chelsea fc
JF-Expert Member
- Nov 10, 2011
- 864
- 213
Hiyo imekuwa ni kauli ya mke wangu,niliyezaa naemtoto mmoja,ambaye ana umri wa miezi 9.Kauli hiyo amekuwa akiitoa mara kwa mara hasa kunapotokea ungomvi(mara nyingi unatokana na wivu mwingi alo nao) wa aina yeyote ile unaopelekea kupigana.
Hayo maneno ya kuwa ipo siku ataniua ,nimekuwa nikijiuliza sana,endapo anamaanisha au ni hasira tu!!Kila nikitafakali na kuangalia mwenendo wake na tabia yake, nashindwa kuelewa km ni kweli hilo suala lipo kichwani mwake kwa maana ipo siku atalitekeleza ua la!!.ni miaka 3 imepita tangu tuanze maisha na huyu mke wangu.
Suala hili nalileta kwenu JF MEMBERS,mnipe walau mwanga wa nini nifanye juu ya hii kauli ya mke wangu.
Natanguliza shukrani kwa mchango wenu wadau.
baby umeona e? tuendelee kuchunga ndimi zetu kwa lugha ya upendo
ni sahihi kabisa
Aisee kama ni mmachame jua anamaanisha
ni kweli ,ila kukosana ni kwa kawaida,ila siyo mpaka umwambie mwenzio kuwa utamuua.na siyo mara moja,ni kila mara,umekuwa km wimbo
mkuu ukishamchukulia RB huyo si mke tena bali ni muhalifu, jee inawezekana kweli unakaa, kula na kula ya muhalifu... itakua hamna ndoa tena hapo. Hizo kesi niza kawaida sana kwa sisi wazoefu, atakute shida ilianza wapi, ajaribu kukaa ma mkewe kwa ukaribu zaidi, amuonyeshe mapenzi ya kweli hata kama ana stress za kimaisha basi amshirikishe mkewe hadi mke aone thamani yake kwa mumewe, ni ngumu lakini inawezekana, sisi tumeshapitia huko kote na tuko salama tu....chukua RB kabisa umuonyeshe,ili ajue siku nyingine aanze kujicontrol
Aisee kama ni mmachame jua anamaanisha
Mimi Nina tabia ya kukaa kimya, ni ngumu sana Hasa pale unaposingiziwa kitu au kuambiwa lugha za maudhi. Thank God I always swallow them na Nina hakikisha siku hio nasali mwenyewe, ukitaka amka tusali hutaki endelea but nahakikisha nasali as usual Kisha nalala.
Kama ntajiskia kuduu basi ntafanya hivyo bila kujali chochote. ILA jamani MAOMBI yanasaidia tuacheni utani.....
Paloma utumie hii dawa na wewe pia