nisaidieni sample ya mkataba nauza nyumba

nisaidieni sample ya mkataba nauza nyumba

superfisadi

JF-Expert Member
Joined
May 22, 2009
Posts
553
Reaction score
54
jamani wanasheria nisaidieni sample nauza nyumba nimeelezwa gharama za lawyers ni kubwa nisaidieni chonde chonde
 
nashukuru ila nimejaribu kufungua inashindikana umeme ukirudi nitaifungua thu pc
 
jamani mbona mnanipotezea wakati nahitaji msaada , watu wakianzisha mada za malavidavi mnazichangia kwa muda huu ingekuwa pg ya tatu km si ya tano nisaidieni mbona mnakuwa hivyo
 
jamani mbona mnanipotezea wakati nahitaji msaada , watu wakianzisha mada za malavidavi mnazichangia kwa muda huu ingekuwa pg ya tatu km si ya tano nisaidieni mbona mnakuwa hivyo
Acha ubahili,nenda kwa mwanasheria,atakuandikia mkataba kufuatana na matakwa yako.gharama ya mwanasheria inafuatana na thamani ya unachouza.kuwa mwerevu ndugu.pia usisahau kulipa kodi ukishauza,nchi yetu inategemea kodi kuendesha hospitali na huduma nyinginezo.

haya download sample ya mkataba wa mauzo.
 

Attachments


Hii Attachment ya contract document usiichukulie kama ilivyo kwa vile hiyo ni ya sheria za Marekani. Kila nchi ina sheria zake kuhusu ardhi na nyumba.
Nakushauri nenda wizara ya ardhi watakusaidia dondoo za kuandika mkataba wa kuuza nyumba yako. Ukitumia wanasheria utadaiwa asilimia kadhaa ya mauzo ya nyumba iende kwao.
Afadhali wape posho kidogo watu wa ardhi na asilimia zote utaingiza mfukoni mwako.

Utaratibu mwingine ambao ni gharama nafuu unaweza kuandika mkataba wako mwenyewe na ukampa mnunuaji asome na akikubaliana na yaliyomo basi nendeni pamoja mahakamani mkatie sahihi mbele ya hakimu na hakimu akishatilia sahihi huo ni mkataba wenye nguvu kisheria tayari. Hiyo ni njia wengi wanatumia, na mimi nimeshawahi tumia njia hiyo.
 
Hamna namna ni wakati wa kuuza tulivyo navyo, hali imebana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom