Njiapanda kuelekea siasa safi na uongozi bora: Kutoka kutumia 'msuli' hadi siasa za 'ushawishi'.

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
Ukweli ni kwamba kwa dunia ya sasa ili kufanikiwa , inatakiwa kutumia akili na ushawishi mwingi huku ukitumia nguvu kidogo sana au usitumie nguvu kabisa. Ukifanya kinyume chake yaani kutumia nguvu za tembo na ushawishi sungura huwezi kuwa na mafanikio ya maana sana.

Angalau moja ya mambo ya kutia moyo, sasa tunahama tena kutoka siasa za msuli na kwenda kwenye siasa za kutumia akili na kujenga ushawishi.

Kutoka 'wewe balozi nakupa mwezi, ole wako nisione watalii' kana kwamba wanafungwa na kamba na kuletwa kibabe, hadi kwenye 'kushirikiana kwa pamoja kuwashawishi watalii kwa nini waje kwetu'.

Kutoka kuwatisha wenye mawazo tofauti hadi kukaribisha mijadala.(Japo taratibu taratibu kwa sababu 'too rapid transformations may lead to cracks')

Kutoka kuumizana sababu ya mitizamo hadi 'Njooni tuzungumze'
Kutoka 'forced economy' hadi 'Influenced economy' n.k

Maswali yanayoulizwa sana:

1. Kwa nini suala la katiba mpya halishughulikiwi kwa haraka? hili ni suala ni sensitive na linalohitaji timing na kutuliza vichwa na sio emotions na kukurupuka. Hivyo pamoja na umuhimu wake, Halihitaji kushughulikiwa kwa kukurupuka kwani uwezekano wa kukwamia njiani unakuwa ni mkubwa kama ilivyotokea hapo awali.

2. Ushirikiano mkubwa na nchi zilizoendelea (ni mabeberu?). Kwanza kuwaita wenzako mabeberu ni jambo lisilofaa, kama mwenzako beberu wewe ni nini? Hakuna namna nchi zenye uchumi mdogo zinaweza kuendelea bila kushirikiana vyema na waliofanikiwa. Matajiri sio maadui zetu bali ni development partners, hivyo tunaenda vizuri na kwenye muelekeo sahihi.Hata mtaani kwako usichukie matajiri bali shirikiana nao nawe utajirike. Kuwachukia ni roho ya uchawi ambayo nawe haikusaidii.

3. Nchi tajiri hazitupendi: Hii ni atitude ya ovyo kweli. Haya, hawatupendi sisi tunawapenda? ni kiashiria gani kinachoonesha kuwa wao hawatupendi ila sisi tunawapenda? ok wanatupa vitu kibao,sisi tunawapa nini? hatujui kuwa uhusiano ni kunufaishana na kama humnufaishi rafiki yako wewe rafiki mzigo? (na ni bora uwe unamnufaisha rafiki kuliko wewe kusubiria kunufaishwa tu, huo nao ni aina flani ya uhuni) so ni suala tu la kuangalia tunasaidiana vipi lakini hawa ni marafiki 'development partners'. Dhana ya ubeberu ilikuwa ni hila na tuliikataa toka mwanzo.

Kwa kuhitimisha, tunaenda kwenye muelekeo mzuri, siasa inayofanyika sasa ndio siasa ambayo watu wenye busara, uungwana na akili timamu wamekuwa wakiitamani wakati wote, siasa ya kuongea, kubadilishana mawazo, kufanya kazi pamoja, kushawishiana na sio siasa za msuli na kuumizana.

Hivyo kuna mema mengi yanakuja kwenye nchi hii. Tuendeleeni kuwa positive.
 
Kuna watu wanasema mbona transformations na reconciliations zinaenda taratibu? iko hivi, ukitaka kunyoosha kitu kilichopinda nyoosha taratibu na kwa timing. Vinginevyo utakivunja (licha ya dhamira yako njema)

Ukiendesha kwenye barabara mbovu, endesha kwa timing zaidi badala ya spidi kubwa. Haijalishi unawahi nini, usipozingatia hiyo hautafika uendako.

Waswahili husema kawia ufikie. Kwa maoni yangu hii ni busara nzuri na ndio muelekeo sahihi kwa viongozi wanaoongozwa na 'reasoning' na hiki ndio huwatofautisha na wale wazee wa 'emotions'

Kwa hiyo, usione kitu hakifanyiwi kazi kwa ghafla ukadhani hakionekani, au si muhimu bali kuna kitu kinaitwa "the law of timing". Pamoja na uzuri au umuhimu wa jambo, ili lifnikiwe, ni lazima lifanyike kwa timing sahihi.
 
Ukweli ni kwamba kwa dunia ya sasa ili kufanikiwa , inatakiwa kutumia akili na ushawishi mwingi huku ukitumia nguvu kidogo sana au usitumie nguvu kabisa. Ukifanya kinyume chake yaani kutumia nguvu za tembo na ushawishi sungura huwezi kuwa na mafanikio ya maana sana.

Angalau moja ya mambo ya kutia moyo, sasa tunahama tena kutoka siasa za msuli na kwenda kwenye siasa za kutumia akili na kujenga ushawishi.

Kutoka 'wewe balozi nakupa mwezi, ole wako nisione watalii' kana kwamba wanafungwa na kamba na kuletwa kibabe, hadi kwenye 'kushirikiana kwa pamoja kuwashawishi watalii kwa nini waje kwetu'.

Kutoka kuwatisha wenye mawazo tofauti hadi kukaribisha mijadala.(Japo taratibu taratibu kwa sababu 'too rapid transformations may lead to cracks')

Kutoka kuumizana sababu ya mitizamo hadi 'Njooni tuzungumze'
Kutoka 'forced economy' hadi 'Influenced economy' n.k

Maswali yanayoulizwa sana:

1. Kwa nini suala la katiba mpya halishughulikiwi kwa haraka? hili ni suala ni sensitive na linalohitaji timing na kutuliza vichwa na sio emotions na kukurupuka. Hivyo pamoja na umuhimu wake, Halihitaji kushughulikiwa kwa kukurupuka kwani uwezekano wa kukwamia njiani unakuwa ni mkubwa kama ilivyotokea hapo awali.

2. Ushirikiano mkubwa na nchi zilizoendelea (ni mabeberu?). Kwanza kuwaita wenzako mabeberu ni jambo lisilofaa, kama mwenzako beberu wewe ni nini? Hakuna namna nchi zenye uchumi mdogo zinaweza kuendelea bila kushirikiana vyema na waliofanikiwa. Matajiri sio maadui zetu bali ni development partners, hivyo tunaenda vizuri na kwenye muelekeo sahihi.Hata mtaani kwako usichukie matajiri bali shirikiana nao nawe utajirike. Kuwachukia ni roho ya uchawi ambayo nawe haikusaidii.

3. Nchi tajiri hazitupendi: Hii ni atitude ya ovyo kweli. Haya, hawatupendi sisi tunawapenda? ni kiashiria gani kinachoonesha kuwa wao hawatupendi ila sisi tunawapenda? ok wanatupa vitu kibao,sisi tunawapa nini? hatujui kuwa uhusiano ni kunufaishana na kama humnufaishi rafiki yako wewe rafiki mzigo? (na ni bora uwe unamnufaisha rafiki kuliko wewe kusubiria kunufaishwa tu, huo nao ni aina flani ya uhuni) so ni suala tu la kuangalia tunasaidiana vipi lakini hawa ni marafiki 'development partners'. Dhana ya ubeberu ilikuwa ni hila na tuliikataa toka mwanzo.

Kwa kuhitimisha, tunaenda kwenye muelekeo mzuri, siasa inayofanyika sasa ndio siasa ambayo watu wenye busara, uungwana na akili timamu wamekuwa wakiitamani wakati wote, siasa ya kuongea, kubadilishana mawazo, kufanya kazi pamoja, kushawishiana na sio siasa za msuli na kuumizana.

