NRM UGANDA kama CHADEMA, CCM mmebaki wapi?

NRM UGANDA kama CHADEMA, CCM mmebaki wapi?

Kwani NRM ni chama cha siasa? Acha upunguani wewe. Unakumbuka mara ya mwisho wamefanya uchaguzi lini? Unajua pia ni tangu lini Museveni amekuwa kiongozi wa NRM
Chabruma, NRM katika maana ya vyama vya siasa, ni chama cha siasa. Pengine kwa muundo haitafanana na CCM lakini bado haiiondolei sifa ya kuwa chama cha siasa. Hata CCM haifanani ki muundo na Democrat au Republican vya Marekani; na labour au conservative vya Uingereza, lakini hauwezi kusema hivi ni vyama vya siasa zaidi ya vingine.

Tatizo la vyama vyetu vya siasa Afrika, ni uongozi kung'ang'ania madarakani na kudhani kuwa bila wao hakuna chama au Serikali. Mh. Kaguta Mseveni ni muumini wa hili. Mbabazi alikuwa mtu wake wa karibu sana, na sasa kwa hisia tu (na hata kama ni ukweli) kwamba anataka kumuondoa kwenye urais ambao ameufanya kama ufalme. Akisikia tetesi tu wewe ni adui.

Tofauti njema iliyopo katika hili kwa CCM na Serikali ya Tanzania kwa ujumla inalala hapa kwenye kubadilisha uongozi. Baada ya uongozi wa kwanza wa mwalimu Nyerere, tuliweka utaratibu mzuri tunaouheshimu na kuufuata, wa kubadilisha viongozi. Huko kwingine sivyo ilivyo na inaonekana huko Uganda na hata Zimbabwe.
 
Mkuu,Yoweri Kaguta Museveni ameziita taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari,kuwa Waziri Mkuu wake Amama Mbabazi,ambaye pia ni Katibu Mkuu wa chama kinachotawala Uganda NRM kwamba ni za upotoshaji.
Katika taarifa yake,Kaguta amesisitiza kuwa Mbabazi bado ni katibu wa chama,lakini kwa wadhifa wake wa uwaziri mkuu,anakabiliwa na majukumu mengi,kwa hiyo amemwekea Bw Todwong,waziri asiyekuwa na wizara maalum kama msaidizi wake.

link:Mbabazi is still NRM Secretary General - Museveni
 
NRM ni chama kinacho ongozwa na Dikteta Museveni na Chadema inaongozwa na Dikteta Mbowe!
Hapo ni kweli vipo sawa

hivi kwa akili yako ndogo tu alonayo ya bila hata kwenda shule,unaona ccm imekufanyia mambo makubwa,hapa ndo naamini ccm na ujinga na umasikini ni kitu kimoja.
 
Kwani NRM ni chama cha siasa? Acha upunguani wewe. Unakumbuka mara ya mwisho wamefanya uchaguzi lini? Unajua pia ni tangu lini Museveni amekuwa kiongozi wa NRM

NRM ni genge la kitusi linalotawala uganda sawa na M 23 walivyokuwaa wanafanya uhalifu DRC Ya mashariki
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom