Ilumine
Senior Member
- Dec 27, 2008
- 196
- 4
Leo, jioni hii katika runinga, nimesikia ya kuwa makampuni mawili ya huko ulaya yameshinda zabuni ya kuchapisha fesha/noti mpya za Tanzania. Hawakusema lini utekelezaji utaanza, na lini tutaanza kubadilisha noti tulizonazo nk.
Hoja yangu: Ninajua fika ya kuwa zoezi hili hutumia gharama kubwa sana. Mimi sijui, labda ni kwa sababu ya uelewa wangu mdogo, sijui sababu za msingi hasa zinazotufanya watanzania tuingie katika matumizi makubwa kama hayo. Ninajua, wataalamu wetu wanaweza kutoa maelezo mazuri ya kutujulisha uzuri au faida au lengo zima la zoezi, ambalo kwa vyovyote watasema litasaidia kuuinua uchumi wetu unaochechemea. Yapo mambo makubwa yanayotukaba watanzania kwa sasa, mfano tatizo la mgawo wa Umeme. Mambo kama haya, tunabaki kuyajadili tu bila kuchukua hatua zozote za haraka, tunaendelea namambo mengine ambayo hata yakicheleweshwa hatutaonja utofauti wowote. Noti zetu zina kasoro? au ndio tunauboresha uchumi wetu? Pengine hii ni njia ya kutaka kufanya kamchezo fulani, huku sisi raia tunapigwa changa la macho.
Hoja yangu: Ninajua fika ya kuwa zoezi hili hutumia gharama kubwa sana. Mimi sijui, labda ni kwa sababu ya uelewa wangu mdogo, sijui sababu za msingi hasa zinazotufanya watanzania tuingie katika matumizi makubwa kama hayo. Ninajua, wataalamu wetu wanaweza kutoa maelezo mazuri ya kutujulisha uzuri au faida au lengo zima la zoezi, ambalo kwa vyovyote watasema litasaidia kuuinua uchumi wetu unaochechemea. Yapo mambo makubwa yanayotukaba watanzania kwa sasa, mfano tatizo la mgawo wa Umeme. Mambo kama haya, tunabaki kuyajadili tu bila kuchukua hatua zozote za haraka, tunaendelea namambo mengine ambayo hata yakicheleweshwa hatutaonja utofauti wowote. Noti zetu zina kasoro? au ndio tunauboresha uchumi wetu? Pengine hii ni njia ya kutaka kufanya kamchezo fulani, huku sisi raia tunapigwa changa la macho.