GE2025 No Reforms No Election sababu ya mkutano wa Kenani kuzuiliwa

GE2025 No Reforms No Election sababu ya mkutano wa Kenani kuzuiliwa

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Mbunge anayemaliza muda wake wa Jimbo la Nkasi Kaskazini mkoani Rukwa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Aida Kenani, amedai kuzuiwa na Jeshi la Polisi kufanya mkutano wa ndani na wanachama wa chama hicho na kwamba baadhi yao walikamatwa na kupigwa.

Akizungumza kwa njia ya simu na Jambo TV siku ya Jumapili, Kenani amesema mkutano huo wa ndani ulikuwa umepangwa kufanyika katika ukumbi mmoja eneo la Nkasi, lakini akadai kuwa mmiliki wa ukumbi huyo alitishwa na mamlaka na kulazimika kufuta matumizi ya ukumbi huo.

Baada ya hali hiyo, Kenani ameeleza kuwa aliamua kufanya kikao nyumbani kwake na baadhi ya wanachama, lakini akadai kuwa gari za polisi zilifika katika eneo hilo na kuwakamata baadhi ya washiriki, wakati yeye akiwa ametoka eneo hilo. Aidha alidai kuwa baadhi ya waliokamatwa walipigwa.

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, ACP Shadrack Masija, alipotafutwa na Jambo TV kuhusu madai hayo, alisema yupo mbali na eneo la tukio, lakini atawasiliana na maofisa wa eneo husika ili kupata taarifa kamili juu ya kilichotokea.
 
Back
Top Bottom