North eastern zone examination syndicate (nezes) hovyo!!

Mpigaji

JF-Expert Member
Feb 6, 2011
384
42
Jumatatu tarehe 4/6/2012 wanafunzi wa kidato cha nne kanda ya kaskazini mashariki (TANGA NA KILIMANJARO) mwaka 2012 wataanza mitihani ya Utamilifu (MOCK).Mitihani huandaliwa na NEZES.Kila shule hupeleka orodha ya masomo yaliopo shule husika na idadi ya watahiniwa ili mitihani husika ifungwe na kupelekwa shuleni.Ajabu kabisa kuna mitihani ambayo haipo katika baadhi ya shule,lakini imefungwa na kupelekwa!Sasa huku si ndo kuvujisha mitihani?Kama shule inaondoka na mitihani hiyo,kwa kuwa imefungwa kwa jina la shule husika,lakini masomo hayo hayapo,wasio waadilifu wanaweza kuwapa wanafunzi wanaosoma masomo hayo!Kuna bahasha za mitihani zipo wazi kabisa,hazijafungwa!!Halafu mwanafunzi analazimika kulipa elfu 15,000!
 
Back
Top Bottom