Nitatokaje kwenye hili janga?

Nitatokaje kwenye hili janga?

JF2050

JF-Expert Member
Joined
Sep 25, 2010
Posts
2,085
Reaction score
45
Kuna mtu huwa ananitumia Messages, mara ananisalimia, mara ananiambia forward kwa watu hamsini utabarikiwa, messages kibao zingine hazina kichwa wala miguu. Nikijaribu kuchunguza, kwa kweli hiyo namba ni ngeni, kwa maana kwamba kama vile sikupeana na mtu. Kila nikimpigia hapokei, nikikaa kidogo sms, ananiudhi! Siku moja nilimsms kumwuuliza wewe nani? Akanijibu una haraka ya nini, utanifahamu tu!

Nikaona niachane naye, maana huu ni wehu, nisubirie kumfahamu ili iweje hali ananisumbua na messages zake. Nikawa nimesave jina lake kwenye simu "Who?", halafu kila akituma sms nadelete bila kuisoma.

Sasa tulikuwa na mazungumzo sehemu ambapo niliamua kuweka simu yangu katika silence mode. Hata nilipoondoka hilo eneo la mazungumzo nilisahau kuondoa silence mode kwenye simu, nikawa natembea kwenda nyumbani. Kumbe huyo mtu ambaye hunitumia sms za ajabuajabu, akawa amenitumia picha WhatsApp ambayo kwa kweli siwezi kuielezea, imeambatana na ujumbe "karibu Apple, samahani lakini".

Kwa bahati mbaya nikiwa natembea huku simu ikiwa kwenye mfuko wa suruali, hiyo message ikawa imejituma kwenda kwa watu kadhaa akiwemo Boss wangu (ni mwanamke).

Sikujua kama yule mtu amenitumia picha ya namna hiyo, mpaka pale nilipofika nyumbani na kuangalia simu na kukutana na missed calls lukuki, za Boss zipo 21, na za watu wengine pia. Bahati nzuri message haikwenda kwa wazazi. Kulikuwa na missed call ya Boss hadi mida ya saa tano kasoro.

Sasa kuna mgongano ulishawahi kutokea kati ya mimi na Boss, ingawa nilimwomba msamaha, lakini alichukua muda kuamini kwamba ilikuwa ni bahati mbaya. Kwa kweli kwa hii picha sijui itakuwaje!

Wadau naombeni ushauri namna ya kujinasua maana naona hii issue yaweza kuwa nzito! Sijajibu chochote mpaka sasa, nafikiria labda nizime simu na kesho akiniuliza nimwambie simu nimeibiwa tangu jana mida ya jioni, lakini nashangaa kuna muda nilikuwa napiga inaita! Picha yenyewe nimeiattach.
 
na kushauri acha kutumia masimu ya kichina,,,m screen una respond adi ukiguswa na fabric, kucha chuma kama coins,,njoo smartphones kama ma galaxy,,kitu mpaka kidole joto lake ndo kina respond
 
mkuu samahani lakini naomba unijibu hili swali we ni mjasiliamali au mtumishi?
 
Pray to God n say ur story if they don't believe it then utakuwa mweupe rohon! Pole sama
 
mmh kwa mfumo wa whatsapp ilivyo ni wachache watakao amini hii labda kama ingekuwa massage ya kawaida.

Hii mimi siwezi kuamini.

hapo hata mimi siamini kwa 100% hii whatsapp nayoijua? Hapana haiwezekani
 
mkuu samahani lakini naomba unijibu hili swali we ni mjasiliamali au mtumishi?

hahaha wazungu wanasema ukiwa mkweli uwe na kumbu kumbu.

1."mjasiliamali"?(yesterday)

2."kuna mgongano ulisha tokea kati yangu na boss"?(today)

hahaha
"NMB MOROGORO BRANCH"
 
ha ha ha ha haaaaaa naomba nikupe mji,maana hadithi cjaielewa inamaanisha nini.....nenda fb labda wapo watoto wanasikilizaga hadithi hizo..
 
una2mia mchina nini..!?maana whatsapp hilivyo swala hilo wala haliingi akilini.......uongooooooooo uacheeeeeeeeee.
 
Ruttashobolwa na omary mwene. Huwa nashauri mara nyingi kwenye swala la teknolojia usikurupuke, hata engineers walio artect simu au whatsApp kama ningeripoti hili tatizo kwao, wangechukulia kama huenda ni flaw aidha ya app au simu na kurespond kwa kufanya tech review. Hapa huwezi jua kama tatizo lipo kwenye simu au WhatsApp, Smartphones (sio za kichina) nyingi tu zinakutwa na flaws kibao na zinarepotiwa na kufanyiwa kazi!

Rutta, whatsApp msg sio message ya ajabu kama unavyotaka kudai, ni ya kawaida: WhatsApp Messenger App for Android (reviewed).

Ufanyaji wa kazi wa WhatsApp usidhani unafanana kila simu/platform, bali inategemea na mambo kadhaa, mfano: ulivyofanya settings, sychronization/embedment na apps zingine, contact integration (unaweza kwa mfano kutuma message, file, etc., kutoka WhatsApp kama email, text, n.k).

Njoo na technical grounds kwamba haiwezekani, sio kwa sababu uko na nyumba ndogo yako imekupa pauchi umelewa na wewe ukakurupuka na kupost!

Nimetafuta solution ya hili swala, wakati nagoogle nimekutana na watu wengi tu waliopata tatizo kama hili, mfano:

I`ve accidentally sent a whatsapp message from an iPhone to the wrong person they are not online and it only has 1 tick, is there anyway of deleting i - Is there anyway of deleting a whatsapp message sent from 1 iPhone to another, before they read it
 
Last edited by a moderator:
Ndo hapo sasa.....subir nilale

Sijajua kitu gani hakieleweki. Jana nilikuwa Moro, na walioniPM tumeweza kukutana (wewe ulitaka nikuambie exact place ili uje kuniwinda na mishale!), we had funny anyway.

Kuwa mjasiriamali hata kama ni mfanyakazi kwani haiwezekani? Kukosana na Boss (halafu je Boss lazima awe wa ofisi za serikali? Kama mna kikundi chenu cha ujasiriamali, mtu ambaye yuko juu yako sio Boss?) wako nacho ni kitu cha ajabu? Sijawaelewa. Unaweza kuwa unasoma, umejiajiri/umeajiriwa, mjasiriamali, etc., tatizo ni nini!
 
hahaha wazungu wanasema ukiwa mkweli uwe na kumbu kumbu.

1."mjasiliamali"?(yesterday)

2."kuna mgongano ulisha tokea kati yangu na boss"?(today)

hahaha
"NMB MOROGORO BRANCH"
Alikuwa anataka kutuletea hilo apple lakini akawa hana cha kuandika. Ungepeleka kwenye jamii photos kulikoni kutupotezea muda kusoma u.......zi wako hapa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom