Nissan Leaf 3rd gen imeshazinduliwa: Bonge la improvements kutoka kwenye matoleo yaliyotangulia!

Nissan Leaf 3rd gen imeshazinduliwa: Bonge la improvements kutoka kwenye matoleo yaliyotangulia!

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
31,139
Reaction score
88,800
Nissan wako serious sana kwenye issue ya EV na hybrids hivi karibuni. Kwa sisi wapenzi wa magari madogoa na economy, wametugusa sana na Nissan Note (hybrid) na Nissan Ariya (EV).
021-2026-nissan-leaf.jpg

Sasa wametuletea all new Nissan Leaf 3rd gen, soon inaingia masokoni.
027-2026-nissan-leaf.jpg

Wamefanya mapinduzi makubwa sana kuanzia architecture mpya, muonekano wa nje na ndani na charging systems.
014-2026-nissan-leaf.jpg

Kwa kuanza na charging systems, Nissan wameachana na ile outdated system ya CHAdeMO na sasa wamekuja na system mpya ya J1772 kwa AC charging (ambazo zimesambaa sana na magari mengi yanatumia) na upande wa pili kuna port ya NACS kwaajili ya DC Fast Charging ambayo unaweza kutumia hadi charger za Tesla.
010-2026-nissan-leaf.jpg

Pia Leaf kwasababu sahivi ina betri kubwa, unaweza kuconnect appliances za umeme moja kwa moja (V2L) ila iko limited to 3.5 kWh AC output. Kwa lugha nyepesi, ukienda camping na hili gari, unaweza pika wali kwa rice cooker (1kWh) bila shida.
013-2026-nissan-leaf.jpg

Hapo kwenye battery, Leaf wameipa battery mbili 52 kWh (ili ndio dogo, zamani dogo lilikua 40 kWh) na 75 kWh (ili ndio kubwa, zamani kubwa ilikua 60 kWh) zote ni Lithium -ion na zote ni Liquid cooled. Hii ni bonge la step ukifananisha na air cooled za matoleo yaliyotangulia. Technology ya liquid cooling inasaidia sana kwenye battery management na inapelekea battery likae muda mrefu zaidi.
012-2026-nissan-leaf.jpg

Range imeimprove kama zilivyo battery, sasa hivi zinaenda hadi kilometa 480 akwa single charger kutegemeana na trim.
026-2026-nissan-leaf.jpg

Bei itakua kati ya $29,000 hadi $35,000 ambazo ni bei nzuri sana kwa features wanazozitoa.
 
Kabisa mkuu kama watu bado wanunua rav4massawe ya mwaka 1998/1999 kisa kikokotoo cha tra wafanye nini mkuu,ushuru wake hapo unapata ist 10
Mimi pia huwa naangalia ushuru kwanza harafu nafata bei ya gari maana kama SA gari nyingi zipo chini ukinunua kwa kulipemda ukija kuangalia TRA wanataka ngapi na gari ushanunua unabaki kusonya tu..
 
Mimi pia huwa naangalia ushuru kwanza harafu nafata bei ya gari maana kama SA gari nyingi zipo chini ukinunua kwa kulipemda ukija kuangalia TRA wanataka ngapi na gari ushanunua unabaki kusonya tu..
Acha tu mkuu, niliipenda gari volvo s60 nikaona naimudu bei, nikasema ngoja niingie kwenye kikokotoo cha tra, kwa kweli niliishia kulaani tu maana ushuru wake ulikuwa mara mbili ya bei.
 
Acha tu mkuu, niliipenda gari volvo s60 nikaona naimudu bei, nikasema ngoja niingie kwenye kikokotoo cha tra, kwa kweli niliishia kulaani tu maana ushuru wake ulikuwa mara mbili ya bei.
Ilikua ya mwaka gani Volvo haipo kwenye kundi la kodi kubwa na pia ili usiingie mkenge mtumie ofisa wa TRA/ agents aweke chassis number ajue kodi harisi maana kwenye mtandao wao ni mwaka ukija na gari wao wanatumia mwaka na chassis hapo ndio mtihani mwingine na ukitoka ushuru wa chassis ni sawa ila kwa mwaka ni mtihani hapo..
 
Ya kawaida kabisa
Kuliko gari zipi tunazotumia mkuu gari nyingi vitu vya kubonyeza vipo ndani kama Haval za China katoa gari kaburu mwenyewe anakimbizwa jinsi alivyoweka vitu vingi ila ukiiangalia kwa nje utasema zipo sawa na gari fulani kujua gari ya kawaida au sio ya kawaida kwa matoleo mapya ni uitumie sio kwa macho..
 
Kuliko gari zipi tunazotumia mkuu gari nyingi vitu vya kubonyeza vipo ndani kama Haval za China katoa gari kaburu mwenyewe anakimbizwa jinsi alivyoweka vitu vingi ila ukiiangalia kwa nje utasema zipo sawa na gari fulani kujua gari ya kawaida au sio ya kawaida kwa matoleo mapya ni uitumie sio kwa macho..
Jamaa wanawekeza aana kwenye R&D, inabaki kua gari ya kawaida yes kwakua ina matairi manne, ila ziko na technology ya hali ya juu.
 
Back
Top Bottom