NSSF yaelekea kufilisika

Hiyo ripoti ya shirika la NSSF ikijibu gazeti la Mwanahalisi nafikiri inapotosha. "Unqualified Report" haina uhusiano na kufilisika au kutokufilisika bali kama mahesabu yanatoa picha halisi ya shirika. Hata hivyo, naamini Mkaguzi inabidi aandike ripoti ingine kuhusu "Going Concern" (i.e uwezekano wa kufilisika au kutofilisika) ya shirika analolikagua ambayo nafikiri hiyo ripoti ni sehemu ya ripoti ya Manajementi na haihusu jinsi uwekaji wa mahesabu ulivyokuwa. Ni tofauti na "Auditor's Opinion". Sasa NSSF wanapotumia ripoti inayohusu jinsi mahesabu yao yanavyowekwa kama sababu ya kujenga hoja kuwa shirika halifilisiki, ni kupotosha umma. Watupe Management Report ya Wakaguzi.

Kama huoni kwa macho basi walau papasa! yaani hii hukuiona!

NSSF hatarini kufilisika

Kuhusu dai kuwa NSSF ipo hatarini kufilisika, hii pia si kweli. Kipimo kizuri cha uwezo wa kifedha wa mfuko (financial soundness) ni Tathmini ya Mfuko yaani Actuarial Valuation ambayo inafanywa kila baada ya miaka 3. Kwa upande wa NSSF, Actuarial Valuation ya mwisho ni ya mwaka 2010.

Zoezi hili lilifanywa na Kampuni ya xxxxxxx kutoka Canada ambayo mwaka xxxxx iliteuliwa na Shirika la Kazi Duniani yaani International Labour Organisation (ILO) kufanya Tathmini ya Shirika la NSSF. Matokeo ya Actuarial Valuation inayoishia mwaka 2010, yanaonyesha kuwa Reserve Ratio ya NSSF ni 6.8. Tafsiri ya matokeo haya ni kuwa NSSF inaweza kumudu kulipa mafao YOTE kwa wanachama na kulipa gharama ZOTE za uendeshaji kwa miaka 6.8 bila kuingiza hata senti moja kwa maana ya ukusanyaji wa michango au mapato kutokana na vitega uchumi.
 
When the Gov't is dead this is part of orders of the day!,More are still to come,Let's wait n' see what's next!
 
Silaha pekee tuliyonayo wafanyakazi Tanzania dhidi ya sheria hii kandamizi ni kufanya mambo yafuatayo.

[1] Kuandaa mgomo nchi nzima ili kushinikiza serekali kuifuta sheria hii mbaya.

[2] kuandaa maandamano ya amani mikoa na wilaya zote Tanzania.

[3] kutafuata wanasheria mahiri kwaajili ya kuipinga sheria hii mahakamani.

Harlod Sungusia na LHRC washaanza
 
Nileteeni kiboko,kuna mtu niliwahi kusikia akiropoka eti dhaifu ni chaguo la Mungu! Najiuliza: Mungu wanayemjua wao ni yupi? Najua Mungu huyu aliyeumba mbingu,dunia na tunae muabudu hajawahi kufanya ujinga na hawezi kuanza kwa kumchagua Kikwe kuwa rais wa wadanganyika!
 
Suluhisho ni kujiajiri tu, siku zote masikini hana chake na sheria zote duniani zimeundwa ili kuwalinda matajiri.

yaani kati ya wote wewe ndo umenena! ngoja nilifanyie kazi wazo lako..maana kusubiria pension mil 100-200 miaka 30 ijayo kwangu haiwezekani
 
MFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) uko hatarini kufilisika na kupoteza fedha za wanachama wake.

Hii inatokana na serikali kushindwa kurejesha katika mfuko huu, mabilioni ya shilingi iliyokopa au kudhamini katika miradi mbalimbali.

Kwa mujibu wa Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya 2010/2011, fedha za wanachama, hata katika mifuko mingine ya jamii, ziko hatarini kupotea.


