Nitauvunja vunja moyo wake soon

Nitauvunja vunja moyo wake soon

The Wolf

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2013
Posts
9,445
Reaction score
20,811
kwanza kabisa niseme sikuwa na nia hii ila itabidi, siyo kosa lake tatizo ni mimi.

Huyu binti nilikutana nae mwanzoni, mwaka huu, nilitokea kumtamani na kutamani kuwa nae hata kwa usiku mmoja tuu, nilifanikiwa kupata namba yake na kuanza mawasiliano.

Date ya kwanza ilienda vizuri na nilimrudisha anapokaaa salama baada ya kufurahi usiku kucha, kukaa nae na kuongea nae usiku huo nikatokea kumpenda, sikufanya nae mapenz aliniambia yupo period mapema na nilimkubalia.

Baada ya hapo kaja kwangu mara nyingi sana, tunapika na kula, na siku nyingine analala baada ya kumsikiliza story yake na malengo yangu nikaona kabisa hatupo njia moja alikuwa ametoka kuachwa na mshkaji wake, alikuwa kwenye maumivu makali nikachukua jukumu la kumpa faraja kuhakikisha hata mitihani yake anafanya vizuri ishu ni kwamba mtoto amenielewa na mipango yake yote ni mimi! Mimi mipango yangu ni mama mtoto ambaye natarajia kufunga nae ndoa mwezi may.

Nimefanikiwa kwa kiasi fulani kuishi double life, mke wangu mtarajiwa alishajua kuhusu huyu binti tukayamaliza, ila binti hajui chochote kuhusu kuwa na mke wala mpango wa ndoa. Last month nilimletea figisu tuachane akaniambia ntakuwa responsible kwa atakachokifanya hawezi kuishi, nikarudi nyuma.

Msinitupie mawe wakuu, naombeni ushauri nini cha kufanya kwa sasa, namna gani nimuache asiumie, binafsi ninampenda pia yani ninawapenda wote yeye na mke mtarajiwa kuoa ni lazima nioe mwezi wa 12
 
Anha unawapenda wote sio? Usipokuwa makini utakuwa na ndoa yenye mitihani mpaka utajihisi ni mwenye mikosi, kuwa na msimamo kijana, mpaka utapoingia ktk ndoa uwe na jibu moja, usijeoa huyu wakati mapenzi yapo kwa Yule na wakati unaona umeshakosea urudishe mapenzi kwa wife nae ushamvunja moyo anauza mechi kwangu labda..jitahidi kutuliza akili yako ndugu ndoa yataka busara sana, zaidi ya mihemko.
 
Mweleze ukweli mwisho mmalizie ulikuwa unampenda ndo maana imekuwa ngumu kwako
Mfanye aelewe kuwa yeye ndo kawakuta nyie mkiwa wapenz na si yeye kakutwa
Itampunguzia maumiv kidogo lkn
 
Mwambie ukweli (una mke) kama ulivyo tuambia hapa.
Baada ya hapo, kitakacho jiri ndipo ukuje utushirikishe na ndipo itapendeza tukikushauri.
Yaani namaanisha, anza na kumuelewa kwamba unamke na watoto, na mueleze kwamba ulimficha kwasababu ulikua unampenda na haukutaka kumkosa.
Reaction ya utakacho mueleza ndio uje uilete hapa ndipo tukushauri
 
Ni lazima kuoa au kuolewa ndoa za mitaala,
Atakaye kataa kifungo cha maisha jela,

Nafikiri hii sheria inatufaa sana!
 
Mweleze ukweli mwisho mmalizie ulikuwa unampenda ndo maana imekuwa ngumu kwako
Mfanye aelewe kuwa yeye ndo kawakuta nyie mkiwa wapenz na si yeye kakutwa
Itampunguzia maumiv kidogo lkn
Thanks mkuu
 
Back
Top Bottom