Hivyo kuna mema mengi yanakuja kwenye nchi hii. Tuendeleeni kuwa positive.
Anayetumia nguvu na ubabe kwa dunia ya sasa ni yule asiye na akili tu
 
...
Maswali yanayoulizwa sana:

1. Kwa nini suala la katiba mpya halishughulikiwi kwa haraka? hili ni suala ni sensitive na linalohitaji timing na kutuliza vichwa na sio emotions na kukurupuka. Hivyo pamoja na umuhimu wake, Halihitaji kushughulikiwa kwa kukurupuka kwani uwezekano wa kukwamia njiani unakuwa ni mkubwa kama ilivyotokea hapo awali.
...
... suala la Katiba Mpya halitakiwi kushughulikiwa kwa kukurupuka? Umehamia leo Tanzania? Mchakato umeanza leo? Mchakato una zaidi ya miaka 10 unazungumzia kukurupuka? Hizo ni hadaa za CCM ili iendelee kutawala kimabavu kwa kutumia Katiba mbovu inayowapa kila aina ya upendeleo.
 
... suala la Katiba Mpya halitakiwi kushughulikiwa kwa kukurupuka? Umehamia leo Tanzania? Mchakato umeanza leo? Hizo ni hadaa za CCM ili iendelee kutawala kimabavu kwa kutumia Katiba mbovu inayowapa kila aina ya upendeleo.
Mkuu, Mzee kikwete alikuwa fair sana kwenye hili suala la katiba lakini mwisho yalitumika mabilioni na ilivyoishia uliona. So issue hapa sio uharaka, issue ni muda sahihi, kwa timing sahihi kwa utaratibu na muelekeo sahihi.

Huu mtizamo tu wa kwamba katiba mpya inalenga kumtoa huyu madarakani na kumuungiza yule au kumbakiza huyu na yule, tayari ni tatizo kubwa kabisa.

Kuwa na mtizamo huo tu katika hatua za mwanzo, ni kuanza na mguu wa kushoto kwa kuwa tayari kitakachokuwa kinatafutwa hapo sio muafaka wa kitaifa tena bali mnyukano wa makundi masilahi. Sasa katika mnyukano wa makundi maslahi, anayeshinda ni kundi lenye nguvu wakati kwenye katiba mshindi anapaswa kuwa taifa. Wewe huoni mkwamo hapo tayari kabla hata ya kuanza?
 
Mkuu, Mzee kikwete alikuwa fair sana kwenye hili suala la katiba lakini mwisho yalitumika mabilioni na ilivyoishia uliona. So issue hapa sio uharaka, issue ni muda sahihi, kwa timing sahihi kwa utaratibu na muelekeo sahihi.

Huu mtizamo tu wa kwamba katiba mpya inalenga kumtoa huyu madarakani na kumuungiza yule au kumbakiza huyu na yule, tayari ni tatizo kubwa kabisa.

Kuwa na mtizamo huo tu katika hatua za mwanzo, ni kuanza na mguu wa kushoto kwa kuwa tayari kitakachokuwa kinatafutwa hapo sio muafaka wa kitaifa tena bali mnyukano wa makundi masilahi. Sasa katika mnyukano wa makundi maslahi, anayeshinda ni kundi lenye nguvu wakati kwenye katiba mshindi anapaswa kuwa taifa. Wewe huoni mkwamo hapo tayari kabla hata ya kuanza?
... lengo #1 la Katiba Mpya sio kumtoa huyu na kumwingiza yule acha kupotosha. HAKI SAWA KWA WOTE
 
Mkuu, Mzee kikwete alikuwa fair sana kwenye hili suala la katiba lakini mwisho yalitumika mabilioni na ilivyoishia uliona. So issue hapa sio uharaka, issue ni muda sahihi, kwa timing sahihi kwa utaratibu na muelekeo sahihi.

Huu mtizamo tu wa kwamba katiba mpya inalenga kumtoa huyu madarakani na kumuungiza yule au kumbakiza huyu na yule, tayari ni tatizo kubwa kabisa.

Kuwa na mtizamo huo tu katika hatua za mwanzo, ni kuanza na mguu wa kushoto kwa kuwa tayari kitakachokuwa kinatafutwa hapo sio muafaka wa kitaifa tena bali mnyukano wa makundi masilahi. Sasa katika mnyukano wa makundi maslahi, anayeshinda ni kundi lenye nguvu wakati kwenye katiba mshindi anapaswa kuwa taifa. Wewe huoni mkwamo hapo tayari kabla hata ya kuanza?
Hapo ndipo Chadema wanakwama, wanataka katiba ili waitoe CCM madarakani, CCM hata wakiwa na nia njema, watajibu mapigo. Chadema wanasahau kuwaeleza wananchi uhusiano wa katiba na maisha yao, kwa hiyo wananchi hawaoni hasara yoyote, na wanaona mambo mengi yanaweza kutibiwa kwa sheria mpya(sio katiba mpya) na uongozi imara unaofuatilia maendeleo ya watu
 
Mkuu, Mzee kikwete alikuwa fair sana kwenye hili suala la katiba lakini mwisho yalitumika mabilioni na ilivyoishia uliona. So issue hapa sio uharaka, issue ni muda sahihi, kwa timing sahihi kwa utaratibu na muelekeo sahihi.

Huu mtizamo tu wa kwamba katiba mpya inalenga kumtoa huyu madarakani na kumuungiza yule au kumbakiza huyu na yule, tayari ni tatizo kubwa kabisa.

Kuwa na mtizamo huo tu katika hatua za mwanzo, ni kuanza na mguu wa kushoto kwa kuwa tayari kitakachokuwa kinatafutwa hapo sio muafaka wa kitaifa tena bali mnyukano wa makundi masilahi. Sasa katika mnyukano wa makundi maslahi, anayeshinda ni kundi lenye nguvu wakati kwenye katiba mshindi anapaswa kuwa taifa. Wewe huoni mkwamo hapo tayari kabla hata ya kuanza?

..mchakato ulikuwa unaendelea vizuri mpaka pale JK na Ccm walipoamua kuuhujumu.

..JK hakutegemea kwamba tume ya Warioba itatoa mapendekezo yale, haswa pendekezo la serikali 3.
 
Mada yako mjadala ungekuwa kutoka kwenye siasa za ‘kuambiana ukweli’ na kurudi kwenye mambo ‘kufarijiana uongo wa mchana kweupe bila ya aibu’.

Yaani una-amini kabisa kwa kumsikiliza mtu kama Msigwa anapodai mayor wa Dallas anampango wa kuleta safari ya ndege ya moja kwa moja kutoka Dallas mpaka Tanzania; as if huyo mayor ni mkurugenzi wa shirika la ndege. Hao watu wanadhani nchi za wenzetu mambo yanafanyika kama kwetu kiongozi anajisemea tu.

Surely you are better than that mara nyingi binafsi huwa na enjoy elimu inayopatikana katika mada zako there are always ‘thought provoking’ point of views.

Usipoteze brand yako kirahisi rahisi, stick to your analytical writing. Mama ana chawa wake wa kutosha jumlisha genge la wahuni mitandaoni wa kueneza propaganda zao za kitoto na kuharibu ata hayo machache mazuri anayofanya kwa kuongezea chumvi zisizo na lazima.
 
... lengo #1 la Katiba Mpya sio kumtoa huyu na kumwingiza yule acha kupotosha. HAKI SAWA KWA WOTE
Hivyo ndivyo inavyopaswa kuwa lakini tayari kuna tatizo la kimtazamo miongoni mwa vyama vya siasa na kwa kuanzia ni lazima kwanza wote wawe na uelewa kama huu ulio usema hapa ndio uanze mchakato. Ukinza kabla ya kuweka sawa mitizamo hiyo kwanza, lazima mchakato ukwame mahali.
 
