Njoo ujue urembo asilia na Arabian Queen

Arabian queen

JF-Expert Member
Nov 23, 2016
2,557
4,824
Hali zenu.
Jukwaa hili katika thread hii ntakua napost urembo wa asili ambao natumia na naendelea kutumia na pia ukanisaidia,hope pia na nyinyi utawasaidia,na ningeomba mirejesho ili nijue maendeleo na imewasaidia kwa kiwango gani as how imenisaidia mm,i hope tutaungana mkono na kua kitu kimoja.leme start...

Namna ya kutengeneza bleach ya asili

Mahitaji
  1. Ukwaju
  2. asali
  3. rose water(kama huna hata maji ya kawaida yanafaa)
Jinsi ya kuchanganya na kutumia
Chukua ukwaju kias unachopenda changanya na ayo maji kias,sio sanaaa kias kwamba ikawa rojo jepes.changanya ukwaju na maji kias alafu wacha kwa mda wa nusu saa.

Baada ya hio nusu saa anza kuufikichafikicha mpk upate rojo zito,baada ya hapo tia asali kias pia.Alaf koroga tena,changanya vizuri tayar kwa matumizi.

Osha uso wako vizuri ,alaf paka huo mchanganyiko usoni mpk ukauke.
ukishakauka osha uso wako,paka ur favourate cream,huu mchanganyiko unakaa katika friji hata for one month.

Huu mchanganyiko ni very very best na matokeo utaanza kuyaona dakika ileile baada ya kuosha uso.mm napendelea kutumia kila baada ya siku nne,ni nzuri sana sana inabadilisha muonekano wako na kuonekana wa asili zaid na wa kungara.

Inasaidia kusafisha uso complitely.

msisahau mrejesho,
love u all.
 
Namna ya kutengeneza dawa ya chunusi nyumbani.

mahitaji
  1. Asali vijiko vitatu
  2. mdalasini kijiko kimoja
Namna ya kuandaa na kutumia
changanya asali na mdalasini,mpk vichanganyike.
osha uso wako vizuri pakaa usk wacha kwa dakika 20 alaf osha kwa maji.
Au
pakaa usiku sehem ambayo zinachunusi ,lala nayo usku ,ukiamka asbuh osha uso wako vizuri.

Hii husaidia kukausha chunus ,ni vizuri zaid ukatumia usk ukapakaa sehem ilokua na chunus then ukalala nayo.

Matokeo utayaona three days after use.

 
Pata muonekano ya kung'aa (fair skin tone)

Mahitaji
  1. Unga wa maganda ya machungwa
  2. yoghurt.
Namna ya kuandaa na matumizi

kausha maganda yako ya machungwa juani mpk yakauke alaf saga upate huo unga wa machungwa.
changanya unga wa machungwa na huo mtindi upate ujazo sawia.
osha uso uwe msafi,pakaa huo mchanganyiko usoni ,wacha mpk ikauke then osha.

Hii remedy inasaidia kutakatisha uso ,unapata mngao flani,pia inatoa madoa,unga wa machungwa inacontain vitamin C ambayo husaidia kutakatisha ngozi.

tumia kila baada ya siku mbili.
matokeo utayaona baada ya kutumia zaid ya mara tatu
 
Lakini kazi yake si ileile ya kublichi ama?
Kitu cha asili siku zote hakina madhara,na utakatishaji wake unangara as if ndo ulivo,lkn blich ya masokoni inakua na makemikali ambayo inaleta madhara baadae kama ukunyazi wa uso kwa haraka
 
Back
Top Bottom