NSSF yaelekea kufilisika

Baada ya kuona hali ngumu na wanashindwa kulipa mikopo...Wanata kuleta sheria ya kipuuzi ya miaka 55 mpaka 60 ndio upate Mkwanja wako.
 
CAG nae ni mnafiki tu! kwa sababu kunawakati wanafunzi wa UDOM waligoma na dai moja wapo ni kuwa estate manager na mkuu wa finance ambaye ni maarufu kama Porf Mlacha wanatumia pesa za ujenzi kwa manufaa yao!

Mfano malacha amechukua viti vya chuo cha dodoma na kupeleka kwenye shule yake alikanjenje makanya same! n.k, huyu estate manager kajenga mijengo kibao ya zaidi ya 100mil kwa kila 1,moja wapo lipo msuguli mbezi ambapo nicollage inaitwa mlimani school of business!


Lakini CAG alipo kagua mahesabu akapitisha kuwa wako sahihi tu na hakuna ubadhilifu wowote, sasa iweje leo akubaliane na kusema kuna makosa ya kimahesabu ujenzi wa chuo cha dodoma!

Kifupi CAG mwizi, mifuko ya jamii nao wizi walioufanya kwa muda mrefu kwa kuibeba serikali hata vitu visivyo wahusu kama makampeni! ndio hii sasa! nabado kunamwashirika kibao tu! mwisho wa siku ata ikulu itabinafsishwa sasa!
 
Hii serikali yetu au imetuchoka sisi wafanyakazi au inatafuta vita na sisi wafanyakazi! mshahara hawaongezi, wametubebesha kodi kubwa, sasa hata kile kiakiba tunachojiwekea ndicho wamekomba? hizi kongwa tutazibeba hadi lini wafanyakazi wenzagu? hapana kwanza tupige chini TUCTA tuweke uongozi thabiti ili tuwe tayari kupambana na hawa mafisadi, sasa hivi wapo busy kuchota mabilioni ya mifuko yetu ili kujijenga kugombea urais 2015!
 
Ndugu zangu mimi niko NSSF Tanga kwa sasa hivi, wamegoma kunipa mafao yangu eti amri hiyo ilianza kutekelezwa kwanzia tarehe 23. ninaadmission ya chuo nilitaka kuchukua hela ili nilipe ada wamegoma kabisa kuanzisha mchakato wa kuchukua hela.

Itabidi tuandamane!
 
hawakuwa wakijua kuna a very thin line between pension fund and pyramid style upatu.sasa ipo siku hata hao wanaofikia umri nao waatakosa hela, na kuna mifuko itafulia sana sasa itabidi sheria iamue tena kuunganisha mifuko.
 
Nimesikia katika taarifa ya habari ya leo 7 mchana redio Uhuru kuwa eti MD wa SSRA amesema wanakusudia kupeleka bungeni muswaada wa marekebisho ya sheria kuhusu mafao na wameamua hivyo baadaad ya kuupokea maalalamiko menfi
 
nchi yeyote ikikaribia kuangamia na kuchafuka inakuwaga hivi hivi.utekaji,kuuana,kusengenyana,kudhulumiana,na kulazimishana.hii ukijumlisha na gharama kubwa ya upatikanaji mgumu wa chakula,kupanda kwa gharama za maisha haya yamezivuruga nchi nyingi sana.wadau nchi yetu haiko sawa yatupasa tuitazame zaidi ya tuionavyo.nawasilisha.
 
CAG nae ni mnafiki tu! kwa sababu kunawakati wanafunzi wa UDOM waligoma na dai moja wapo ni kuwa estate manager na mkuu wa finance ambaye ni maarufu kama Porf Mlacha wanatumia pesa za ujenzi kwa manufaa yao!

Mfano malacha amechukua viti vya chuo cha dodoma na kupeleka kwenye shule yake alikanjenje makanya same! n.k, huyu estate manager kajenga mijengo kibao ya zaidi ya 100mil kwa kila 1,moja wapo lipo msuguli mbezi ambapo nicollage inaitwa mlimani school of business!


Lakini CAG alipo kagua mahesabu akapitisha kuwa wako sahihi tu na hakuna ubadhilifu wowote, sasa iweje leo akubaliane na kusema kuna makosa ya kimahesabu ujenzi wa chuo cha dodoma!

Kifupi CAG mwizi, mifuko ya jamii nao wizi walioufanya kwa muda mrefu kwa kuibeba serikali hata vitu visivyo wahusu kama makampeni! ndio hii sasa! nabado kunamwashirika kibao tu! mwisho wa siku ata ikulu itabinafsishwa sasa!

Mkuu, si estate manager wala finance manager wala kiongozi yoyote wa UDOM anayehusika kwa namna yoyote kwenye hela za ujenzi wa hicho chuo. Majengo yote yanajengwa kwa hela za mifuko ya jamii (NSSF, PPF, etc) na wasimamizi wote wanatoka kwenye mashirika hayo, wakandarasi na washauri ujenzi wote wako chini ya hayo mashirika. Hao viongozi wa UDOM wanakabidhiwa Majengo tu, hawajui chochote juu ya pesa za hayo majengo unawaonea tuu.
Kama kula hela basi ni zingine tu labda za usimamizi wa hayo majengo (maintenance costs)
 
mkuu, si estate manager wala finance manager wala kiongozi yoyote wa udom anayehusika kwa namna yoyote kwenye hela za ujenzi wa hicho chuo. Majengo yote yanajengwa kwa hela za mifuko ya jamii (nssf, ppf, etc) na wasimamizi wote wanatoka kwenye mashirika hayo, wakandarasi na washauri ujenzi wote wako chini ya hayo mashirika. Hao viongozi wa udom wanakabidhiwa majengo tu, hawajui chochote juu ya pesa za hayo majengo unawaonea tuu.
Kama kula hela basi ni zingine tu labda za usimamizi wa hayo majengo (maintenance costs)

ni kweli! Ila hizo pesa hata kama niza maintenance zinatokea huko! Napia hawawezi kufanya ujenzi bila finance officer wa chuo pia kuweka kwenye board yao,napia kunatenda za kukodisha majengo kwa biashara na ni majengo yaliojengwa na mifuko hii! Lakini tenda inapitishwa na uongozi wa chuo! Mkuu yani kwa vyovyote hawa jamaa wanashirikiana tu kwenye kuiba! Mana hata chuo kina maengeneer wake, yale matank ya maji ya chuo ni tenda mlacha kampa shemejie, je? Hela za kuwekea matank zinatokea wapi ka si kwa mifuko hii! Yani hii ni chai kama kawaida ya ubadhilifu wa fedha walivo! Alafu kwenye return za chuo kwa mifuko hii kupitia serikali! Bado watu wanakata mzigo! Ndo mana wanakwamia mahesabu hayaendi vzr! Inamaana cag hapitii hii kitu! Wanabebana tu mkuu hawa jamaa! Miradi iko kisiasa zaidi,kuwasafishia watu njia! Wewe waangalie nhif ndo best africa mashariki na kati mpaka kenya walikuja kufanya study huu mfuko unavyoendeshwa! Na wanatuzo hiyo!
 
Wafanyakazi popote tulipo tushikamane pamoja, huu ni unyanyasaji wa hali ya juu wa serikali, tukizingatia Kikwete alishawahi kusema hana shida na kura za wafanyakazi!
 
Jamani hii nchi visiasa vitatuangamiza. Angalia taarifa ya hatari ya kufilisika mifulo ya jamii.Na kutokana na madeni ndio maana serikali inawazuia watu wasipate mafao kabla ya muda wa kustaafu. Chadema na vyama vya wafanyakazi jipangeni kupinga



MFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) uko hatarini kufilisika na
kupoteza fedha za wanachama wake.

Hii inatokana na serikali kushindwa kurejesha katika mfuko huu, mabilioni
ya shilingi iliyokopa au kudhamini katika miradi mbalimbali.

Kwa mujibu wa Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
(CAG) ya 2010/2011, fedha za wanachama, hata katika mifuko mingine ya
jamii, ziko hatarini kupotea.

Mbali na NSSF, mifuko mingine inayotajwa kuwa katika hatari hiyo ni Mfuko
wa Pensheni wa Mashirika ya Umma (PPF); Mfuko wa Wafanyakazi wa Serikali
Kuu (PSPF), Mfuko wa Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (LAPF) na Mfuko wa
Bima ya Afya (NHIF).

Kulingana na taarifa ya CAG, sehemu kubwa ya fedha za wanachama ambazo
hazijarejeshwa, zilikopeshwa kwa serikali kwa ajili ya ujenzi wa Chuo
Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Katika chuo hiki, NSSF peke yake iliingiza Sh. 234.1 bilioni. Mifuko
iliyosalia ilitoa jumla ya Sh. 181.3 bilioni.

Katika ujenzi wa UDOM, PPF ilitoa Sh. 39.99 bilioni, PSPF (Sh. 105.9
bilioni), LAPF (Sh. 22 bilioni) na NHIF (Sh. 13.4 bilioni). Fedha hizo na
riba yake hazijarejeshwa.

Ripoti ya CAG, Ludovick Utouh, inasema kutorejeshwa kwa mikopo hiyo,
iliyochukuliwa au kudhaminiwa na serikali, ni kinyume cha sheria ya
udhamini ya mwaka 1974.

“Kutolipika kwa mikopo hii iliyodhaminiwa na serikali kunaiweka mifuko
hii ya hifadhi katika hatari ya kupoteza fedha za wanachama na kuhatarisha
uwezo wa mifuko kufanya uwekezaji zaidi,” anasema na kuongeza:

“Kushindwa kulipa madeni taasisi hizi ambazo baadhi yake zilipata
udhamini wa serikali, kunatia shaka iwapo upembuzi wa kina wa wakopaji
ulifanywa na mifuko ya kijamii kabla ya kutoa mikopo hiyo.”

Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk. Ramadhan Dau hakupatikana kwa maelezo kuwa
alikuwa kwenye mkutano mkoani Mbeya.

Lakini Meneja Kiongozi Uhusiano wa NSSF, Eunice Chiume amesema mikopo kwa
serikali imetolewa kwa uangalifu na inalipwa bila matatizo na kwa misingi
ya kibiashara.

“Mikataba ya kisheria imesainiwa kukidhi mazingira mbalimbali ikiwa ni
pamoja na iwapo itacheleweshwa…. Hakuna hatari yoyote ya fedha kutolipwa
wala kupoteza fedha za wateja,” amesema Chiume.

Lakini CAG katika taarifa yake ya kurasa 183, anasema, “Ukubwa wa
kibiashara kati ya serikali na mifuko unatia shaka kutokana na kusuasua
kwa serikali katika ulipaji madeni yake. Hii inahatarisha uendelevu wa
mifuko hii.”

Katika ukaguzi wake, CAG amebaini kuwa NSSF ilitoa Sh. 234.1 bilioni kwa
mradi wa UDOM, lakini mkataba uliosainiwa ni wa Sh. 35.2 bilioni tu. Hii
ni hatari kwa fedha za wafanyakazi na wastaafu.

Akifafanua suala la fedha kwenye mkataba kutofautiana na fedha
zilizotolewa, Chiume alisema mkataba ulitakiwa kuwa mmoja ambao ulisainiwa
wakati wa awamu ya kwanza.

Chiume alisema kwa awamu ya pili, kilichotakiwa ni kusaini addendum
(makubaliano ya nyongeza), ambayo “yako mbioni kukamilika.”

Utouh anaripoti, “Majengo kwa ajili ya awamu ya kwanza yalikamilika na
kuwekwa katika matumizi mwezi Septemba 2008. Mpaka wakati wa ukaguzi
2010/2011, mfuko ulikuwa haujafanikiwa kukusanya malipo ya pango kutoka
serikalini.

Kwa msingi huo, hadi sasa limbikizo la riba limefika thamani ya Sh. 14
bilioni,” anasema Utouh.

Mkopo huo ulitolewa kwa utaratibu wa kubuni, kujenga, kumiliki na
kuhamisha ambapo mfuko ungepokea kodi iliyokokotolewa kwa riba ya asilimia
15 kwa kipindi cha miaka kumi.

Vilevile CAG amebaini kuwa majengo yaliyojengwa kwa mkopo huo, hayako
kwenye vitabu vya UDOM wala katika vitabu vya NSSF, kutokana na uelewa
tofauti uliopo kati ya pande mbili zinazohusika.

Kuna mikanganyiko katika uelewa kwa serikali na mifuko ya hifadhi,
ameeleza CAG. Wakati mifuko inasema fedha zilizotumika kujenga majengo
hayo zilikuwa mikopo kwa serikali, yenyewe serikali inadai fedha hizo ni
uwekezaji wa kawaida wa mifuko hiyo.

Mbali na UDOM, serikali pia haijalipa jumla ya Sh. 19.77 bilioni
zilizotumika katika ujenzi wa ukumbi wa bunge, ambazo hazilipwi kulingana
na makubaliano. Hadi wakati wa ukaguzi, NSSF ilikuwa inadai Sh. 8.96
bilioni, PPF (Sh. 7.9 na LAPF Sh. 2.91.

Pia upo mkopo mwingine wa NSSF wa Sh. 5.33 bilioni na riba ya asilimia 15
kwa miaka kumi, uliotolewa kwa ajili ya ujenzi wa “taasisi ya serikali
ya kiusalama” mwaka 2007.

Mfuko mwingine uliowekeza katika mradi huo ni PSPF uliotoa Sh. 6.4 bilioni.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, NSSF kwa udhamini wa serikali ilikopesha
taasisi kwa shughuli mbalimbali.

Kwa mfano, ujenzi wa nyumba za polisi kwa Sh. 20 bilioni na Sh. 12. 9
bilioni kwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam mwaka 2007 kwa ajili ya
ujenzi wa Machinga Complex, Ilala.

“Hadi sasa hakuna malipo ya riba wala sehemu ya mkopo hiyo yaliyofanywa.
Hii ni kinyume cha mkataba,” inasema sehemu ya ripoti ya CAG.

Kwa upande wa Machinga Complex, hadi tarehe 30 Juni 2011, mkopo na riba
yake ulikuwa umefikia Sh. 15.3 bilioni.

Ripoti ya CAG imeainisha pia mikopo mingine ambayo hailipwi kulingana na
mikataba ya mifuko hiyo, bila ya kutaja viwango vyake.

Mikopo hiyo ni iliyotolewa kwa Continental Venture (T) Limited, Meditech
Industrial Co. Ltd, General Tyre (GT), Kiwanda cha Sukari Kagera, Bodi ya
Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) na mgodi wa mkaa wa mawe wa Kiwira, mkoani
Mbeya.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa PPF, William Erio amesema hajaona
ripoti ya CAG na yuko safarini Tanga.

Hata hivyo amedokeza kuwa hivi karibuni walikaa na CAG kujadili suala hilo
na kubaini makosa ya kifundi katika uhasibu baina ya mifuko na serikali
katika ujenzi wa UDOM; hivyo CAG kuahidi kuyashughulikia kwa upande wa
serikali.

Alipoulizwa ni makosa yapi hayo, Erio alimtaka mwandishi awasiliane na
kaimu wake, Stephen Alfred ambaye ilielezwa kuwa yuko kwenye mkutano. Hadi
tunakwenda mitamboni, Alfred hakupatikana.
 
Kama serikali ilikopa kwenye hiyo mifuko na mifuko itafute sehemu ya kukopa ili mwanachama anapoacha kazi apewe chake la sivo itafika mahali sasa nchi hii isiwe sehemu salama kutokana na sheria kandamizi zinazotungwa kwa maslahi ya watu flani.Hela yangu utaitungieje sheria? wakati naitafuta tulikuwa wote
 
Nimesoma mpaka nikaogopa. Hata mfuko wa bima ya afya unakopwa ni hatari sana. Hii nchi inaongoza na majambazi. Bora tufute hii mifuko kila mtu apwewe chake kama vibarua
 
kwa hakika tumeangalia haya matatizo ya kisheria zaidi na uzembe lakini huenda kuna tatizo liliko kubwa zaidi nalo hata hatujalifikiria. Hili linaweza kuwa lile linalotafuna Billion 9 kila mwaka (stand to be corrected) kwenye 'ghost workers'. Hili sasa limeibukia kwenye NSSF ya Uganda na naamini hata hapa inawezekana ikawa inaendelea chinichini kwa walipwa mafao hewa.

Soma hii ya Uganda.

Shs60 billion pension paid to 1,000
[h=1]Shs60 billion pension paid to 1,000 ‘ghosts’[/h]
A police investigation is closing-in on a racket of senior staff in the ministries of Public Service and Finance who paid out at least Sh63 billion to 1,000 ghost pensioners last year.



The money was paid out between February and November as gratuity but detectives have established that the beneficiaries were all non-existent.


CID chief Grace Akullo confirmed yesterday she was investigating the scam and senior Public Service officials are expected to make statements today. Download List of ghost pensioners.
Detectives have since Wednesday been sifting through documents at the Ministry of Public Service, sparking off panic.

This year, the government allocated Shs63.9b for teachers’ pension, which could have been cleared had the money squandered last year been put to intended use.

It would have also cleared Local Government pensions and civil service gratuity combined whose estimates this year is Shs36.6 billion and Shs34.1 billion, respectively.

A senior official in the Finance ministry said last evening that while the overall pension arrears vacillates between Shs250b to Shs300b, it was “difficult to quantify the actual arrear figures because of the mess in Public Service ministry.”
 
Mhh nakumbuka angalizo la Mheshimiwa Ngongo hii mifuko inatakiwa uwakilishi mzito wa wafanyakazi wenyewe.
 
Ni kweli NSSF iko taabani lakini sababu ni nyingi moja kubwa ni hili swala la kugharamia uendeshaji wa serekali lingine ni miradi yake mingi haina tija na kujikuta fedha zake nyingi zikipotea bure.Mradi wa ujenzi wa UDOM umechota fedha nyingi wakati hata mkataba haujasainiwa,miradi ya majengo mengi ni kwaajili ya ulaji wa wakubwa.Chama cha wafanyakazi wa sekta mbali mbali yafaa waungane kupinga uonevu wa wafanyakazi unaandaliwa chini ya mwavuli wa kuficha utawala mbovu wa serekali ya CCM.
Kinachoimaliza nssf ni miradi fictitious,over inflated ya garama za miradi,usanii wa ujenzi was shule ya michezo na real Madrid ambao nasikia wametapeliwa na watafikishwa mahakamani,udini ulopitiliza,over employment na mabosi kujitajirisha kupita kiasi na ndugu zao,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom