Niulize chochote kuhusu Michael Jackson

Niulize chochote kuhusu Michael Jackson

The real Michael Jackson died in 1982??

you are not serious.....After 1982 michael alikuja na classics kubwa zilizobadilisha maisha yake ..mfano mzuri ni record zilizowekwa na album ya Bad na Dangerous..labda niwe nimekuelewa tofauti
 
Conspiracy Theories hazikosekani hasa kwa watu maarufu kama MJ.Hiyo documentary niliiona youtube kuwa kauawa na Freemasons na DMX kuwindwa all in all hizo ni theorioes.MJ alikuwa kutoka uanamuziki wa kawaida hadi superstar mkubwa sana kwa ubunifu aliokuwa nao tangu Jackson 5 hadi kuwa solo na alijiunga na Motown records ambayo ilikuwa lebo ya weusi na akatingisha dunia nzima.Tungo zake zenye akili nyingi na ujumbe mzuri zitadumu mpaka dunia itakapoisha na sasa wanamuziki wa sasa hawafikii hata kidogo kiwango chake katika utunzi,kuvaa,kucheza,productions za audio na video,management,uwekezaji n.k.Bahati mbaya ni kwenye mahusiano The Wacko Jacko hakufanikiwa.Kuhusu ishu ya rangi MJ alikuwa haupendi weusi ukiachana na hizo sababu za ugonjwa wa Vitiligo.Alifanya show kubwa ya kuitangaza Pepsi miaka ya 80 ambapo aliungua moto kichwani.Pepsi walimlipa fidia kubwa na ikabidi awe anavaa mawigi maisha yake yote yaliyobakia.Alibadili pua yake na rangi pia kwani alikuwa analala kwenye kitanda maalum ambapo anaweka kichwa chake katika kifaa maalum.Alichongwa pua miaka ya 1989,1990 na mara nyingi tu.Alifanya operesheni nyingi tu kurekebisha kidevu,mashavu,paji la uso macho na hiyo ni sababu ya usuperstar kuwa mashabiki watamuonaje.Kama mastaa wengine kama MARYLIN MONROE alijikuta anaingia kwenye uteja wa dawa za usingizi mpaka zikamuua.Baada ya kukaa nje ya game kwa muda mrefu sana na albamu zake kutovunja rekodi kama za miaka ya 1980s ilimuuma sana na kumsumbua.Mapromota waliandaa shoo kubwa sana yenye thamani kubwa ya THIS IS IT iliyokuwa ifanyikie ukumbi wa O 2 jijini London.Waliweka matumaini makubwa ya kutengeneza pesa nyingi na pia kumrudisha MJ kwenye chati yake hivyo ilimpa msukumo mkubwa.Tafuta videos za show ya Rehearsals za This is it utaona mzee alivyokuwa anawapeleka vijana kwa viwango vyake vya 1980s na alikuwa hafanyi mzaha .Hiyo pole pole ilipelekea kwenye kifo chake kwani alizidisha utumiaji wa dawa za usingizi.Alikuwa akimlazimisha Daktari wake Murray mtaalam aliyebobea katika fani ya dawa hizo amuongezee dose na dose mpaka zikamuua.NIKIRUDI NTAANGAZIA NYIMBO NA ALBAMU ZAKE.

asante sana kwa kujazia ila kama mpenzi wa Mj hilo jina la the wacko jacko lina maana iliyolenga kumdhalilisha sana ni vema tukamuita majina yake tuu
 
Je? ni mwaka gani alikuja kwa mara ya kwanza Tanzania?
Tunakumbuka uwanja wa ndege alipokelewa na Hassan Diria (R.I.P) huku akiwa amevaa uniform za umoja wa vijana ni nani alimshauri kuvaa vile?

alikuja Tanzania mwka 1992 kufungua kituo cha watoto wenye utindio wa ubongo pale sinza
 
alikuja tanzania mwka 1992 kufungua kituo cha watoto wenye utindio wa ubongo pale sinza

nashukuru kwa majibu yako mujarab,na ni nani alimshauri kuvaa uniform za umoja wa vijana? Na kile kituo bado kipo?
 
MJ ni legend hakuna atakayekuja kutokea kama yeye katika muziki wa pop.MJ ameuza nakala nyingi za cd hakuna atakayeuza zaidi tena kama yeye mpaka dunia inaisha hii ni kutokana na mfumo wa mauzo kubadilika kutokana na teknolojia.Yaani analoji hadi dijitali ambapo kwa sasa muziki unauzwa kupitia online stores na hivyo nakala za online ni nyingi kuliko za cd na tapes.Alipata platinums,double platmus na zaidi nyingi.Ni genious wa muziki ambaye dunia haijawahi kumuona kabla yake.Ni mwanamuziki pekee aliyependwa mno pande zote za dunia kuanzia Japan,Phillipines hadi Ulaya na Amerika ya kusini. Ni mwanamuziki pekee ambaye akifika kutumbuiza akipanda jukwaani kabla hajasema chochote mashabiki walimshangilia huku wakilia na kuzimia kwa dakika 45 au saa moja.MJ alitolewa na akina Diana Ross pia alikuwa best sana na marehemu Liz Taylor.Producer wake ambaye kamjengea jina,umaarufu na utajiri ni mzee mzima QUINCY JONES ambaye waligombana kuhusu hati miliki kiasi kwamba siku ya mazishi ya MJ QUINCY JONES alikuwa nje ya nchi ya Marekani lakini alikataa kurudi ili ahudhurie. Kwa ujumla MJ alinyang'anywa utoto wake na babaake JESSE JACKSON na ndio sababu kuu aliwapenda sana watoto,alitumia sehemu ya utajiri wake kwenye charities na philanthropist causes.

Hapo kwenye red ni Joe Jackson sio Jesse.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom