Njoo uwekeze kwenye biashara ya mafuta (Fuel) kwa laki 1 tu kama kima cha chini

Mkuu napenda kukufanulia kuwa baishara ya mafuta haiko hivyo kama ulivyoandika jaribu kufanya utafiti. Napenda kukufahamisha kuwa 10% ya 200 mil ni 20mil tu ambayo ni pesa ya kawaida sana kwenye faida ya Kituo cha mafuta kwa mwezi. So biashara hii ni tofauti sana na unavyoandika mkuu na usipate woga kuijaribu siku moja ili uujue undani wake!

FYI wala usiongelee tankers mbili nyingi sana hizo ni lita elfu 80, hata nusu tanker tu lita elfu 20 pekee inaweza kutoa hiyo 20 mil kwa mwezi na kampuni ikabaki na faida nzuri tu!
Karibu sana tufanye biashara mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndugu zangu tujitahidi kuwa wakweli kwa sasa biashara ya mafuta haelipi kabisa kwa watu wenye mitaji midogo kutokana na kodi na tozo mbalimbali kwenye bidhaa za petrol. Mashine za EFP zimeharibu sana TRA wanachukuwa full kodi, Services levy wanachuukuwa periodic report bado OSHA, EWURA, WMA, NEMC, TAPSOA , bika kusahau. Sheria ya mpya upakiaji mizigo imeongeza gharama za uchukuzi
 
Mfumo wa benki una taratibu zake. Hizo fixed deposit accounts hazijakuwepo tu. Kuna biashara ambako hio hela inapelekwa "low risks" kama government bonds au treasury bonds na vitu km hivyo. Na bado kuna usimamizi mkubwa wa BOT ili kumantain liquidity ya taasis husika

Pia biashara nyingine ambayo unawekeza na hela yako inaongezeka tu(haiwezi kula kwako) na haina gharama za uendesheji ni mifuko ya pensheni. Ina taratibu mahususi zake

Ila hii yalwako nashangaa. Hakuna gharama za uendeshaji na hakuna hasara ni faida tu. Nyie mnachapisha noti au?

Halafu kusema sehemu nyingi duniani wanafanya hivo hata telegram/deci kila aina ya ponzi schemes ziko dunia nzima hio sio sababu.

Kinachoniogopesha ni kuwa mfumo wenu wa biashara unavunja miiko yote ya biashara toka dunia iumbwe.

Unaposema ukiweka hio hela unakua sio shareholder sasa shareholder ni nani kama anayewekeza sio shareholder. Kitendo cha kuongeza mtaji kwa nia ya kupata faida automatically unakua shareholder.

Labda unipe maelezo zaidi. Unaweza kunishawishi mimi nifunge biashara zangu zoote niwaletee hata milion 200 halaf nikae likizo nasubiria miez mi3 nipate gawio la 10% bila kufanya kazi yoyote bila risk yoyote
Utapigwa hio 200M upate ukichaa wa ghafla!
 
Biashara ya mafuta imekuwa na ushindani sana , huu ushindani umrpunguza sana faida , unakuta ubaoni bei inasoma 2218 PMS , GO 2251 ukiengia ndani unapewa discount had I 150- 200|= kituo kinachojitahidi kuwa na mauzo mazuri kinauza Lita 300,000 kwa mwezi vituo vya kawaida vinauza Lita 150,000. Vingine vjnauza chini ya Lita 100,000/= profit margin per liter 70-120|= times mauzo then toa Upotevu was mafuta kwenye tanker lako kituoni (UST) then toa truck short madereva wanaeba mafuta wanayokubebea, then toa services kevy 0.03 ya mauzo yako then toa kodi ya pango / kituo cha mafuta sio less than 4M per months,then toa salary ya wafanyakazi, then toa OSHA Bills in more than 2M per year then toa NEMC fee, then toa EWURA licences fees then toa business licences fee , finally toa utakavyopigwa na manager wako. Hapo utaweza toa Gawio ka 10% kwa kila aliyewekeza?



