Hivi sisi lini tutakuwa serious!? Nilitegemea website za vyuo ziwe na course & module handbooks ambazo zingeainisha modules zinazosomwa katika kila course na coverage & references kwa kila module. Huyu mtu asingekuja hapa, angejiangalizia zake references za hiyo module, tafuta kitabu (softcopy/hardcopy) mdogomdogo angeanza kukandamiza shule. Hii pia inasaidia kabla ya mtu kufanya application, anakuwa na uwezo wa kufanya survey ya nini anategemea kukisoma katika course na module fulani. Lakini pia course moja UDSM inacoverage tofauti na ukiikuta Tumaini, UDOM, Mzumbe nk, kwa nini msiwaoneshe wateja (w/funzi) mapema wajue kwa nini wachague wapi badala ya wapi. Kuna watu wako makazini, wanataka kubadilisha career, na hawana background nzuri ya wanachotaka kukisoma; wakipata hizi information mapema wanaanza kujisoma vitabu hata kabla ya application. Haya maisha ya kumfanyia mteja surprise yalishapitwa na wakati!!