Nitafikaje Kisiwa cha Saa Nane Mwanza

Nitafikaje Kisiwa cha Saa Nane Mwanza

Jambo Tz

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2013
Posts
670
Reaction score
203
Nahitaji kufanya utalii Mikoa kanda ya Ziwa na hasa Mwanza kwenye visiwa vya Saa Nane , Ukerewe, na kupacha chakula pale Malaika
kwa wale wenyeji nifahamisheni kufika sehemu hizo
 
Malaika ipo Ilemela, kama km 5 hivi toka airport pinda kulia nenda na barabara ya vumbi.Ukerewe panda boti zipo maeneo ya kirumba TSH 7, hivi hadi Ukerewe mwendo wa saa 2 hivi majini. Ukifika tuwasiliane.Kisiwa cha saa 8 hakuna issue labda kama unataka kupoteza hela zako bure.....utabahatisha nyani, sungura na mbweha.
 
....yeye kataka kwenda huko, nyie mnaona hapana maana kivipi, utalii haupo hivyo, kwani wanoenda picnic kwenye mapori ambayo hayana kitu huwa hawa enjoy?, huenda hata hao nyani na pimbi hajawahi kuwaona, nyie muacheni aende ni kuzuri tu, mstake kuleta kupajuajua sana, na huenda mnaishi mwanza na hamjawahi hata kufika. ndugu ww nenda kisiwa kipo hapo mwanza karibu kabisa na mjini, naul pamoja na kiingilio haizidi hata elfu mbili maana sijui kwa sasa, fika maeneo ya tilapia hoteli
 
....yeye kataka kwenda huko, nyie mnaona hapana maana kivipi, utalii haupo hivyo, kwani wanoenda picnic kwenye mapori ambayo hayana kitu huwa hawa enjoy?, huenda hata hao nyani na pimbi hajawahi kuwaona, nyie muacheni aende ni kuzuri tu, mstake kuleta kupajuajua sana, na huenda mnaishi mwanza na hamjawahi hata kufika. ndugu ww nenda kisiwa kipo hapo mwanza karibu kabisa na mjini, naul pamoja na kiingilio haizidi hata elfu mbili maana sijui kwa sasa, fika maeneo ya tilapia hoteli

Kweli Mkuu Assistant Tutor lengo la mwanzisha uzi anataka kufanya utalii maeneo ya kanda ya ziwa kwahiyo kufika kisiwa cha saa nane ambapo wapo pimbi,swala na tumbili pamoja na mazingira ya kisiwa hicho inatosha.
 
Last edited by a moderator:
Malaika ipo Ilemela, kama km 5 hivi toka airport pinda kulia nenda na barabara ya vumbi.Ukerewe panda boti zipo maeneo ya kirumba TSH 7, hivi hadi Ukerewe mwendo wa saa 2 hivi majini. Ukifika tuwasiliane.Kisiwa cha saa 8 hakuna issue labda kama unataka kupoteza hela zako bure.....utabahatisha nyani, sungura na mbweha.
Mkuu toka airport hadi kwenye hiyo kona ni kama km 2 tu,na barabara yake si vumbi tena,ni mkeka tu mpaka malaika
 
....yeye kataka kwenda huko, nyie mnaona hapana maana kivipi, utalii haupo hivyo, kwani wanoenda picnic kwenye mapori ambayo hayana kitu huwa hawa enjoy?, huenda hata hao nyani na pimbi hajawahi kuwaona, nyie muacheni aende ni kuzuri tu, mstake kuleta kupajuajua sana, na huenda mnaishi mwanza na hamjawahi hata kufika. ndugu ww nenda kisiwa kipo hapo mwanza karibu kabisa na mjini, naul pamoja na kiingilio haizidi hata elfu mbili maana sijui kwa sasa, fika maeneo ya tilapia hoteli

Kaka nashkuru saaana kwa mchango wako
 
nashkuru kwa mchango mlo nipa ila kuna watu bado hawajajua matumizi sahihi ya hii mitandao but wata jua tuu
 
Kweli Mkuu Assistant Tutor lengo la mwanzisha uzi anataka kufanya utalii maeneo ya kanda ya ziwa kwahiyo kufika kisiwa cha saa nane ambapo wapo pimbi,swala na tumbili pamoja na mazingira ya kisiwa hicho inatosha.

Mkuu, kweli tuna safari ndefu sana.

Ukiachia mbali nia ya Mleta Uzi ya kwenda Saa Nane kwa utafiti, tarehe 04/09/2013 Saa Nane ilipewa hadhi ya Hifadhi ya Taifa ya Saa Nane (SAA NANE NATIONAL PARK)!!

Mbali na maboresho yatakayofanywa ikiwemo kuingiza Wanyama kadhaa, Saa Nane na Rubondo kuna Uoto wa Asili ambao ni kivutio tosha kabisa kwa utalii hasa wa ndani.

Kwa "Bird Watchers", Saa Nane ni moja ya maeneo machache hapa Tanzania yenye hazina ya ndege!

Bila kusahau safari ya Kapili-Mposhi (Kapri Point) - Saa Nane kwa kutumia mtumbwi mwepesi (fiber boat) ni "experience" ya aina yake.

Hivyo, mtu anapochangia kuwa "Saa Nane hakuna ishu" ninatamani kujua vigezo anavyotumia!
 
Last edited by a moderator:
I went there two months ago.it is very beatiful place.go my cousin and you wont regret!
 
Natamani sana kufika huko saa 8 nasikia kisiwa kina sq km 2.1 hata kama hakuna wanyama bado ni utalii.
 
....yeye kataka kwenda huko, nyie mnaona hapana maana kivipi, utalii haupo hivyo, kwani wanoenda picnic kwenye mapori ambayo hayana kitu huwa hawa enjoy?, huenda hata hao nyani na pimbi hajawahi kuwaona, nyie muacheni aende ni kuzuri tu, mstake kuleta kupajuajua sana, na huenda mnaishi mwanza na hamjawahi hata kufika. ndugu ww nenda kisiwa kipo hapo mwanza karibu kabisa na mjini, naul pamoja na kiingilio haizidi hata elfu mbili maana sijui kwa sasa, fika maeneo ya tilapia hoteli
Nani ambaye hajafka Mwanza? Si bora akajianike kwenye jiwe la Bismark acheki ferry la Nyehunge!
 
Malaika ipo Ilemela, kama km 5 hivi toka airport pinda kulia nenda na barabara ya vumbi.Ukerewe panda boti zipo maeneo ya kirumba TSH 7, hivi hadi Ukerewe mwendo wa saa 2 hivi majini. Ukifika tuwasiliane.Kisiwa cha saa 8 hakuna issue labda kama unataka kupoteza hela zako bure.....utabahatisha nyani, sungura na mbweha.

nafurahia sana ndugu
PM
 
Enenda usiwe na shaka. Usisahau kurudi na sato wa kutosha......

Mwanza Pazuuuuuuri nimepakumbuuuuuuuuka hakika natamani kuishi ndani ya mjii huuu ulozungukwa na Majabali makubwa
watu wake wengi ni wakareeeeeemu kila kitu ni ndoho tabuuu
hali ya hewa ni yakuvutia
Naaaam safari yangu nyingine mwanzaaaa
 
Back
Top Bottom