Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,316
- 33,125
Ramadhan Semtawa
WAZIRI mwandamizi katika serikali ya awamu ya pili na tatu, Arcado Ntagazwa, ameshauri mawaziri wasiwe wabunge ili kutenganisha nguvu za bunge na serikali.
Kauli ya Ntagazwa inakuja kipindi ambacho mjadala huo, umeanza kutawala ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), baada ya Kenya kutangaza mabadiliko makubwa ya katiba kuzuia mawaziri wasiwe wabunge.
Ntagazwa akizungumza jana kwa njia ya simu, alisema hatua ya waziri kuwa mbunge inanyima fursa ya uwakilishi mzuri jimboni.
"Unajua kuna jambo la Collective Responsibility (uwajibikaji wa pamoja), mbunge akiwa waziri hawezi kuwakilisha vema matatizo ya jimbo kwa sababu hawezi kuikosoa serikali," alifafanua Ntagazwa wakati akichangia maoni kupitia safu ya Gumzo la Wiki inayochapishwa katika gazeti la Mwananchi Jumapili.
Makala hayo ya Gumzo la Wiki, yalibeba kichwa cha Habari: "Wakati ni huu, mawaziri wasiwe wabunge."
Akitoa maoni yake, alisema kwamba, nchi kama Cameroon, mbunge akishateuliwa kuwa waziri, nafasi take inachukuliwa na mtu wa pili katika matokeo ya uchaguzi.
"Mimi kusema ukweli, ningependa na sisi sasa tuangalie mfumo wetu wa uongozi wa dola, ili tuweze kufumua pale ambapo tunaona kuna mapungufu," alisema Ntangazwa.
Alisema wananchi wanapaswa kuwasilishwa vema majimboni kwao, lakini fursa hiyo, haiwezi kutimia vema kama mbunge atakuwa ni sehemu ya serikali kwa maana ya waziri.
Ntagazwa alisema mfumo wa waziri kutokuwa mbunge umekuwa ukitumika pia katika katiba ya Rwanda, ambayo waziri anapoitwa bungeni hujikuta katika wakati mgumu kama atakuwa haifahamu vema wizara yake.
Tayari mawaziri wawili wamepoteza kazi zao nchini Rwanda baada ya kushindwa kujibu vema maswali ya wabunge bungeni, licha ya kuitwa zaidi ya mara tatu.
WAZIRI mwandamizi katika serikali ya awamu ya pili na tatu, Arcado Ntagazwa, ameshauri mawaziri wasiwe wabunge ili kutenganisha nguvu za bunge na serikali.
Kauli ya Ntagazwa inakuja kipindi ambacho mjadala huo, umeanza kutawala ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), baada ya Kenya kutangaza mabadiliko makubwa ya katiba kuzuia mawaziri wasiwe wabunge.
Ntagazwa akizungumza jana kwa njia ya simu, alisema hatua ya waziri kuwa mbunge inanyima fursa ya uwakilishi mzuri jimboni.
"Unajua kuna jambo la Collective Responsibility (uwajibikaji wa pamoja), mbunge akiwa waziri hawezi kuwakilisha vema matatizo ya jimbo kwa sababu hawezi kuikosoa serikali," alifafanua Ntagazwa wakati akichangia maoni kupitia safu ya Gumzo la Wiki inayochapishwa katika gazeti la Mwananchi Jumapili.
Makala hayo ya Gumzo la Wiki, yalibeba kichwa cha Habari: "Wakati ni huu, mawaziri wasiwe wabunge."
Akitoa maoni yake, alisema kwamba, nchi kama Cameroon, mbunge akishateuliwa kuwa waziri, nafasi take inachukuliwa na mtu wa pili katika matokeo ya uchaguzi.
"Mimi kusema ukweli, ningependa na sisi sasa tuangalie mfumo wetu wa uongozi wa dola, ili tuweze kufumua pale ambapo tunaona kuna mapungufu," alisema Ntangazwa.
Alisema wananchi wanapaswa kuwasilishwa vema majimboni kwao, lakini fursa hiyo, haiwezi kutimia vema kama mbunge atakuwa ni sehemu ya serikali kwa maana ya waziri.
Ntagazwa alisema mfumo wa waziri kutokuwa mbunge umekuwa ukitumika pia katika katiba ya Rwanda, ambayo waziri anapoitwa bungeni hujikuta katika wakati mgumu kama atakuwa haifahamu vema wizara yake.
Tayari mawaziri wawili wamepoteza kazi zao nchini Rwanda baada ya kushindwa kujibu vema maswali ya wabunge bungeni, licha ya kuitwa zaidi ya mara tatu.