Habari zenu hii ni mara yangu ya kwanza kuingia katika mtandao huu naomba mnipokee. licha ya ugeni wangu ila nimekuja nina shida nahitaji mawazo yenu.
Mimi ni msichana wa miaka kati ya 25-30, nimekuwa na mwanaume ambaye tumekuwa na urafiki wa kimapenzi sasa ni muda wa mwaka mmoja na miezi nane, huyo jamaa yeye ni raia wa Kenya.
kwa mara ya kwanza nilivyokutana nae aliniaweka wazi kuwa anawatoto wawili wa kiume na wakike ila akaniambia kuwa mke wake alimkimbia na aliolewa na mwanume mwengine.
Nilimpokea yeye na watoto wake ingawa watoto walikuwa Kenya ila nilichukua nafasi ya mama kwa kuwafanyia hata shopping na kutuma vitu kuwafikia huko walipo.
katika familia yao wanaonifahamu ni wadogo zake na kaka zake na wajomba zake ila plan zetu ilikuwa mwezi wa sita mwaka huu niende nae kwao, lakini ilivyofika aliondoka akaniambia alipata msiba hivyo anakwenda kuzika itakuwa siyo vizuri kuna msiba na yeye ndiyo anipeleke kwa mama yake kama kunitambulisha.
Nilikubaliana naye ila cha ajabu alikaa huko miezi miwili lakini hakukuwa na mawasiliano kama ilivyokawaida katika hiyo miezi miwili alinipigia simu mara tano tuu.
Baadae alirudi na alivyokuja aliniomba msamaha kuwa simu yake ilipata matatizo, sikujibu kitu nikaamua kufanya uchunguzi. mwezi huu wa nane nimegundua kuwa huyu jamaa anamke na watoto wanne, nilijua kwa kuchukua passport yake na kuangalia kule nyuma kuna vitu amejaza.
Nikazipiga zile namba nikaongea na huyo mwanamke aliumia sana mama wa watu alilia sana kwenye simu kiukweli nilijisikia vibaya sana akanimbia huku nilipo inafikia kipindi mimi na watoto tunalala njaa, kumbe yeye anafanya starehe huko, nikamjibu kwa kweli mimi nimekuwa msaada sana kwa watoto wako kwani hata ada za mwaka huu mimi nimetoa kwa kuwa jamaa mambo yake hayakwenda vizuri.
Yule dada akaniambia nimpe muda then atanijibu, ila baadae akanipigia akaniambia yeye ni mama wa nyumbani hana kipato chochote basi niendelee tuu kumsaidia ila hakugusia swala la mume wake.
Baadae nilikaa na huyu mwanaume nikamuuliza kwanini alinificha muda wote huo kama anamke akadai kuwa kuna matatizo ya kifamilia hivyo nimwachie yeye anajua jinsi ya kuyatatua, nilimkomalia sana inabidi aniweke wai kuwa yeye aliplan toka mwanzo kuwa awe na wake wawili mmoja kwa kuwa hana kazi basi wapili akiwa na kazi watasaidiana kwenye maisha.
Wapendwa mimi naombeni ushauri licha ya nyumbani kwetu nikimanisha wazazi wanajua ni rafiki yangu na plan zetu ilikuwa mwezi wa tisa aje kujitambulisha rasmi, sasa wapendwa kwa uongo wote huo huyu ni mwanaume sahihi?
Kitabia ni mpole ila sasa amekuwa na tabia ya kuwa na wasichana wasichana wengine napo nilipo mbona akaniambia ni wasichana anawapata kwenye mtandao wa Twoo na nisipokuwepo kwake anawapeleka hao wasichana hadi kwake.
Naombeni ushauri wenu nifanyeje anadai sheria ya kwao inaruhusu wake wawili ila dini yetu hairuhusu hivyo, na mimi mwenyewe siko tayari kuwa mke wapili, ila muda mwingine naona kwakuwa ameshanipotezea muda simwezi kupata tena mtu mwingine na miaka inakimbia.
Na umri wa huyu mwanaume ni kati ya 40-45