Mbali na NSSF, mifuko mingine inayotajwa kuwa katika hatari hiyo ni Mfuko wa Pensheni wa Mashirika ya Umma (PPF); Mfuko wa Wafanyakazi wa Serikali Kuu (PSPF), Mfuko wa Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (LAPF) na Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF).


Kulingana na taarifa ya CAG, sehemu kubwa ya fedha za wanachama ambazo hazijarejeshwa, zilikopeshwa kwa serikali kwa ajili ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).


Katika chuo hiki, NSSF peke yake iliingiza Sh. 234.1 bilioni. Mifuko iliyosalia ilitoa jumla ya Sh. 181.3 bilioni.


Katika ujenzi wa UDOM, PPF ilitoa Sh. 39.99 bilioni, PSPF (Sh. 105.9 bilioni), LAPF (Sh. 22 bilioni) na NHIF (Sh. 13.4 bilioni). Fedha hizo na riba yake hazijarejeshwa.


Ripoti ya CAG, Ludovick Utouh, inasema kutorejeshwa kwa mikopo hiyo, iliyochukuliwa au kudhaminiwa na serikali, ni kinyume cha sheria ya udhamini ya mwaka 1974.


“Kutolipika kwa mikopo hii iliyodhaminiwa na serikali kunaiweka mifuko hii ya hifadhi katika hatari ya kupoteza fedha za wanachama na kuhatarisha uwezo wa mifuko kufanya uwekezaji zaidi,” anasema na kuongeza:


“Kushindwa kulipa madeni taasisi hizi ambazo baadhi yake zilipata udhamini wa serikali, kunatia shaka iwapo upembuzi wa kina wa wakopaji ulifanywa na mifuko ya kijamii kabla ya kutoa mikopo hiyo.”


Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk. Ramadhan Dau hakupatikana kwa maelezo kuwa alikuwa kwenye mkutano mkoani Mbeya.


Lakini Meneja Kiongozi Uhusiano wa NSSF, Eunice Chiume amesema mikopo kwa serikali imetolewa kwa uangalifu na inalipwa bila matatizo na kwa misingi ya kibiashara.


“Mikataba ya kisheria imesainiwa kukidhi mazingira mbalimbali ikiwa ni pamoja na iwapo itacheleweshwa…. Hakuna hatari yoyote ya fedha kutolipwa wala kupoteza fedha za wateja,” amesema Chiume.


Lakini CAG katika taarifa yake ya kurasa 183, anasema, “Ukubwa wa kibiashara kati ya serikali na mifuko unatia shaka kutokana na kusuasua kwa serikali katika ulipaji madeni yake. Hii inahatarisha uendelevu wa mifuko hii.”


Katika ukaguzi wake, CAG amebaini kuwa NSSF ilitoa Sh. 234.1 bilioni kwa mradi wa UDOM, lakini mkataba uliosainiwa ni wa Sh. 35.2 bilioni tu. Hii ni hatari kwa fedha za wafanyakazi na wastaafu.


Akifafanua suala la fedha kwenye mkataba kutofautiana na fedha zilizotolewa, Chiume alisema mkataba ulitakiwa kuwa mmoja ambao ulisainiwa wakati wa awamu ya kwanza.


Chiume alisema kwa awamu ya pili, kilichotakiwa ni kusaini addendum (makubaliano ya nyongeza), ambayo “yako mbioni kukamilika.”


Utouh anaripoti, “Majengo kwa ajili ya awamu ya kwanza yalikamilika na kuwekwa katika matumizi mwezi Septemba 2008. Mpaka wakati wa ukaguzi 2010/2011, mfuko ulikuwa haujafanikiwa kukusanya malipo ya pango kutoka serikalini.


Kwa msingi huo, hadi sasa limbikizo la riba limefika thamani ya Sh. 14 bilioni,” anasema Utouh.


Mkopo huo ulitolewa kwa utaratibu wa kubuni, kujenga, kumiliki na kuhamisha ambapo mfuko ungepokea kodi iliyokokotolewa kwa riba ya asilimia 15 kwa kipindi cha miaka kumi.


Vilevile CAG amebaini kuwa majengo yaliyojengwa kwa mkopo huo, hayako kwenye vitabu vya UDOM wala katika vitabu vya NSSF, kutokana na uelewa tofauti uliopo kati ya pande mbili zinazohusika.


Kuna mikanganyiko katika uelewa kwa serikali na mifuko ya hifadhi, ameeleza CAG. Wakati mifuko inasema fedha zilizotumika kujenga majengo hayo zilikuwa mikopo kwa serikali, yenyewe serikali inadai fedha hizo ni uwekezaji wa kawaida wa mifuko hiyo.


Mbali na UDOM, serikali pia haijalipa jumla ya Sh. 19.77 bilioni zilizotumika katika ujenzi wa ukumbi wa bunge, ambazo hazilipwi kulingana na makubaliano. Hadi wakati wa ukaguzi, NSSF ilikuwa inadai Sh. 8.96 bilioni, PPF (Sh. 7.9 na LAPF Sh. 2.91.


Pia upo mkopo mwingine wa NSSF wa Sh. 5.33 bilioni na riba ya asilimia 15 kwa miaka kumi, uliotolewa kwa ajili ya ujenzi wa “taasisi ya serikali ya kiusalama” mwaka 2007.


Mfuko mwingine uliowekeza katika mradi huo ni PSPF uliotoa Sh. 6.4 bilioni.


Kwa mujibu wa ripoti hiyo, NSSF kwa udhamini wa serikali ilikopesha taasisi kwa shughuli mbalimbali.


Kwa mfano, ujenzi wa nyumba za polisi kwa Sh. 20 bilioni na Sh. 12. 9 bilioni kwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam mwaka 2007 kwa ajili ya ujenzi wa Machinga Complex, Ilala.


“Hadi sasa hakuna malipo ya riba wala sehemu ya mkopo hiyo yaliyofanywa. Hii ni kinyume cha mkataba,” inasema sehemu ya ripoti ya CAG.


Kwa upande wa Machinga Complex, hadi tarehe 30 Juni 2011, mkopo na riba yake ulikuwa umefikia Sh. 15.3 bilioni.


Ripoti ya CAG imeainisha pia mikopo mingine ambayo hailipwi kulingana na mikataba ya mifuko hiyo, bila ya kutaja viwango vyake.


Mikopo hiyo ni iliyotolewa kwa Continental Venture (T) Limited, Meditech Industrial Co. Ltd, General Tyre (GT), Kiwanda cha Sukari Kagera, Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) na mgodi wa mkaa wa mawe wa Kiwira, mkoani Mbeya.


Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa PPF, William Erio amesema hajaona ripoti ya CAG na yuko safarini Tanga.


Hata hivyo amedokeza kuwa hivi karibuni walikaa na CAG kujadili suala hilo na kubaini makosa ya kifundi katika uhasibu baina ya mifuko na serikali katika ujenzi wa UDOM; hivyo CAG kuahidi kuyashughulikia kwa upande wa serikali.


Alipoulizwa ni makosa yapi hayo, Erio alimtaka mwandishi awasiliane na kaimu wake, Stephen Alfred ambaye ilielezwa kuwa yuko kwenye mkutano. Hadi tunakwenda mitamboni, Alfred hakupatikana.


 
MFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) uko hatarini kufilisika na kupoteza fedha za wanachama wake.

Hii inatokana na serikali kushindwa kurejesha katika mfuko huu, mabilioni ya shilingi iliyokopa au kudhamini katika miradi mbalimbali.

Kwa mujibu wa Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya 2010/2011, fedha za wanachama, hata katika mifuko mingine ya jamii, ziko hatarini kupotea.


Mbali na NSSF, mifuko mingine inayotajwa kuwa katika hatari hiyo ni Mfuko wa Pensheni wa Mashirika ya Umma (PPF); Mfuko wa Wafanyakazi wa Serikali Kuu (PSPF), Mfuko wa Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (LAPF) na Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF).


Kulingana na taarifa ya CAG, sehemu kubwa ya fedha za wanachama ambazo hazijarejeshwa, zilikopeshwa kwa serikali kwa ajili ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).


Katika chuo hiki, NSSF peke yake iliingiza Sh. 234.1 bilioni. Mifuko iliyosalia ilitoa jumla ya Sh. 181.3 bilioni.


Katika ujenzi wa UDOM, PPF ilitoa Sh. 39.99 bilioni, PSPF (Sh. 105.9 bilioni), LAPF (Sh. 22 bilioni) na NHIF (Sh. 13.4 bilioni). Fedha hizo na riba yake hazijarejeshwa.


Ripoti ya CAG, Ludovick Utouh, inasema kutorejeshwa kwa mikopo hiyo, iliyochukuliwa au kudhaminiwa na serikali, ni kinyume cha sheria ya udhamini ya mwaka 1974.


“Kutolipika kwa mikopo hii iliyodhaminiwa na serikali kunaiweka mifuko hii ya hifadhi katika hatari ya kupoteza fedha za wanachama na kuhatarisha uwezo wa mifuko kufanya uwekezaji zaidi,” anasema na kuongeza:


“Kushindwa kulipa madeni taasisi hizi ambazo baadhi yake zilipata udhamini wa serikali, kunatia shaka iwapo upembuzi wa kina wa wakopaji ulifanywa na mifuko ya kijamii kabla ya kutoa mikopo hiyo.”


Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk. Ramadhan Dau hakupatikana kwa maelezo kuwa alikuwa kwenye mkutano mkoani Mbeya.


Lakini Meneja Kiongozi Uhusiano wa NSSF, Eunice Chiume amesema mikopo kwa serikali imetolewa kwa uangalifu na inalipwa bila matatizo na kwa misingi ya kibiashara.


“Mikataba ya kisheria imesainiwa kukidhi mazingira mbalimbali ikiwa ni pamoja na iwapo itacheleweshwa…. Hakuna hatari yoyote ya fedha kutolipwa wala kupoteza fedha za wateja,” amesema Chiume.


Lakini CAG katika taarifa yake ya kurasa 183, anasema, “Ukubwa wa kibiashara kati ya serikali na mifuko unatia shaka kutokana na kusuasua kwa serikali katika ulipaji madeni yake. Hii inahatarisha uendelevu wa mifuko hii.”


Katika ukaguzi wake, CAG amebaini kuwa NSSF ilitoa Sh. 234.1 bilioni kwa mradi wa UDOM, lakini mkataba uliosainiwa ni wa Sh. 35.2 bilioni tu. Hii ni hatari kwa fedha za wafanyakazi na wastaafu.


Akifafanua suala la fedha kwenye mkataba kutofautiana na fedha zilizotolewa, Chiume alisema mkataba ulitakiwa kuwa mmoja ambao ulisainiwa wakati wa awamu ya kwanza.


Chiume alisema kwa awamu ya pili, kilichotakiwa ni kusaini addendum (makubaliano ya nyongeza), ambayo “yako mbioni kukamilika.”


Utouh anaripoti, “Majengo kwa ajili ya awamu ya kwanza yalikamilika na kuwekwa katika matumizi mwezi Septemba 2008. Mpaka wakati wa ukaguzi 2010/2011, mfuko ulikuwa haujafanikiwa kukusanya malipo ya pango kutoka serikalini.


Kwa msingi huo, hadi sasa limbikizo la riba limefika thamani ya Sh. 14 bilioni,” anasema Utouh.


Mkopo huo ulitolewa kwa utaratibu wa kubuni, kujenga, kumiliki na kuhamisha ambapo mfuko ungepokea kodi iliyokokotolewa kwa riba ya asilimia 15 kwa kipindi cha miaka kumi.


Vilevile CAG amebaini kuwa majengo yaliyojengwa kwa mkopo huo, hayako kwenye vitabu vya UDOM wala katika vitabu vya NSSF, kutokana na uelewa tofauti uliopo kati ya pande mbili zinazohusika.


Kuna mikanganyiko katika uelewa kwa serikali na mifuko ya hifadhi, ameeleza CAG. Wakati mifuko inasema fedha zilizotumika kujenga majengo hayo zilikuwa mikopo kwa serikali, yenyewe serikali inadai fedha hizo ni uwekezaji wa kawaida wa mifuko hiyo.


Mbali na UDOM, serikali pia haijalipa jumla ya Sh. 19.77 bilioni zilizotumika katika ujenzi wa ukumbi wa bunge, ambazo hazilipwi kulingana na makubaliano. Hadi wakati wa ukaguzi, NSSF ilikuwa inadai Sh. 8.96 bilioni, PPF (Sh. 7.9 na LAPF Sh. 2.91.


Pia upo mkopo mwingine wa NSSF wa Sh. 5.33 bilioni na riba ya asilimia 15 kwa miaka kumi, uliotolewa kwa ajili ya ujenzi wa “taasisi ya serikali ya kiusalama” mwaka 2007.


Mfuko mwingine uliowekeza katika mradi huo ni PSPF uliotoa Sh. 6.4 bilioni.


Kwa mujibu wa ripoti hiyo, NSSF kwa udhamini wa serikali ilikopesha taasisi kwa shughuli mbalimbali.


Kwa mfano, ujenzi wa nyumba za polisi kwa Sh. 20 bilioni na Sh. 12. 9 bilioni kwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam mwaka 2007 kwa ajili ya ujenzi wa Machinga Complex, Ilala.


“Hadi sasa hakuna malipo ya riba wala sehemu ya mkopo hiyo yaliyofanywa. Hii ni kinyume cha mkataba,” inasema sehemu ya ripoti ya CAG.


Kwa upande wa Machinga Complex, hadi tarehe 30 Juni 2011, mkopo na riba yake ulikuwa umefikia Sh. 15.3 bilioni.


Ripoti ya CAG imeainisha pia mikopo mingine ambayo hailipwi kulingana na mikataba ya mifuko hiyo, bila ya kutaja viwango vyake.


Mikopo hiyo ni iliyotolewa kwa Continental Venture (T) Limited, Meditech Industrial Co. Ltd, General Tyre (GT), Kiwanda cha Sukari Kagera, Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) na mgodi wa mkaa wa mawe wa Kiwira, mkoani Mbeya.


Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa PPF, William Erio amesema hajaona ripoti ya CAG na yuko safarini Tanga.


Hata hivyo amedokeza kuwa hivi karibuni walikaa na CAG kujadili suala hilo na kubaini makosa ya kifundi katika uhasibu baina ya mifuko na serikali katika ujenzi wa UDOM; hivyo CAG kuahidi kuyashughulikia kwa upande wa serikali.


Alipoulizwa ni makosa yapi hayo, Erio alimtaka mwandishi awasiliane na kaimu wake, Stephen Alfred ambaye ilielezwa kuwa yuko kwenye mkutano. Hadi tunakwenda mitamboni, Alfred hakupatikana.


 
Serekali izilipe hizo fedha, hayo mashirika yamekuwa msaada kwa miradi mingi nchini.
 
Haya Mashirika ni ya kitapeli, yananitia uchungu nikikumbuka kifo cha marehemu baba yangu, baada ya kufariki akiwa Mtumishi Serikalini hatukuambulia chochote, hata michango aliyochangia alilipwa kidogo tu wakati alipostaafu. Jamaa yangu alisimamishwa kwa manufaa ya umma miaka ya nyuma eti mpaka afikishe miaka 55, na kwa sasa bado miaka 6
Nawauliza hawa kina William Erio, Mustafa Mkullo, na dr Ramadhani Dau wakurugenzi waliopitia hapo hawaoni ni dhambi kujilipa mamilioni ya Watumishi pesa zao na mbaya zaidi kutumia fedha zao kujenga mijengo ya hasara kwa 10% na huku watumishi pesa zao hazizai kwa 15% ambayo wangepata km wangewekeza katika Mabenki?

