Niwasaidiaje kaka zangu?

Niwasaidiaje kaka zangu?

Malizia ujenzi, huo ndo msaada mkubwa kuliko woote utakaoutoa, Jenga nyumba ya kawaida kabisa na hata finishing isiwe kuubwa, ukiweka chunba na sebule cha wazee na room @ bro plus roon ya wageni(ya kwako) inatosha sana.
Ukimaliza ujenzi utakuwa umewasaidia saana, then utaendelea na support ndogo,ndogo ila kimaisha/status utakuwa unewanyanyua saana kwa wao kuendelea na issue zao mdogo,mdogo
 
Mwalimu wetu wa physics form two sijui alikua anafundisha topic gani akatuambia ili rocket ipae inahitaji ukinzani wa hali ya juu sana kisha akaendelea akili ya binadamu ni kama rocket ili ifanye kazi inatakiwa ibanwe kisawasawa na kuanzia hapo alitupeleka mchakamchaka mpaka wengine walikimbia somo lake

Sasa nachotaka kusema hapa ni kwamba hao kaka zako acha kuwadekeza we wakatie mirija kabisa ikiwezekana hata wakikupigia simu usipokee badili namba kabisa kisha fanya mambo yako ya msingi haiwezekani dume zima at age of 30 unalilipia kodi na hela ya nauli unalipa litajiongeza saa ngapi sasa

We kata misaada fanya mambo yako wangekua wa kike kidogo inge make sense
Kwaroho mbaya watu weusi tuko vizuri. Mleta mada kaomba ushauri wa jambo la kufanya lakini wengi wanamzuia asitimize nia yake ilhali hajaomba msaada wa pesa.

Watu wako tayari kuchangia harusi na misiba lakini sio kutoa msaada wa pesa za matibabu ama kumkopesha mtu mtaji.
 
  • Thanks
Reactions: a45
Huwez kumsaidia ndugu akaridhika hata siku moja,na wewe mwenyewe bado Sana una Safari ndefu,jiwekeze wewe kwanza ujijwnge vzr ili hata ndugu akila mtaji usiwe unawaza Tena,Jenga nyumba weka vitega uchumi Kama ni elimu jiendeleze,upate kazi nzuri Zaid ya hiyo unayofanya,mpaka utakapokuwa financially stable ..
 
Mtoto wa kwanza ana vita kubwa sana ya kiroho ila kwa leo sitozungumzia hilo....ila Shetani anapenda kuwaharibia future sana watoto wa kwanza kwa kuwa anajua kwamba mtoto wa kwanza akifanikiwa basi kwa wanaofuata huwa ni rahisi....Lichunguze hilo....

Nimesema hivyo kumaanisha kuwa wewe ndie umebahatika na unaeweza kurejesha amani tena kwenye familia hivyo Focus kutengeneza maisha yako kwanza huku ukimuomba MUNGU akuongoze utimize hilo kwa haraka then ndio uangalie utaratibu wa kutengeneza ya hao wa nyuma yako....Hapo ukicheza vibaya mtajikuta level moja japo unasema una elimu maana hiyo vita ni ya Shetani
Hakuna Vita yoyote ya kiroho,ni ujinga tu wa kimalezi kutokana na wazazi kuwa na excitement na mtoto,hii Imani mnalishana Sana kwenye makanisa yenu ya sadaka,Lea watoto vzr wape exposure,kuwa muwazi kwao wote na wafundishe kuwajibika tangu wakiwa wadogo hakutakuwa na kitu sijui vita ya kiroho Wala nn ..
 
Back
Top Bottom