North Korea says; It will be An All Out War

North Korea says; It will be An All Out War

Mi sijawah shuhudia vita yoyte kubwa....napenda waanze hata kesho il njue hizo nuclear zina uwezo kias gan.
 
Jamaa wanajifanya kukubaliana na mazungumzo ila hawana imani na north korea. wanadai imepita miongo 2 tangu mwaka 1992 wanazungunza ila north korea wanageuka geuka.

So, wanasema dawa ni kuilipua hiyo mitambo ya nuklia na kumchakaza serikali yao
Jiulize tangu 1992 marekani kavamia nchi ngapi? Mbona huko N.K hajaenda wakati huyo ndio mkaidi wa maagizo yao? Saddam alikubali kijinga kuangamiza silaha za sumu na kusitisha miradi yote ya silaha kisha jamaa walipopata uhakika ametii maagizo yote hakuna makombora hatari wala kemikali au silaha za kibaiolojia ndio wakamzushia zengwe kwamba bado zipo wakamvamia na kumuua kisha wanavuna mafuta yao kiulaini. Huku usalama na amani nchini Iraq vikibaki historia ya vitabuni. Kim bora awakazie tu, hatutaki kusikia tena ujinga kama ule wa kuwasikia wamarekani na waingereza wakikili hadharani kwamba waliivamia nchi huru kimakosa ya intelijensia zao.
 
hivi kumbe sayansi inanguvu kuliko uchawi? na kama sio kwann wachawi wa marekani wasiloge mitambo ya nuclear
 
Mipango yote imekamilika kwa zaidi ya 100%; kinachosubiriwa ni signature ya Trump tu wanaume wamchakaze kiduku live. Signature ya Mzee Trump ndicho kitu pekee kilichoiweka dunia kwenye tension ya ajabu kuliko kitu kingine chochote kwa sasa. Hadi Makamu wa Rais wa US kutembelea DMZ na kuongea aliyoyaongea lile ni tangazo la vita kwa zaidi ya 50%. In short, kwa sasa vita haiepukiki tena. Kinachotakiwa ni kuomba isilete madhara makubwa.
Uingie na vitani na NK utaepukaje madhara. Kauli yao umeielewa lakini?!
 
Heshima kwenu wakuu.
Fita ni fita mura.. makamu wa rais wa marekani yuko ziarani katika nchi 4 zikiwepo south korea, japan, indonesia.. wachambuzi wanasema ziara yake inalenga kuweka mambo sawa kwa washirika muhimu hasa kupata maeneo ya ardhi, anga na bahari watakayotumia kumchakaza mkorea. Mike Pence alikaririwa akisema " the era of strategic passion was over" kwamba zama za obama za kuishi kwa makubaliano na ahadi zimekwisha.

Naye mzee trump amesema "mipango yote tayari ipo mezani"

Nao North korea wameweka wazi kuwa wataendelea kufanya majaribio ya silaha na makombora yao 'on weekly, monthly & yearly basis'. Wameonya kwamba endapo U.S.A watadhubutu kutumia jeshi dhidi yao.. basi watajibu mapigo kwa nguvu zote. "We will counter react with all our weapons & missiles using our own style and method; from day one onwards"

North korea wameonya kwamba kamwe hakuna mtu wa kuwaamulia maisha yao. Kwani wanajiamini katika waliyo amua kuyatenda.

Mpaka sasa hakuna nchi yoyote iliyokwisha tangaza kwamba wataunga mkono, upande upi. Ila inasadikika kuwa katika hii vita, marekani ina washirika wengi nyuma yake.

Joto la mapambano linazidi kupanda.
Kama anajiamini kwa nini atafute support? Daud vs Goliath
 
VP Mike Pence anasema "Table for negotiations is open" na akarudia, sasa hapo unapoleta mbwai zako hivi unajua madhara makubwa ya vita kama hizi wewe?
Mazungumzo alianza mika 20 iliyopita. Tatizo north korea hawataki kusimamia makubaliano wanayo ingia. Ndo maana vice president kasema zama za kuvumiliana zimefika mwisho
 
Kuna watu humu wanafikiri yaani Usa akiivamia atamaliza vita kwa siku moja hii inaweza ikachukua muda mrefu sana
karibu vita vyote alivyo pigana mmarekani zilichukua zaidi ya siku zilizokuwa zimepangwa. So, mda mrefu hapo haiepukiki
 
Kama anajiamini kwa nini atafute support? Daud vs Goliath
Katika uwanja wa vita sapoti ni muhimu. Mfano wenzake wanaweza hata kumsaidia kupata taarifa muhimu za kiintelijinsia.

Lakini pia, kubwa zaidi ni ili dunia ione hii vita hapigani marekani mwenyewe, bali ni suala la mataifa mengi wanapinga silaha za nyuklia.
 
Mazungumzo alianza mika 20 iliyopita. Tatizo north korea hawataki kusimamia makubaliano wanayo ingia. Ndo maana vice president kasema zama za kuvumiliana zimefika mwisho
We will never tolerate any More,this rat and cat Games.

G W Bush 2003!
 
Mkuu,
Hayo makombora yanaeza 2pata had huku?
Inasemekana north korea wana makombora yanayoweza kwenda umbali wa kilomita 15,000. hiyo ni sawa na kusema yanaweza kufika kokote pale katika uso wa dunia, endapo wataamua kuelekeza.
 
Huu usemi sidhani wanajali maisha ya watu kwa kweli. Afadhali kuna watu wanaoona beyond wanavyoona Trump and Kim. Other options on the table and not a War. Watakaoumia zaidi ni wasio na hatia kama ni vita kweli.

Baada ya hili sakata la Kim&Trump and how close it got to getting into 'IT', I hope kuna watu wataelewa utaratibu na ukimya wa Obama when it comes to NK. WAR ain't fun people, Nuclaer War to be exact.
 
Back
Top Bottom