa hata kabla hamjafikia maamuzi, mijizi hiyo inatoka nje".

2. "Mijadala ndio namna ya kuendeleza nchi yetu, mijadala ndiyo inatufanya tujisahihishe. Hatuwezi kusonga mbele bila mijadala. Tumekosea sana katika nchi yetu, tumepotea sana katika nchi yetu. Mbaya zaidi tumeanza kuogopa kusema ukweli, lazma tubadilike".

3. "Tuambizane ukweli; kuanzia sasa CCM haitachukua tena wanamuziki kwaajili ya kampeni za chaguzi. Hivi wananchi mkiishapewa kofia na fulana halafu nyimbo za "mbele kwa mbele" zikapigwa, huwa mnapata nafasi ya kuhoji sifa za mnayetaka kumchagua? Wanamuziki wanakichaji chama fedha nyingi na wanafaidika wao na matumbo yao. Hivyo, kuanzia sasa hakuna tena kitu kama hicho";

4. "Wapigakura wajanja wameanza tabia ya kudharau chaguzi. Wanabaki nyumbani kwani wanaona chaguzi ni kituko, ni mchezo wa kuigiza. Ndio maana leo kupata watu wa kwenda kupiga kura imekuwa shida. Note CCM tunakoshinda ni chini ya 30%, chini ya 40% . Hakuna mahali ambako wapigakura wamejitokeza kwa 50%. Na mwaka 2010 ulitia fora. Watu wengi walijiandikisha kumbe walikuwa wanataka kile kiparata (kitambulisho cha mpigakura) kwasababu huwa kinatumika polisi kumwekea mtu dhamana. Wakiishakipata wanaingia mitini. Kwa mara ya kwanza katika historia nchini, mwaka 2010 tukapata serikali ambayo haina uhalali wa kisiasa kwasababu 50% ya wapigakura walibaki nyumbani".

5. "Msimu wa uchaguzi umekuwa msimu wa rushwa. Imefika mahali wagombea wanauza adi nyumba. Wengine wanaomba sana michango. Usipomchangia anakuwa mkali na kununua uso utadhani anakwenda kutibiwa. Akiishazikusanya fedha anakwenda kuwanunua mawakala, nao wanawanunua wananchi. Wananchi mnachotakiwa kufanya ni kubomoa soko la kura".

6. "Napenda kuwafahamisha kwamba HUSSEIN BASHE sio mkorofi bali ni miongoni mwa wabunge wa CCM wadadisi. Kuna tofauti kubwa kati ya mdadisi na mkorofi. BASHE na NAPE NNAUYE ni miongoni mwa wanachama wetu wadadisi na wanasaidia kulichangamsha bunge ila wanatofautiana katika udadisi wao. NAPE kidogo ana joto zaidi kuliko BASHE. Wote nawafahamu vizuri hivyo msidanganywe kuwa NAPE na BASHE ni watukutu. Sio watukutu, ni wadadisi na wamewezesha mawaziri kufikiri kabla ya kutenda. Kutenda kila mmoja anawezakutenda, hata mwendawazimu anaweza kutenda lakini ili uweze kutenda kwa ufanisi na tija lazma ufikiri. Michango ya BASHE bungeni inafikirisha".

7. "Mimi ninachosisitiza ni nidhamu na si kunyamazisha watu. Tutapata wapi fikra mpya bila kuhojiana, bila kujadiliana na bila kudadisi? Tusipofanya hivyo, Chama Chetu cha Mapinduzi kitakuwa chama mfu".

8. "Nilikuwa Morogoro na akatajwa Waziri kuwa anamiliki hekari 1000. Watu wanatakakujua amezipataje na mi ntamwita waziri huyo nimuulize kusudi nikawajibu walioniuliza. Hatuwezi kuwa na viongozi ndani ya chama kinachojitambulisha kama chama cha wanyonge halafu baadhi yetu tunapora ardhi ya wanyonge. Ni suala la kuchagua kati ya kuwa Kiongozi wa CCM au kuwa Mporaji wa ardhi".

9. "Na hii habari ya "Dar Es Salaam ya MAKONDA" sio sahihi. Hakuna "Dar es Salaam ya MAKONDA" ni "Dar we Salaam chini ya Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam, MAKONDA". Kuna wakati huwa namsikia MAKONDA akasema "Wananchi wangu", nani kamwambia ana wananchi wake? Hakuna wananchi wako. Hakuna kiongozi anamiliki wananchi, ni "wananchi wenzangu". Mwalimu Nyerere aliwahi kuonya juu ya ubinafsi .."mkianza kusema- mimi, wewe, sisi au wao hamfiki". Vongozi vijana mnapaswa kuwa wanyenyekevu na kuacha papara. Vinginevyo mtapotea kama walivyopotea viongozi wengine vijana waliopewa madaraka wakakosa unyenyekevu" .

10. "Nawashukuru sana watanzania. Nawashukuru watanzania kwa kunisomesha kwa kodi zao na hatimaye nikaweza kupata shahada zote tatu, kamwe sitawasahau watanzania. Nina deni kubwa la kulipa utumishi uliotukuka. Kazi niliyopewa ya kuwa Mtendaji Mkuu katika chama ni kubwa mno".

KWA hakika, nukuu hizi kuntu zinamtanabaisha Mh. BASHIRU kuwa ni mwanadamu wa aina gani, amedhamiria kuifanya CCM iwe chama cha aina gani na pia viongozi wa serikali ya CCM waweje.

KANYAGA TWENDE, MH. KATIBU MKUU🤙🤙🤙


ALLEZ ALLEZ ALLEZ LIVERPOOL FC: YNWA!!!
Ccm ina wenyewe....
 
Back
Top Bottom