Misunderstood
JF-Expert Member
- Aug 4, 2020
- 385
- 887
Habari zenu ndugu zangu!
Mimi ni mdada at my early 20’s. Na ni mtoto wa mwisho na wa kike katika familia yetu nikiwa na kaka zangu wawili mmoja early 30’s mwingine late 20’s. Katika familia yetu mimi ndiye niliyefanikiwa kufika hadi degree nawashukuru wazazi wangu waliweza kunipigania na juhudi zangu pia. Ila kaka zangu mmoja alifanikiwa kufika diploma tu.
Familia yetu ilipitia changamoto nyingi sana sana za kuumiza lakini nashukuru Mungu tupo hai mpaka sasa. Na Mungu kanijalia kazi nzuri, ninajitegemea na kusaidia ndugu zangu pale niwezapo. Nilianza kazi mwaka jana mwezi wa Tano, nikasave nikafanikiwa kununua kiwanja na kufikia hadi hatua ya kuweka msingi! Niliamua kufanya hivyo kwasababu familia yetu hatujawahi kuwa na nyumba yetu wenyewe ya kumiliki! Kwahiyo ni kitu kilichokuwa kinanipa wasiwasi sana vipi siku kikitokea cha kutokea tutaenda wapi? Hivyo nikalipa lengo langu hilo priority.
Lakini sasa kaka zangu bado wanabangaiza vibarua walivyo navyo vinawasaidia kula na nauli za kwenda vibaruani na mara nyingine hata inanibidi niwape mimi hata hela ya nauli na ya kula! Na ilifika kipindi cha kulipa kodi basi nitoe yote au niwachangie! Hili sio tatizo maana najua Mungu kanipa uwezo ili niwasaidie ndugu zangu.
Swali ni ‘niwasaidiaje kakazangu?’ ili waweze kusimama vizuri kiuchumi? Maana mmoja tulishawahi kumchangia mtaji lakini biashra ikawa ngumu ikafeli. Mwingine hana passion na biashra na haiwezi tu niseme ila kibarua chake ni cha kipato kidogo sana. Wanashindwa hata kuoa kwasababu hawako vizuri kiuchumi. Kiukweli naumiaga sana na ni kama inaniongezea depression nikiwafikiria! Kuna wakati nakwama lakini najua sina ndugu wa kumuomba msaada naumia sana!
Sasa naomba mnisaidie ushauri na maoni, niwasaidieje? Je, ina maana mimi kuendelea na ujenzi ilihali ndugu zangu hawako vizuri kiuchumi? Natamani nichukue mkopo niwape kwaajili ya biashara lakini vipi zikifeli maana tayari ilishafeli! Je, ni sawa kuwawazia sana?
Samahani kwa kuwachosha! Natanguliza shukrani.
Mimi ni mdada at my early 20’s. Na ni mtoto wa mwisho na wa kike katika familia yetu nikiwa na kaka zangu wawili mmoja early 30’s mwingine late 20’s. Katika familia yetu mimi ndiye niliyefanikiwa kufika hadi degree nawashukuru wazazi wangu waliweza kunipigania na juhudi zangu pia. Ila kaka zangu mmoja alifanikiwa kufika diploma tu.
Familia yetu ilipitia changamoto nyingi sana sana za kuumiza lakini nashukuru Mungu tupo hai mpaka sasa. Na Mungu kanijalia kazi nzuri, ninajitegemea na kusaidia ndugu zangu pale niwezapo. Nilianza kazi mwaka jana mwezi wa Tano, nikasave nikafanikiwa kununua kiwanja na kufikia hadi hatua ya kuweka msingi! Niliamua kufanya hivyo kwasababu familia yetu hatujawahi kuwa na nyumba yetu wenyewe ya kumiliki! Kwahiyo ni kitu kilichokuwa kinanipa wasiwasi sana vipi siku kikitokea cha kutokea tutaenda wapi? Hivyo nikalipa lengo langu hilo priority.
Lakini sasa kaka zangu bado wanabangaiza vibarua walivyo navyo vinawasaidia kula na nauli za kwenda vibaruani na mara nyingine hata inanibidi niwape mimi hata hela ya nauli na ya kula! Na ilifika kipindi cha kulipa kodi basi nitoe yote au niwachangie! Hili sio tatizo maana najua Mungu kanipa uwezo ili niwasaidie ndugu zangu.
Swali ni ‘niwasaidiaje kakazangu?’ ili waweze kusimama vizuri kiuchumi? Maana mmoja tulishawahi kumchangia mtaji lakini biashra ikawa ngumu ikafeli. Mwingine hana passion na biashra na haiwezi tu niseme ila kibarua chake ni cha kipato kidogo sana. Wanashindwa hata kuoa kwasababu hawako vizuri kiuchumi. Kiukweli naumiaga sana na ni kama inaniongezea depression nikiwafikiria! Kuna wakati nakwama lakini najua sina ndugu wa kumuomba msaada naumia sana!
Sasa naomba mnisaidie ushauri na maoni, niwasaidieje? Je, ina maana mimi kuendelea na ujenzi ilihali ndugu zangu hawako vizuri kiuchumi? Natamani nichukue mkopo niwape kwaajili ya biashara lakini vipi zikifeli maana tayari ilishafeli! Je, ni sawa kuwawazia sana?
Samahani kwa kuwachosha! Natanguliza shukrani.