Hapo ndipo Chadema wanakwama, wanataka katiba ili waitoe CCM madarakani, CCM hata wakiwa na nia njema, watajibu mapigo. Chadema wanasahau kuwaeleza wananchi uhusiano wa katiba na maisha yao, kwa hiyo wananchi hawaoni hasara yoyote, na wanaona mambo mengi yanaweza kutibiwa kwa sheria mpya(sio katiba mpya) na uongozi imara unaofuatilia maendeleo ya watu
Sahihi kabisa. Ukishaanza kwa hoja ya kwamba lengo ni kuitoa CCM madarakani, obviously tayari una uhakika wa kupata upinzani kutoka kwa CCM . hiyo ni simple logic tu.

Sasa ndio maana upo umuhimu wa ku settle makandokando ya uelewa kwanza kabla ya mchakato wenyewe ili wakati watu wanaingia kwenye mchakato,wanaenda wakiwa na uelewa kuwa katiba ni muafaka wa wananchi kwa maslahi ya taifa na sio kuwekana au kutoana madarakani.
 
Mada yako mjadala ungekuwa kutoka kwenye siasa za ‘kuambiana ukweli’ na kurudi kwenye mambo ‘kufarijiana uongo wa mchana kweupe bila ya aibu’.

Yaani una-amini kabisa kwa kumsikiliza mtu kama Msigwa anapodai mayor wa Dallas anampango wa kuleta safari ya ndege ya moja kwa moja kutoka Dallas mpaka Tanzania; as if huyo mayor ni mkurugenzi wa shirika la ndege. Hao watu wanadhani nchi za wenzetu mambo yanafanyika kama kwetu kiongozi anajisemea tu.

Surely you are better than that mara nyingi binafsi huwa na enjoy elimu inayopatikana katika mada zako there are always ‘thought provoking’ point of views.

Usipoteze brand yako kirahisi rahisi; mama ana chawa wake wa kutosha jumlisha genge la wahuni mitandaoni wa kueneza propaganda zao za kitoto na kuaribu ata hayo machache mazuri anayofanya.
Mzee, demokrasia ni kusikiliza mawazo unayoyataka na usiyoyataka. Mawazo yenye akili na yakijinga bila kugombana. Kumbuka kuwa kila mtu ana kichwa chake na uwezo wake wa kufikiri na hata kama mtu anafikiri low, anaamini yuko sahihi.

Sasa hata huyo anayesema Mayor wa Dallas ataleta ndege Tanzania, unadhani ipo haja ya kugombana naye na pengine kumdhuru? wewe huoni hizo ni hoja nyepesi tu ambazo zinajibika, so huyo anastahili tu kuelimishwa? sasa tulipita kipindi mtu kama huyo anaumizwa, unadhani tulikuwa tunaenda muelekeo sahihi?
 
Mada yako mjadala ungekuwa kutoka kwenye siasa za ‘kuambiana ukweli’ na kurudi kwenye mambo ‘kufarijiana uongo wa mchana kweupe bila ya aibu’.

Yaani una-amini kabisa kwa kumsikiliza mtu kama Msigwa anapodai mayor wa Dallas anampango wa kuleta safari ya ndege ya moja kwa moja kutoka Dallas mpaka Tanzania; as if huyo mayor ni mkurugenzi wa shirika la ndege. Hao watu wanadhani nchi za wenzetu mambo yanafanyika kama kwetu kiongozi anajisemea tu.

Surely you are better than that mara nyingi binafsi huwa na enjoy elimu inayopatikana katika mada zako there are always ‘thought provoking’ point of views.

Usipoteze brand yako kirahisi rahisi, stick to your analytical writing. Mama ana chawa wake wa kutosha jumlisha genge la wahuni mitandaoni wa kueneza propaganda zao za kitoto na kuharibu ata hayo machache mazuri anayofanya kwa kuongezea chumvi zisizo na lazima.

Sisi Tanzania (Wao) Viongozi ni wajinga wakifikiri na sisi raia #thecommonmwananchi ni wapumbavu
 
Mzee, demokrasia ni kusikiliza mawazo unayoyataka na usiyoyataka. Mawazo yenye akili na yakijinga bila kugombana. Kumbuka kuwa kila mtu ana kichwa chake na uwezo wake wa kufikiri na hata kama mtu anafikiri low, anaamini yuko sahihi.

Sasa hata huyo anayesema Mayor wa Dallas ataleta ndege Tanzania, unadhani ipo haja ya kugombana naye na pengine kumdhuru? wewe huoni hizo ni hoja nyepesi tu ambazo zinajibika, so huyo anastahili tu kuelimishwa? sasa tulipita kipindi mtu kama huyo anaumizwa, unadhani tulikuwa tunaenda muelekeo sahihi?
Hakuna anaekataa kusikiliza mawazo kinzani issue ni pale mtu anapoleta hoja asizoweza kuzi back up.

Mfano ata kama bila ya kutaja majina una imply safari yetu imetoka kulazimishana hadi kwenye ushawishi; hizo ni propaganda ambazo hazina merit wakati kuna info kibao unaweza tumia to back up your claims with evidence.

Mfano mimi naweza kukwambia Magufuli alikuwa master wa uchumi na aliweza kuwajibu IMF, WB na wadau wengine wa misaada hadharani kwa sababu alikuza uchumi kiasi kwamba anaweza pata mikopo kupitia commercial financial institution through economic data wanazozikagua hao hao IMF na WB kwenye kuandikia ‘debt sustainability analysis’ reports.



Unaweza pitia hizo info na kusoma uchumi wa Magufuli kabla ya COVID mwamba alikuwa anashusha debt to GDP ratio info ambazo zinamfanya kuaminika kukopesheka sio kwa data za kupika bali through endorsements report kama hizo za IMF na World bank wenyewe wanasema alipeleka uchumi wa Tanzania na makusanyo yake kuwa low risk kwenye kukopesheka.

Ni hizo ‘debt sustainability report’ zao ndio watu duniani wanaangalia unafaa kukopeshwa au la; na utaona ya WB na IMF azitofautiani kwa sababu wanafanya scrutiny ya pamoja and it’s a joint report.

Sasa embu leta ushahidi wa makatasi mama ana ushawishi wa kuvutia chochote zaidi ya kelele za MoU ambazo none have materialised to anything yet, hakuna mafanikio yoyote zaidi ya kurudi kulamba miguu ya wazungu na kuwaacha wahuni wachote hela wanavyotaka.

Issue sio kuwa na mawazo kinzani bali kuwa objective kwenye hoja zako surely you are capable of that, siasa za uchawa waachie wengine.
 
Sisi Tanzania (Wao) Viongozi ni wajinga wakifikiri na sisi raia #thecommonmwananchi ni wapumbavu
Wana audience zao wanapokuwa wanaongea hayo mambo it’s understable, lakini kwa mwerevu na mtu asie na maslahi katika upigaji kueneza propaganda zao ni kutudharau watanzania.

Msigwa posho yake ya week mbili kwenye hiyo ziara ya kuzurura marekani inaweza kufika ata $20,000 so you understand yupo ndani ya ulaji kusifia kwake kunaendana na maslahi binafsi. Lakini tena sio chawa wengine kutuambia huo upuuzi anaongea Msigwa ni uthibitisho wa ushawishi wa mama kimataifa.
 
Katiba mpya ndio kitu cha msingi. Swala ni je mheshimiwa raisi ana moyo wa chuma wa kuwashawishi na ikibidi kupambana na wahafidhina wa ccm?
 
Back
Top Bottom