Ndugu zangu tujitahidi kuwa wakweli kwa sasa biashara ya mafuta haelipi kabisa kwa watu wenye mitaji midogo kutokana na kodi na tozo mbalimbali kwenye bidhaa za petrol. Mashine za EFP zimeharibu sana TRA wanachukuwa full kodi, Services levy wanachuukuwa periodic report bado OSHA, EWURA, WMA, NEMC, TAPSOA , bika kusahau. Sheria ya mpya upakiaji mizigo imeongeza gharama za uchukuzi
 
Biashara ya mafuta imekuwa na ushindani sana , huu ushindani umrpunguza sana faida , unakuta ubaoni bei inasoma 2218 PMS , GO 2251 ukiengia ndani unapewa discount had I 150- 200|= kituo kinachojitahidi kuwa na mauzo mazuri kinauza Lita 300,000 kwa mwezi vituo vya kawaida vinauza Lita 150,000. Vingine vjnauza chini ya Lita 100,000/= profit margin per liter 70-120|= times mauzo then toa Upotevu was mafuta kwenye tanker lako kituoni (UST) then toa truck short madereva wanaeba mafuta wanayokubebea, then toa services kevy 0.03 ya mauzo yako then toa kodi ya pango / kituo cha mafuta sio less than 4M per months,then toa salary ya wafanyakazi, then toa OSHA Bills in more than 2M per year then toa NEMC fee, then toa EWURA licences fees then toa business licences fee , finally toa utakavyopigwa na manager wako. Hapo utaweza toa Gawio ka 10% kwa kila aliyewekeza?
Hivi bado hujang'amua kwamba huyu jamaa ni tapeli. Tena amekuja na mbinu ya kishamba kweli. Hamna biashara inayoweza ku guarantee faida ya namna hio duniani labda ya stocks and bonds ambayo ni ngumu sana kwa wasio na mitaji!
 
UWEKEZAJI KATIKA BIASHARA YA MAFUTA

Nimeona niwaletee fursa niliyonayo ambayo inahusiana na uwekezaji kwenye biashara na kuweza kujiongezea kipato nje ya mshahara au kazi yako unayofanya, fursa hii inawahusu watu wote ila nimeona ni vyema nanyi niwashirikishe kuliko kuwafaidisha wengine tu nikawasahau ndugu zangu, sasa twende pamoja kuijua fursa hii!

Tuna kampuni inayojihusisha na biashara ya mafuta na gas ambapo tumeona ni vyema kuwashirikisha wadau katika uwekezaji wa biashara hii ya mafuta.

Tunakaribisha watu mbalimbali kuwekeza kwenye mradi wetu wa mafuta kiasi ambapo mwekezaji atakua anapata Gawio la 10% kila mwezi kutokana na uwekezaji wake na baada ya muda wa mkataba tuliokubaliana kumalizika mhusika anaweza kuamua kuhuisha mkataba wake ama akachukua hela yake aliyowekeza. Namna ya kuwekeza ni kama ifuatavyo ;

1. uwekezaji huu unafanyika kisheria kwa kufuata taratibu zote za uwekezaji katika miradi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya usimamizi wa mwanasheria wa kampuni!

2. Mwekezaji atalipwa gawio la 10% ya Gharama ya uwekezaji wake kila mwezi bila kuathiri pesa yake aliyowekeza.

3. Mwekezaji hatahusishwa na hasara yoyote itakayojitokeza ktk uendeshaji.

4. Mwekezaji hatohusishwa na Gharama yoyote ya uendeshaji.

5. Kiwango cha chini cha uwekezaji ni 100,000 na Kiwango cha juu ni 2,000,000 kwa mtu binafsi. Kwa taasisi au kampuni kima cha chini cha uwekezaji ni 500,000 na kima cha juu ni 10,000,000 kwa taasisi au kampuni moja.

6. Mkataba wa uwekezaji kwa mtu binafsi utahuishwa kila baada ya miezi 3 ( hivyo kila baada ya miezi 3 utaamua kuendelea kuwekeza au kuondoa pesa yako kwenye uwekezaji). Kwa taasisi au kampuni muda wa kuhuisha mkataba ni kila baada ya miezi 6.

7. Gawio litatolewa tar 1 ya kila mwezi kupitia account ya kampuni ( hapa pesa hutumwa kwa mhusika automatically kwa kutumia system ya bank inayotumiwa na kampuni yetu).

8. Mwekezaji anaruhusiwa kukagua mradi wetu wa mafuta na documents zote za usajiri kisheria ili kujiridhisha kabla hajaamua kuniunga na mradi.

9. Mwekezaji anaruhusiwa kuwa na mwanasheria wake au shahidi wakati wa kufanya makubaliano ya mkataba.

Sifa za Mwekezaji ni kama ifuatavyo ;
1. Anatakiwa kuwa mtanzania wa kuzaliwa au kuandikisha (akiwa sio mtanzania anapaswa kuwa na kibali cha kuishi nchini na kibali cha kufanya kazi nchini)

2. Anatakiwa kuwa na umri usiopungua miaka 18.

3. Awe na akili timamu.

4. Jinsi zote.

5. Awe na kitambulisho cha Taifa, cha mpiga kura au leseni ya udereva. Picha moja passport size.

6. Shilingi elfu 2 ya kulipia form.

7. Pesa ya uwekezaji isiyopungua 100,000 kwa mtu binafsi na 500,000 kwa taasisi.

NB : Kwa aliyekidhi vigezo tajwa hapo anazo sifa za kuwa mwekezaji wetu, tunahitaji wawekezaji 100 kwa awamu ya kwanza.
Dirisha la usajiri kwa awamu ya kwanza litafungwa tarehe 30 April 2019.

Tunapenda kuwakaribisha nyote katika uwekezaji huu wa kibiashara, kwa watakaowiwa kuwekeza wawasiliane nami kwa maelezo zaidi kupitia ;
0764 143 900
0715 143 900
hemedrenatus@yahoo.com
hgecompany@gmail.com

Ahsante

Sent using Jamii Forums mobile app
Haya maneno kwa sasa ni matamu kweli lakini ukijiunga baadaye yatakuwa machungu sana
 
Tangu nimepigwa pesa na yule mama Anajiita Bi.Ubwa wa NAMAINGO ahahah..sitakaa kutapeliwa kizembe namna hii.I believe in hard work ili kupata pesa.
"Ukiona unaitwa sanaa kwenye dili nwa watu wa design hii, basi jua ww ndio dili lenyewe"

Sitasahau huu msemo
 
UWEKEZAJI KATIKA BIASHARA YA MAFUTA

Nimeona niwaletee fursa niliyonayo ambayo inahusiana na uwekezaji kwenye biashara na kuweza kujiongezea kipato nje ya mshahara au kazi yako unayofanya, fursa hii inawahusu watu wote ila nimeona ni vyema nanyi niwashirikishe kuliko kuwafaidisha wengine tu nikawasahau ndugu zangu, sasa twende pamoja kuijua fursa hii!

Tuna kampuni inayojihusisha na biashara ya mafuta na gas ambapo tumeona ni vyema kuwashirikisha wadau katika uwekezaji wa biashara hii ya mafuta.

Tunakaribisha watu mbalimbali kuwekeza kwenye mradi wetu wa mafuta kiasi ambapo mwekezaji atakua anapata Gawio la 10% kila mwezi kutokana na uwekezaji wake na baada ya muda wa mkataba tuliokubaliana kumalizika mhusika anaweza kuamua kuhuisha mkataba wake ama akachukua hela yake aliyowekeza. Namna ya kuwekeza ni kama ifuatavyo ;

1. uwekezaji huu unafanyika kisheria kwa kufuata taratibu zote za uwekezaji katika miradi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya usimamizi wa mwanasheria wa kampuni!

2. Mwekezaji atalipwa gawio la 10% ya Gharama ya uwekezaji wake kila mwezi bila kuathiri pesa yake aliyowekeza.

3. Mwekezaji hatahusishwa na hasara yoyote itakayojitokeza ktk uendeshaji.

4. Mwekezaji hatohusishwa na Gharama yoyote ya uendeshaji.

5. Kiwango cha chini cha uwekezaji ni 100,000 na Kiwango cha juu ni 2,000,000 kwa mtu binafsi. Kwa taasisi au kampuni kima cha chini cha uwekezaji ni 500,000 na kima cha juu ni 10,000,000 kwa taasisi au kampuni moja.

6. Mkataba wa uwekezaji kwa mtu binafsi utahuishwa kila baada ya miezi 3 ( hivyo kila baada ya miezi 3 utaamua kuendelea kuwekeza au kuondoa pesa yako kwenye uwekezaji). Kwa taasisi au kampuni muda wa kuhuisha mkataba ni kila baada ya miezi 6.

7. Gawio litatolewa tar 1 ya kila mwezi kupitia account ya kampuni ( hapa pesa hutumwa kwa mhusika automatically kwa kutumia system ya bank inayotumiwa na kampuni yetu).

8. Mwekezaji anaruhusiwa kukagua mradi wetu wa mafuta na documents zote za usajiri kisheria ili kujiridhisha kabla hajaamua kuniunga na mradi.

9. Mwekezaji anaruhusiwa kuwa na mwanasheria wake au shahidi wakati wa kufanya makubaliano ya mkataba.

Sifa za Mwekezaji ni kama ifuatavyo ;
1. Anatakiwa kuwa mtanzania wa kuzaliwa au kuandikisha (akiwa sio mtanzania anapaswa kuwa na kibali cha kuishi nchini na kibali cha kufanya kazi nchini)

2. Anatakiwa kuwa na umri usiopungua miaka 18.

3. Awe na akili timamu.

4. Jinsi zote.

5. Awe na kitambulisho cha Taifa, cha mpiga kura au leseni ya udereva. Picha moja passport size.

6. Shilingi elfu 2 ya kulipia form.

7. Pesa ya uwekezaji isiyopungua 100,000 kwa mtu binafsi na 500,000 kwa taasisi.

NB : Kwa aliyekidhi vigezo tajwa hapo anazo sifa za kuwa mwekezaji wetu, tunahitaji wawekezaji 100 kwa awamu ya kwanza.
Dirisha la usajiri kwa awamu ya kwanza litafungwa tarehe 30 April 2019.

Tunapenda kuwakaribisha nyote katika uwekezaji huu wa kibiashara, kwa watakaowiwa kuwekeza wawasiliane nami kwa maelezo zaidi kupitia ;
0764 143 900
0715 143 900
hemedrenatus@yahoo.com
hgecompany@gmail.com

Ahsante

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii mbinu mnayotumia nyie watu wa biashara za mtandao (Q net, bitclub, Aliance n.k) tulishaishtukia kitambo, atakayepigwa ni kwa ujinga wake. AKILI KICHWANI.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba nije nianze na laki 5, ila ombi langu kama kuna kibarua chochote ila sio chaofisini hata kama kitakuwa kinahitaji nguvu kidogo nipatiacho niwe kibarua vilevile mwekezaji

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu naomba nikujulishe tuu hiki unachokifanya ni kinyume na sheria za nchi kwahiyo hakuna mkataba ambao utasimama kwa sababu mkataba ni batili toka mwanzo ( void ab initio). Kama ungekuwa unauza share za kampuni tungekubaliana ni sawa ila hii kitu unafanya hakuna huwezi kuchukua hela kutoka kwenye public halafu ukaahidi kutoa riba wakati ujasajiliwa kama taasisi ya fedha Soma Kifungu cha sita 6(1mpaka 4 cha Bank and finance act see a link https://www.bot.go.tz/BankingSupervision/BAFIA2006.pdf ) Ukipata muda wa ziada unaweza kusoma kesi namba 66/2007 kati ya ULF NILSON dhidi ya Dr Tito M Andrew imeambtanishwa hapo chini.
Hizi nondo ndio zinampeleka pangoni kabisa.
Maswali rahisi kama jina la kampuni ameshindwa kujibu.
 
Ndugu naomba nikujulishe tuu hiki unachokifanya ni kinyume na sheria za nchi kwahiyo hakuna mkataba ambao utasimama kwa sababu mkataba ni batili toka mwanzo ( void ab initio). Kama ungekuwa unauza share za kampuni tungekubaliana ni sawa ila hii kitu unafanya hakuna huwezi kuchukua hela kutoka kwenye public halafu ukaahidi kutoa riba wakati ujasajiliwa kama taasisi ya fedha Soma Kifungu cha sita 6(1mpaka 4 cha Bank and finance act see a link https://www.bot.go.tz/BankingSupervision/BAFIA2006.pdf ) Ukipata muda wa ziada unaweza kusoma kesi namba 66/2007 kati ya ULF NILSON dhidi ya Dr Tito M Andrew imeambtanishwa hapo chini.
Mambo Ni Moto na Jua linawaka sana siku hizi........mkuu nmekuelewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna point 2 zinanipa shida,
Moja ni kwanini mwanahisa anahusika na faida tu lakini hausiki na hasara.
Mbili...
Je biashara hii ikitokea hasara pesa ya kuwalipa wanahisa inatoka katika mfuko gani?
Na nyongeza ni kwamba ukokotozi wa mgawo wa wanahisa huwa unabase ktk faida iliyo ktk financial report. Sasa kama wanahisa hawaambiwi hasara, nyie kuna siku mtakosa cha kuwalipa wanahisa maana inamaanisha kuwa hapatakuwa na ukaguzi ktk fedha wala mahesabu ya kampuni.
Na nyongeza ni kuwa vp kuhusu isuarance ya mtaji??????????
Kama kampuni haina financial report haiwezi kujua km ina faida au hasara.

People be care this may be a scam
 
Back
Top Bottom