NSSF: Mtajifunza lini kuwajibika?

NSSF: Mtajifunza lini kuwajibika?

HT

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2011
Posts
1,897
Reaction score
414
Huu mfuko umekuwa kero kwa watumiaji. Sijui uteuzi wa watendaji wake ukoje ila unanipa shaka.

Nimefika mara kadhaa ktk ofisi zao, majibu yao mafupi hayana mantiki ukihoji zaidi utaambiwa "jibu ndio hilo".
pamoja na dharau, hawa watendaji ni wavivu na wazembe.

acha nitoe mfano hai.
kwa takribani wiki au zaidi NSSF Kinondoni iliyopo Ubungo hakuna network. huu ni uzembe wa hali ya juu. kwanza walipaswa kuwa na redundancy. pili walipaswa wawe wamepata mbadala wa ttcl network.

Hawashughulikii kikamilifu kwa kuwa ni wavivu. wanafurahi kuvuna bila kupanda.

kwa sababu ya uzembe huu wateja hawataweza kuchukua pesa hadi mwakani. Lini? haijulikani. mpaka system irudi ndio jibu lao.

Lini NSSF Mtajifunza kuwajibika. kodi zetu ndio mishahara yenu ati!
 
hivi waziri na katibu wake hawana mamlaka ya kuingilia kati na kufanya overhaul?
 
Cheza na Tanzania hii, wako likizo... Wakurugenzi wa NSSF...vijana wenu watawaharibia kazi...haya.

Bado wa2 wanauchungu na fao la kujitoa...
 
Sijakuelewa, je kwa anayechukua cheque? Mfano mtu amepangiwa kwenda kuchukua cheque tarehe 24 hawezi kupata?
 
Vipi umejibiwa na yule Mkurya mwenye kisahara? Mpenda rushwa?
 
Pale hakutakuja kutokea ufanisi mpaka siku wakipunguza waswahili walioko pale maana 85% ya wafanyakazi wa NSSF ni waswahili kwa hiyo mswahili yeye alishazoea kunywa kahawa vibarazani na kupiga soga tu basi
 
Wajanja hao.
Watakuwa wanachelewesha kukulipa ili wapate riba/faida katika kuwekeza pesa zilizotakiwa zilipwe kwa wenyewe. Yaani hapo, kama mtandao una matatizo kwa makusudi au bahati mbaya, hawatafanya juhudi za makusudi kurekebisha tatizo.
 
Sijakuelewa, je kwa anayechukua cheque? Mfano mtu amepangiwa kwenda kuchukua cheque tarehe 24 hawezi kupata?

hiyo watakujibu january tu. wanawalaumu ttcl. kwanini wasitumie network nyingine? voda tigo airtel raha et al.
wazembe tu hawa, usipoteze muda.
 
hiyo watakujibu january tu. wanawalaumu ttcl. kwanini wasitumie network nyingine? voda tigo airtel raha et al.
wazembe tu hawa, usipoteze muda.

wapuuzi hawa!
 
hizi ofisi za nssf zinaruka rushwa - hata wafanyakazi macho yao wanapepesa pepesa, indirectly wanakusumbua ili kama unahitaji that fao urgently either kulipa ada, kodi au holidays then uwapatie cha juu -- jamani is that possible network ikawa off for 2 weeks? what are they doing in the office then?

Kodi za poor Tanzanians watu wanachezea chezea tu - we pay them wao wanapiga ma-story ofisini. "network hamna labda uje mwezi january" aisee.
 
Halafu Dau amekazana kuhonga wahariri. Kuna kitu anaficha
 
Na ukiwapigia simu huwa wanaongea kama hawataki:smile:

inabidi kusafishwe wanaongea kana kwamba taasisi yao na wewe unaomba msaada. ningekuwa rais nafuta wote kazi naanza upya
 
Siku nyingine ukienda mtafute mmoja mwmbie utampa 10% ya hela unayochukua uone atakavyokimbizana na faili lako na utalipwa ghafla.........dawa nikuwa tafutia menejimenti nyingine
 
Huu mfuko umekuwa kero kwa watumiaji. Sijui uteuzi wa watendaji wake ukoje ila unanipa shaka.

Nimefika mara kadhaa ktk ofisi zao, majibu yao mafupi hayana mantiki ukihoji zaidi utaambiwa "jibu ndio hilo".
pamoja na dharau, hawa watendaji ni wavivu na wazembe.

acha nitoe mfano hai.
kwa takribani wiki au zaidi NSSF Kinondoni iliyopo Ubungo hakuna network. huu ni uzembe wa hali ya juu. kwanza walipaswa kuwa na redundancy. pili walipaswa wawe wamepata mbadala wa ttcl network.

Hawashughulikii kikamilifu kwa kuwa ni wavivu. wanafurahi kuvuna bila kupanda.

kwa sababu ya uzembe huu wateja hawataweza kuchukua pesa hadi mwakani. Lini? haijulikani. mpaka system irudi ndio jibu lao.


Lini NSSF Mtajifunza kuwajibika. kodi zetu ndio mishahara yenu ati!
Katika mifuko ya jamii mibovu na yenye watu mizigo wasiojua kabisa customer care ni NSSF,nadhani ni kwasababu hawastrugle kutafuta pesa,huwa zinawafata zenyewe ndio maana wanajisahau sana,shirika la kipuuzi kabisa lile
 
Hivi najiuliza, 'is this possible?'
kaka sisi tunaondika ni wahanga wa hii kitu - hatumchukiii mtu ila wafanye kazi walizoomba. Payment gani inakaa zaidi ya wiki 6 hadi 8 guys!! Yangu mimi ina wiki ya 6 na nimeambiwa nikaangalie 4th January.

Tunadai hela utafikiri wale wazee wastaafu wa ile East Africa bwana kaaa :becky: tupeni pesa zetu tulipe kodi za pango na ada za watoto.
 
Mkuu, pole sana, hawa jamaa ni janga sana na wanaendekeza sana rushwa, na hili wanalijua. Ukitoa 20% haki na nakwambia, hiyo "Network" itarudi faster!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom