Tatizo lako wewe ni mbishi...
Unapoambiwa wewe ni mdogo kuingia kwenye ndoa kubali. Yes una busara,
lakini hazitoshi kuhimili mikiki mikiki ya ndoa. Mfano mdogo ndio kama
yanayokukumba sasa. Ungekuwa na busara za kutosha wala yasingekuumiza
kichwa na akili kama yanavyokuumiza sasa.
Kwa umri ulionao huo ukienda nje ya ndoa ndio unaenda kujichimbia
kaburi.
Mimi nakushauri kitu kimoja. Kuanzia sasa anza kuishi kama vile
hujaoa. Usimuache mkeo, lakini pia usimchukulie kama mke. Mchukulie kama
rafiki tu anayeishi katika nyumba yako. Kama mna mtoto/watoto we peleka
care kwa watoto. Akinuna, akigomba, akilia, akicheka, usijali. Jali
maisha yako mengine, but usiwaze tena kuhusu ndoa yako. Kama ni kulala,
akikataa usilale kitandani, kalale chumba kingine au sebuleni. Usijaribu
kabisa kumuomba au kutaka kufanya naye mapenzi. Kama ni chakula
akipikupa kula, asipokupa kale kwa mama ntilie.
AMUA kuishi maisha kama hayo kwa muda utakaojipangia ama MIEZI 3 au 6.
Strickly that way, yaani usimjali kwa lolote. Kwa kifupi chukulia kama
hayupo humo ndani. Ni ushauri mgumu mgumu kidogo but matatizo magumu
yanahusu maamuzi magumu, maana usipochukua hatua, ama utaua au utajiua
au utakufa...