Nitavaa ped muda wote kuanzia leo

Nitavaa ped muda wote kuanzia leo

JEKI

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2013
Posts
4,845
Reaction score
2,966
Nikiwa nahudhuria kikao na wadau wengine katika sekta ninayofanyia kazi, tulipobreak kwa breakfast nanyanyuka huku nikicheka na wanawasha wenzangu, oh my God! damu zimejaa kwenye kiti na sketi yangu nyeupe ipo chepechepe, nimepatwa na mfadhaiko wa kutisha, nimeanza kubreak kabla ya wiki 1 na nusu ya muda wangu bila kutarajia, kuanzia leo nigeuza ped kuwa kama chup, nitaivaa siku zote ".

Hayo si maneno yangu bali ya mwanamke mtaani kwetu, aliyatoa katika hali ya mfadhaiko mkubwa.
 
"... Nikiwa nahudhuria kikao na wadau wengine katika sekta ninayofanyia kazi, tulipobreak kwa breakfast nanyanyuka huku nikicheka na wanawasha wenzangu, oh my God! damu zimjaa kwenye kiti na sketi yangu nyeupe ipo chepechepe, nimepatwa na mfadhaiko wa kutisha, nimeanza kubreak kabla ya wiki 1 na nusu ya muda wangu bila kutarajia, kuanzia leo nigeuza ped kuwa kama chup, nitaivaa siku zote ....".

Hayo si maneno yangu bali ya mwanamke mtaani kwetu, aliyatoa katika hali ya mfadhaiko mkubwa.

Mpe pole sana
 
dah hilo kweli ni tukio la kufedhehesha aliweza kurudi kwenyewarsha siku iliyofuata kweli?
 
mpe pole na asijali kabisa maana hayo ni mambo ya kawaida huwa yanatokea sana, na nini cha kushangaza hapo nani asiyejua kuwa mnasiku zenu, anaye cheka hana akili!
 
hapaswi kufadhaika kwa kuwa hakuna asiyejua kuwa hiyo ni sifa ya mwanamke na hiyo ni sawa na ajali kazini,hata sisi wanaume kuna wakati tunadindisha mpaka wanawake wanaona hata ukiwa unatembea inaonekana wazi lakini wanachukulia kawaida kwa kuwa ndio sifa yetu na kila mtu anajua pale kuna kiungo cha siri,hata ukimuona obama unajua pale kuna nini.

ila nahisi kutakuwa kuna tatizo maana haiwezekani kukawa na mabadiliko kwa zaidi ya siku kumi ghafla tu,aende kwa dakitar
 
uongo mtupu.yaani hadi ulowane usihisi kitu ? hakunaga

mimi si mwanamke lakini kibiolojia inawezekana,kumbuka unahisiana kwa sababu mfumo wa kuhisi unafanya kazi sawasawa lakini kama kuna tatizo huwezi kuhisi kirahisi,hujawahi kusikia unaweza kuugua na mfumo wa taarifa ukapoteza uwezo kiasi cha hata kuangukia na moto usijue mpaka uungue zaidi,pia inategemea na yeye mazingira aliyokuwepo ndio mana wakati mwingine kinatokea kitu unakuwa kama unahisi kwa mbali lakini usijue kama nini mpaka macho yaone
 
aah wapi haipo hivyo huwa unasikia hata kaunyevu unyevu unaenda kujichungulia chooni
 
mpe pole na asijali kabisa maana hayo ni mambo ya kawaida huwa yanatokea sana, na nini cha kushangaza hapo nani asiyejua kuwa mnasiku zenu, anaye cheka hana akili!

zimefika mkuu.
 
aah wapi haipo hivyo huwa unasikia hata kaunyevu unyevu unaenda kujichungulia chooni

usikalili, hata saa mbovu kuna wakati inapatia wakati au siku ya nyani kufa miti yote hutereza.
 
Hilo ni tatizo la kutumia pills bila mpangilio. Pole sana.
 
uongo mtupu.yaani hadi ulowane usihisi kitu ? hakunaga

wewe unadhani siku zote utasitukia kila kitu? hutokea siku usiyoijua likatokea jambo ukashangaa imekuwaje hadi hujasituka.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom