PayGod
JF-Expert Member
- Mar 4, 2008
- 1,259
- 57
NSN sasa kuendesha shughuli za Vodacom Send to a friend
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania, imekubaliana na kampuni ya Nokia Siemens Networks (NSN) ili NSN itoe huduma za mtandao kwa niaba ya Vodacom Tanzania.
Chini ya makubaliano hayo, kampuni ya NSN itaendelea kuboresha na kuuendesha mtandao wa Vodacom kwa miaka mitano ijayo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Dietlof Mare, aliwaambia waandishi wa Habari Jijini Jana kwamba wafanyakazi wa Vodacom watahamishiwa kampuni ya NSN.
Mkurugenzi huyo alisema wafanyakazi hao watakao hamishwa watapata fursa ya kuongeza utaalamu zaidi ndani ya NSN.
Alisema njia hiyo ya uendeshaji si mpya na kwamba Vodacom Tanzania itandelea kutafuta njia bora zaidi za uendeshaji ili kuboresha huduma kwa wateja.
Uwezo wa kampuni ya NSN wa kuendesha huduma za ki-mtandao ni mkubwa na utaiwezesha Vodacom Tanzania kuboresha huduma zake za mtandao na hatimaye kuboresha huduma zetu kwa wateja, alisema.
Kutokana na makubaliano hayo NSN itachukua majukumu yote ya mawasiliano ya mtandao pamoja na yale ya mtandao katika kanda za mbalimbali nchini.
Uzoefu wa Nokia Siemens Networks kimataifa utaiwezesha Vodacom Tanzania kufikia malengo yake ya ubora wa mitandao ubora wa huduma kwa mteja na unafuu wa gharama.
NSN ni waendeshaji wakubwa wa huduma za mitandao Duniani ikiwa na inaendesha vituo vya mitandao 830,000 Duniani kote ikiwa na mikataba 222 ya uendeshaji. Vodacom ina vituo 1,000 vya mawasiliano nchi nzima.
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania, imekubaliana na kampuni ya Nokia Siemens Networks (NSN) ili NSN itoe huduma za mtandao kwa niaba ya Vodacom Tanzania.
Chini ya makubaliano hayo, kampuni ya NSN itaendelea kuboresha na kuuendesha mtandao wa Vodacom kwa miaka mitano ijayo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Dietlof Mare, aliwaambia waandishi wa Habari Jijini Jana kwamba wafanyakazi wa Vodacom watahamishiwa kampuni ya NSN.
Mkurugenzi huyo alisema wafanyakazi hao watakao hamishwa watapata fursa ya kuongeza utaalamu zaidi ndani ya NSN.
Alisema njia hiyo ya uendeshaji si mpya na kwamba Vodacom Tanzania itandelea kutafuta njia bora zaidi za uendeshaji ili kuboresha huduma kwa wateja.
Uwezo wa kampuni ya NSN wa kuendesha huduma za ki-mtandao ni mkubwa na utaiwezesha Vodacom Tanzania kuboresha huduma zake za mtandao na hatimaye kuboresha huduma zetu kwa wateja, alisema.
Kutokana na makubaliano hayo NSN itachukua majukumu yote ya mawasiliano ya mtandao pamoja na yale ya mtandao katika kanda za mbalimbali nchini.
Uzoefu wa Nokia Siemens Networks kimataifa utaiwezesha Vodacom Tanzania kufikia malengo yake ya ubora wa mitandao ubora wa huduma kwa mteja na unafuu wa gharama.
NSN ni waendeshaji wakubwa wa huduma za mitandao Duniani ikiwa na inaendesha vituo vya mitandao 830,000 Duniani kote ikiwa na mikataba 222 ya uendeshaji. Vodacom ina vituo 1,000 vya mawasiliano nchi nzima.