NSSF sio mfuko mzuri kujiunga kwa waajiriwa Wapya

Serendipity

JF-Expert Member
Jan 24, 2009
486
43
Nilitembelea leo ofisi za NSSF Dar es salam zilizopo Ilala karibu na Amana hospital.

Wateja nilio wakuta hapo walikuwa na Khali ya Kukata Tamaa na maisha.
Malalamiko/Manung'uniko yao ni kuhusu mfuko wa NSSF kuwakatisha tamaa wanachama waliostaafu au walioacha kazi kwani Huduma zao Haziridhishi ukilinganisha na mifuko mingine.

Kero kubwa ni pale utakapoanza kufuatilia mafao yako, Madai yako hayatapokelewa mpaka usote mtaani kwa muda wa miezi sita(ni NSSF bylaw) ndipo watakukubalia ufungue madai ya mafao yako kwa mara ya kwanza.

Kero inazidi kukera maana baada ya hiyo miezi sita uliyosota mitaani bila kipato chochote, wakikubali kupokea madai yako wanakupangia tarehe ya mbali(inaweza kuzidi miezi saba) ndio waanze ku process mafao yako. Inasemekana Inaweza kuchukua zaidi ya mwaka mmoja au zaidi bila kulipwa mafao.

Kama Khali itaendelea kuwa hivi basi ni bora vijana wanaoanza ajira wajiunge na mifuko mingine ili kuepuka hii kero ya NSSF.
Mwenye uzoefu kama malalamiko hayo ni ya kweli atueleze kwa kutoa ushuhuda wake hapa jukwaani.
 
Na wanachama wa hiari wanajanga la bima ya afya. Matababu unapangiwa hospitali moja ya kutibiwa. Ukiugua safarini bima haikutambui. Ukikosa dawa hospitali unapotibiwa, hawana maduka ya dawa wanachama kupata huduma ya dawa. Ni shida kubwa!
 
Na wanachama wa hiari wanajanga la bima ya afya. Matababu unapangiwa hospitali moja ya kutibiwa. Ukiugua safarini bima haikutambui. Ukikosa dawa hospitali unapotibiwa, hawana maduka ya dawa wanachama kupata huduma ya dawa. Ni shida kubwa!
NSSF wana bima ya afya?
 
kwani Mkuu ukiacha kazi unalipwa mafao,wabunge wa CCM si waliondoa hii kitu au ipo vp? pia wakikusumbua waone SSRA
 
Mmhh kumbe na nssf pia hawafai mii nlifkiri ppf tuu..... Ila kuna mfanyakazi mwenzangu aliambiwa ivo ivo akae miezi sita kwanza na baada ya miezi sita alivoenda wala hakuzungushwa sana akapata...... Ppf bwana hata hako kaela kako hukapati mpaka ufikishe miaka 55
 
yaani hawafai hata kidogo. kwa wafanyakaz wa serikali wanakatwa asilimia 10 wakati mifuko mingine ni asilimia 5, zaid hawa jamaa mwaka 2014 waliwalaghai watumishi kuwa wanachangia aslimia 5 kumbe ni 10. huu ni utapeli kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kha! hata baada ya Dau kuondoka ??? mie nilidhani na matusi yote na malalamiko yote labda NSSF itazaliwa upya?! ama makubwa haya!
 
mimi nilikuwa na mchuchu nssf.. january 2016 akaniambia mapema kwamba fao la kujitoa linakaribia kufutwa niwahi changu mapema..... kama nina nia ya hizo hela.... nikajilipua nikaacha kazi kabla sijapata kazi ingine nikapewa 21m yangu ndani ya mwezi mmmoja tu... then baada ya kupewa changu nikajenga kajumba kangu kadogo ka vyumba viwili na sebule kwa 16m kalivyoisha tu nikaanza tafuta kazi upya bahati nzuri nikapata ...

so hela yangu ya nssf nailalia now pugu huku kodi nimeshasahau....
 
Mfuko wenye afadhali angalau ni pspf tu.
Ingawa nao una kero zake lakini si kama nssf na ppf.
 
Ila huo ni afadhali mara elfu kuliko PPF.PPF ndo hakufai kabisa.yaani usije ukathubutu.
 
Back
Top Bottom