Nisaidieni, naweza kufa kwa mawazo

JANFE

Member
Nov 10, 2015
21
106
Mimi ni mwanaume,
Nimefikiria sana mambo mengi, nimepitia uzoefu mgumu sana maishani, kijamii na kimahusiano.
Kimaisha (uchumi) sijafeli sana, niko vizuri. Ila kwa changamoto nilizopitia, nimekuwa na mtazamo tofauti kuhusu maisha.
Nimejikuta nachukia wanawake kuliko maelezo, nikimwona mwanamke naona kama jambazi anapita pembeni yangu.
Nimejawa na roho ya ukatili na kisasi. Kitu kinachoitwa mapenzi kwangu ni kama hadithi (myth).

Nilipogundua hali yangu nikaamua kuwa busy na shughuli za kiuchumi, lakini naona hakuna nafuu. Siwezi kueleza yote hapa nishaurini nifanyeje nirudishe ubinadamu wangu na furaha yangu. Naumia sana

Updates!!!!
Nashukuru kwa ushauri, kejeli na mitazamo yenu.
Kwa ujumla Mambo yaliyoniumiza sana katika maisha yangu ni;
  1. Ndoa haiko vizuri. Matarajio yangu kwa niliyempenda na nilivyokuwa namfahamu, yamegeuka kuwa jehanamu ndogo. Sina furaha wala hamu tena, ninapotazama nyuma na nilipo, majuto yananiumiza. Sometimes nawaza kuwa nilifanya makosa fulani katika kufanya maamuzi, sasa ndo yananigharimu.
  2. Pale nilipoamua kujiliwaza kwa kutafuta relief kwingine kila mara huishia kwa maumivu zaidi kuliko faraja. Maumivu ya kutendwa ni afadhali ya jana.
  3. Sioni faida ya elimu yangu niliyoisotea muda mrefu, wala mali ninazomiliki.
  4. Nimegundua ni vigumu sana kumweleza rafiki wa karibu sana ambaye unadhani ni msaada, kumbe ni wanafiki. Sasa kubaki na majipu moyoni naona nakaribisha kifo bila kujielewa.
 
Pole sana ndugu JANFE kwa yote unayopitia,na inavyoonekana kwamba wanawake ndo wamekutenda mabaya mengi, jambo la kufanya badili tu mtazamo wako ili uweze kubadili unavyowaza na kuongea, na hili kwa namna ya kibinadamu ni ngumu ila jitahidi kwa imani ya dini uliyonayo Rudi kwa muumba akuwezeshe hili,ukiwa mtu wa Ibada na kusoma neno hakika chuki haiwezi kukaa ndani yako.

Pili wasamehe wanawake wote hii si kwaajili Yao Bali kwa faida yako binafsi,wanawake wazuri na wema bado wapo wengi tu omba uongozi wa Mungu akukutanishe nao wala hutajuta maishani mwako.
 
Last edited by a moderator:
Kuna njia kuu moja nzuri sana ya kusahau.

Yazungumze hayo yanayokukera na yaliyosababisha ukawa na chuki kwa wanawake. Namna unayazungumza ndivyo yanavyotoka na unapata relief.

Kitu kingine yawezekana uko busy na uchumi lakini Mungu wa kweli hauna muda naye. Sina uzoefu na wenzetu waislam wanakabiliana vipi na mambo ya kiroho, lakini kwa wakristo ukikaa karibu na Mungu na kujihusisha na mambo ya Mungu, lazima vitu vidogo vidogo vitaondoka vyenyewe. Siongelei mtu anayesali siku ya mwisho wa juma tu, naongelea yule mtu ambaye yeye kwake kila siku ni ibaada na moyo wake anamtegemea Mungu. Ukifanya hivyo Mungu anaweza kukutua huo mzigo maana Mungu aliumba mwanaume na mwanamke kwa makusudi iweje wewe umchukie mwanamke??
 
Mimi ni mwanaume,
Nimefikiria sana mambo mengi, nimepitia uzoefu mgumu sana maishani, kijamii na kimahusiano.
Kimaisha (uchumi) sijafeli sana, niko vizuri. Ila kwa changamoto nilizopitia, nimekuwa na mtazamo tofauti kuhusu maisha.
Nimejikuta nachukia wanawake kuliko maelezo, nikimwona mwanamke naona kama jambazi anapita pembeni yangu.
Nimejawa na roho ya ukatili na kisasi. Kitu kinachoitwa mapenzi kwangu ni kama hadithi (myth).

Nilipogundua hali yangu nikaamua kuwa busy na shughuli za kiuchumi, lakini naona hakuna nafuu. Siwezi kueleza yote hapa nishaurini nifanyeje nirudishe ubinadamu wangu na furaha yangu. Naumia sana

Waswahili wanasema, "Mficha maradhi kifo humuumbua". Sasa kama kweli wewe unahitaji msaada kutoka kwetu yakupasa uwe muwazi na mkweli. Funguka, eleza yanayokusibu bila kuficha chochote ili tujue namna ya kukusaidia.
 
Pole sana kwa hali unayopitia.

Kuna maneno kutoka katika kitabu cha mapokeo yanasema "Bwana kama wewe ungalihesabu makosa ni nani angesimama? Lakini kwako Kuna msamaha ili wewe uogopwe"

Ni jambo gumu sababu kila mtu huguswa na matatizo kwa namna yake lakini lililo muhimu ni kujifunza kusamehe. Unaumia na unaendelea kuteseka sababu hutaki kusamehe. Jifunze kusamehe ili moyo upumue.
 
JANFE pole kwa hali uliyonayo unasumbuliwa na uchungu mkuu
 
Last edited by a moderator:
Hizo huwa ni dalili za mwisho kabisa za kufa. Tubu dhambi zako na kumwomba Mungu apost pone.
 
Back
Top Bottom