Tatizo linakonitisha ni hili ambalo dhahiri tumeliwa na bado daraja la Kigamboni
ilevile CAG amebaini kuwa majengo yaliyojengwa kwa mkopo huo, hayako kwenye vitabu vya UDOM wala katika vitabu vya NSSF,
Kuna mikanganyiko katika uelewa kwa serikali na mifuko ya hifadhi, Wakati mifuko inasema fedha zilizotumika kujenga majengo hayo zilikuwa mikopo kwa serikali, yenyewe serikali inadai fedha hizo ni uwekezaji wa kawaida wa mifuko hiyo.
Mbali na UDOM, serikali pia haijalipa jumla ya Sh. 19.77 bilioni zilizotumika katika ujenzi wa ukumbi wa bunge, ambazo hazilipwi kulingana na makubaliano.
Pia upo mkopo mwingine wa NSSF wa Sh. 5.33 bilioni na riba ya asilimia 15 kwa miaka kumi, uliotolewa kwa ajili ya ujenzi wa "taasisi ya serikali ya kiusalama"

 
Watuweke wazi masuala yote,ile fedha aliyokopa Manji aliirudisha? Wanajifanya hawakopeshi lakini katika kumbukumbu zangu kuna kipindi tetesi zilivuma kuwa waziri mkuu aliyejiuzulu kwa ufisadi pia aliwahi kukopeshwa licha ya kuwa hakuwa mwanachama wa mfuko huo.Kimsingi kuna vigogo wengi tu waliofaidika kupitia mfuko huu wa hifadhi ya jamii haswa kwenye tenda za ukandarasi.Labda kwa kuwa wanasema hii nchi ni shamba la bibi n.k Mi ninachohusia ni kwamba,wafanyakazi wanyongeni lakini haki zao wapeni.
 
Mtu akiuawa live ndiyo NSSF na Serikali watatambua kuwa wafanyakazi walikuwa hawatanii
 
Ninachokiona ni kuwa tayari mifuko ya hifadhi ya jamii imeshafilisika.
kwa sasa haina kabisa uwezo wa kuwalipa wanachama wake akiba walizojiwekea.
Hili ndio limepelekea kutungwa kwa sheria ya kutowalipa wanachama hadi watakapofikia umri miaka 55-60 bila kuzingatia future value ya fedha za wanachama.
Mwisho wa siku wanachama wa mifuko hii watakuwa kama wazee wa iliyokuwa east africa community
 
Pesa nyingi,mabilioni kwa mabilioni,yalichotwa na Serikali kwa 'mipango' yao mbalimbali. Mmoja wa mipango hiyo ni ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma. Vilevile pesa nyingine zimetumika kuimarisha chama.Sasa,mifuko hiyo haina pesa. Haiwezi kuwalipa wanachama wao wanaozihitaji pesa zao sasa.Wanaisubiri Serikali na chama tawala kurejesha 'mikopo' yao.

Uamuzi wa Mifuko hiyo kuzuia malipo ya sasa kwa wanachama wao.Naendelea kukusanya nyaraka juu ya sakata hili ili niziwasilishe hapa.Hatahivyo,huu ndio ukweli.CCM wameamua,Mifuko inatekeleza...
 
wameona hawana pesa za kuwalipa wafanyakazi haki yao, pesa inafisadiwa daily!!

nani ana mkataba na Mungu kwamba atakufa baada ya 55 years!
 
Nafikiri huu ni muda muafaka wa wafanyakazi mashirika binafsi kuwithdraw kuweka hela za pension huko ni bora tupewe tu mojamoja kwa moja au zichanganywe kwenye gratuity
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom