Niwasaidiaje kaka zangu?

Niwasaidiaje kaka zangu?

Sasa hivi itakuwa ngumu kuwakacha ghafla wewe chakufanya sitisha kwanza ujenzi kwa muda alafu tafuta kisingizio chochote kwamba kazini Mambo yameharibika na wewe iliye njaa utaone wenyewe wanajiweka pembeni na wewe maana asali imekata, wakati huo unachokipata unakitunza na wazazi unawasaidia kwa shida shida yaani wote muingie kwenye msoto, baadaye Sasa unaweza kujifanya Kuna sehemu umepata mkopo ukajenga haraka kwa ajili ya wazazi.
 
Jisaidie wewe mwenyewe ujenge nyumba kwanza, umalize, uwe na uwezo wa kusaidia wengine vizuri zaidi.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Jitosheleze kwanza wewe na wazazi wako na kutoa kipaumbele kikubwa katika kumalizia nyumba vinginevyo hata wewe utaanguka na hali izidi kuwa mbaya zaidi. Pole sana kwa changamoto za maisha.
 
Watoto wa kike wapogo poa sana,wakpata wanawaza nyumban kwanza,mifano nnayo,npo na wadada wawili Mkubwa kanizid miaka miwili,Mdogo nmemzid miaka mitatu hawa ndugu wananpgania sana mim kaka yao,Vyeti vyangu wanavyo kila sku wanantafutia ajira Mimi npo tu,waliwah npa hela ya biashara nkashndwa hata cha kufanya,NAKUSHAUR DOGO,JENGA KWANZA HATA USIWE NA HARAKA ZA KUWASAIDIA,UKIMALIZA KUJENGA BUNI BIASHARA NZURI MUITE MMOJA AJE ASIMAMIE AKIHARIBU FUKUZA NA UMPOTEZEE,usiwape mtaji,wew ndo unatakiwa ubuni biashara wao wasimamie,wew uwe boss wao,afu uwe mkali mtu akizingua
 
Sasa hivi itakuwa ngumu kuwakacha ghafla wewe chakufanya sitisha kwanza ujenzi kwa muda alafu tafuta kisingizio chochote kwamba kazini Mambo yameharibika na wewe iliye njaa utaone wenyewe wanajiweka pembeni na wewe maana asali imekata, wakati huo unachokipata unakitunza na wazazi unawasaidia kwa shida shida yaani wote muingie kwenye msoto, baadaye Sasa unaweza kujifanya Kuna sehemu umepata mkopo ukajenga haraka kwa ajili ya wazazi.

HAPANA. Kumbuka maneno huumba na haitakiwi kujinenea mabaya maana yatatokea. Few days ago nilikuwa kila nikiulizwa na mtu why sina namba yake nilikuwa nasingizia nimepoteza simu na sina namba zao...aiseee haikuchukua round nikaibiwa simu. Kikubwa tu akate mianya ya support zisizo na ulazima.. asaidie penye ulazima wa kufanya hivyo tu.
 
maamuzi yoyote tumia busara.. busara ambazo mmekuzwa nazo kwenu, kila mtu ana lake hapa kulingana na akivoishi na ndugu zake, kuna waliosalitiwa malengo na ndugu zao watakushauri uwapotezee, na kuna watakaokushari wabebe, ila simamia misingi iliyowalea maana ndo imewafikisha hapa..

tuna uwezo wa kuchagua marafiki,wachumba na wenza ila hatuna uwezo wa kuchagua familia, wazazi na ndugu wa karibu.. tafuta njia ya ku Co-exist kwa nyie nyote bila kurudishana nyuma. nna imani ipo,
 
Mtoto wa kwanza ana vita kubwa sana ya kiroho ila kwa leo sitozungumzia hilo....ila Shetani anapenda kuwaharibia future sana watoto wa kwanza kwa kuwa anajua kwamba mtoto wa kwanza akifanikiwa basi kwa wanaofuata huwa ni rahisi....Lichunguze hilo....Nimesema hivyo kumaanisha kuwa wewe ndie umebahatika na unaeweza kurejesha amani tena kwenye familia hivyo Focus kutengeneza maisha yako kwanza huku ukimuomba MUNGU akuongoze utimize hilo kwa haraka then ndio uangalie utaratibu wa kutengeneza ya hao wa nyuma yako....Hapo ukicheza vibaya mtajikuta level moja japo unasema una elimu maana hiyo vita ni ya Shetani
Ila first born huwa wanawajibika sana kwenye kusaidia familia zao hata ukoo pamoja na changamoto za kiroho zinazowakabili. Cha kushangaza hata madogo wakiwa wametusua bado watamwangalia kwa kila kitu ikiwemo kushughulikia changamoto za wazazi na shida zote za familia, wao kazi yao ni kula bata na lawama kibao.
 
Habari zenu ndugu zangu!

Mimi ni mdada at my early 20’s. Na ni mtoto wa mwisho na wa kike katika familia yetu nikiwa na kaka zangu wawili mmoja early 30’s mwingine late 20’s. Katika familia yetu mimi ndiye niliyefanikiwa kufika hadi degree nawashukuru wazazi wangu waliweza kunipigania na juhudi zangu pia. Ila kaka zangu mmoja alifanikiwa kufika diploma tu.

Familia yetu ilipitia changamoto nyingi sana sana za kuumiza lakini nashukuru Mungu tupo hai mpaka sasa. Na Mungu kanijalia kazi nzuri, ninajitegemea na kusaidia ndugu zangu pale niwezapo. Nilianza kazi mwaka jana mwezi wa Tano, nikasave nikafanikiwa kununua kiwanja na kufikia hadi hatua ya kuweka msingi! Niliamua kufanya hivyo kwasababu familia yetu hatujawahi kuwa na nyumba yetu wenyewe ya kumiliki! Kwahiyo ni kitu kilichokuwa kinanipa wasiwasi sana vipi siku kikitokea cha kutokea tutaenda wapi? Hivyo nikalipa lengo langu hilo priority.

Lakini sasa kaka zangu bado wanabangaiza vibarua walivyo navyo vinawasaidia kula na nauli za kwenda vibaruani na mara nyingine hata inanibidi niwape mimi hata hela ya nauli na ya kula! Na ilifika kipindi cha kulipa kodi basi nitoe yote au niwachangie! Hili sio tatizo maana najua Mungu kanipa uwezo ili niwasaidie ndugu zangu.

Swali ni ‘niwasaidiaje kakazangu?’ ili waweze kusimama vizuri kiuchumi? Maana mmoja tulishawahi kumchangia mtaji lakini biashra ikawa ngumu ikafeli. Mwingine hana passion na biashra na haiwezi tu niseme ila kibarua chake ni cha kipato kidogo sana. Wanashindwa hata kuoa kwasababu hawako vizuri kiuchumi. Kiukweli naumiaga sana na ni kama inaniongezea depression nikiwafikiria! Kuna wakati nakwama lakini najua sina ndugu wa kumuomba msaada naumia sana!

Sasa naomba mnisaidie ushauri na maoni, niwasaidieje? Je, ina maana mimi kuendelea na ujenzi ilihali ndugu zangu hawako vizuri kiuchumi? Natamani nichukue mkopo niwape kwaajili ya biashara lakini vipi zikifeli maana tayari ilishafeli! Je, ni sawa kuwawazia sana?

Samahani kwa kuwachosha! Natanguliza shukrani.
Achana na ndugu, nasema hivi achana na ndugu mdogo wangu

Hata ukiwapiga chini hautapungukiwa kitu asikudanganye mtu

Ndugu pekee wa maana ni wazazi, hao wengine wapambane wenyewe

Kwa umri wako huwezi kuelewa, ukute unafikiri unafanya jambo la maana ila una bahati kusanuliwa mapema kwamba achana nao

Tuliochelewa kushtuliwa tulikuja kushtuka baadae sana tumeshajichelewesha maisha yetu binafsi na tuliowasaidia hawajawahi kushukuru wala kuona maana ya tulichofanya
 
Kwahiyo Dada Jesca kuniomba msaada wa kukuunga JF sikuile ndio nia yako hii kuja kutusema na bora ungebadili User name nisiikujue, haya yote situngeyaongea kifamilia kumbuka sisi kakazako huwezi kutuweka hadharani hivi mtaji kweli ulinipa ila mdogo sana.
 
kusaidia ndugu ni kazi sana.
kwanza hawanaga shukrani
jengea wazee nyumba ,na wewe endelea na mambo yako
hao wakaka watakuja kukuingiza chaka hautakuja kuamini kama ni ndugu zako
Ile roho ya kimaskini ndio inajidhirisha ndani ya comment yako hii. We mtu kusaidia kuwainua kaka zake unaona gere? Acha wivu wa kichawi mkuu!!!

Utabakia hivyo hivyo.
 
Mtoa mada inaonesha ni jinsi gani wazazi wenu wametumia vyema nafasi zao katika kuhakikisha wanawalea watoto kwa upendo. Nafurahi sana kwa hilo.

Kitu ambacho nakuomba usiache kusaidia ndugu zako sababu eti watu wanakupandikiza roho ya chuki na ubinafsi. Wasaidie kadri moyo wako unavyokutuma as long as wanaleta matokeo chanya.

Wasije wakawa wale ndugu wa kutapanya hela makusudi af bado unawajaza hela bali wawe walio na daring spirit hata kama watashindwa at times ila kuna muda watasimama imara. Jaribu kuwafungulia biashara ambazo ni service oriented kama Mpesa,Tigopesa n.k!

Biashara ya I.T solutions kama Graphic design, Media Production ambazo zinaweza kufanyika with minor supervision.

Biashara kama salon ya kisasa ambayo nayo haiumizi kichwa sana ku manage.

Ama mgahawa wa chakula sehemu ambayo imechangamka. Akiwa mjanja akajifunza jinsi ya ku manage vizuri inamtoa hii biashara.

Hizi biashara ziwe at par na shughuli zao za sasa ili kuwaongezea kipato.
 
Back
Top Bottom