Niuzie gari ya abiria

Niuzie gari ya abiria

lawyerrr

Member
Joined
Jun 20, 2017
Posts
66
Reaction score
60
Asalam alaykum ndugu zangu,

Narudi tena baada ya kutopata mafanikio katika uzi wa kwanza.

Bila kuathiri maelezo katika kichwa cha habari hapo juu.

Nahitaji kununua gari kwaajili ya abiria.Gari iwe nzima na iwe haina deni lolote, pia iwe haijarudiwa rangi wala kuwahi kugonga sehemu.Kwa kuzingatia masharti yaliopo kwenye aya ya pili ya Uzi huu, ofa yangu ni shilingi milioni tisa.

Weka gari na bei yako, nikiridhika na gari yako nitakupm kisha tubadilishane namba na hatua zingine zifuate.

Shukrani
 
Show room yapo mengi kulingana na sifa unazohitaji!!
 
Wabongo bana ana hela sawa na hela ya TRa alafu anaweka masharti 700..iwe nzima (mbona hela yako sio nzima), haijapigwa rangi (iweje sasa)

Acheni uswahili bana, huna hela unauziwa screpa, una hela agiza Jpn
 
Wabongo bana ana hela sawa na hela ya TRa alafu anaweka masharti 700..iwe nzima (mbona hela yako sio nzima), haijapigwa rangi (iweje sasa)

Acheni uswahili bana, huna hela unauziwa screpa, una hela agiza Jpn
Anataka gari la abiria!
Je anataka bajaji
-----taxi
-----hiace
Au?jamaa Bdo haeleweki bado

Ova
 
Unagari yoyote ya abiria weka hapa,huna acha maswali
Magari Hapa ndipo mahala pake.....ukitaka kuwekea magari utawekewa magari Hata 1000.....
Jibu Swali nlilokuliza kwanza!

Ova
 
Back
Top Bottom