Nitumie mbinu gani?

Nitumie mbinu gani?

Tuanzie hapa we ni me au ke!!??

Wapenzi nimeangukia kwenye penzi jipya linanipeleka puta kiasi naanza kukosa kujicontrol kumpigia na kumtumia jumbe mpaka najistukia atanichoka au kuonekana msumbufu
Ombi langu naombeni mbinu za kuweza kupunguza hisia juu yake nipunguze kupiga simu na kutuma jumbe kwake.
Nisaidieni yaani nimekuwa teja kabisa hadi najihurumia.

 
Fanya kosa lolote uende jela,kule hutapiga Simu wala kupigiwa,zaidi utajifunza kuandika barua
Wapenzi nimeangukia kwenye penzi jipya linanipeleka puta kiasi naanza kukosa kujicontrol kumpigia na kumtumia jumbe mpaka najistukia atanichoka au kuonekana msumbufu
Ombi langu naombeni mbinu za kuweza kupunguza hisia juu yake nipunguze kupiga simu na kutuma jumbe kwake.
Nisaidieni yaani nimekuwa teja kabisa hadi najihurumia.
 
Ataweza kukaa bila bundle na hela mfukoni anayo? She is overwhelmed by the first intensive feelings of caring. Baada ya muda zitapungua automatically
aasante umemjibu kitaalamu zaidi katka kada yetu ya dark arts
 
Fanya kile kinachokufurahisha kwenye mahusiano wala usizuie hisia furahia sana kwa kadri uwezavyo yani ikibidi kuvaa nguo imeandikwa jina lake vyovyote vile fanya furahia wakati jitahidi mfikie ndoa mjenge familia hakuna fahari ipitayo penzi bora kwa wapendanao
 
Hiyo ya mwisho ndio concern yangu, Ahsante Lizzy
Fanya sehem yako mapenzi ni kitu kizuri sana ukianza kujizuia tu utakuja kulalamika kuachwa penda ukiamka penda ukilala penda ukiamka fanya hivyo wakati wote
 
Ke
Hivi mbinu zaweza kutofautiana kulingana na jinsi
If yes how and why
Huna haja yq kujizuia kuonyesha upendo we mpende tu akiona ni kero basi hayupo sawa kihisia na wewe. Mimi babe wangu anapiga sana simu na text yani haipiti 2 hour au 3 hajapiga amewahi kuniambia nahisi kama nakusumbua sana nikamwambia no it's okay jiachie sababu tunapendana.
 
Back
Top Bottom