The Technologist
JF-Expert Member
- Jun 7, 2015
- 1,043
- 2,194
Mkuu vizuri, ni sahihi, Yesu ndiye Jehovah/Yahweh na nimefurahi kwamba unaujua ukweli huo.Huyo umwitaye Lord Jesus Christ ni Lord God Jehovah! Ana majina MENGI. Hata Allah, Buddha, Jah, Yahweh, yote ni yake.
Sichukulii imani kuwa suala jepesi. Ninachozungumzia ni kwamba WAZAZI HAWANA NAFASI katika kuwachagulia watoto wao waume/wake zao katika UWANDA WOWOTE ULE, iwe suala la kabila, rangi, itikadi AU DINI!!!
Upo hapo? Wanaweza kuwa na imani/dini tofauti kila mmoja akaishi kwa imani/dini yake na hakuna kinachoharibika.
Nilizaliwa kwenye "Uislam wa jina", nikaoa Mkatoliki. Nilipoingia kwenye Ukristo iikuwa jambo jepesi kuwa Mkatoliki. Mwenzangu akabadilika, ndoa ikavunjika. Nilibadilika kutoka kwenye "uritadi" (tayari nilikwisharitadi) na kuwa Mkatoliki Mpenda Yesu. Mwenzangu ALIMPENDA "Muislam wa Jina" kwa kuwa hakuujua ukweli!
SIPENDI KUMCHAGULIA MTU IMANI YAKE. Waachieni waoane kwani maisha ni yao!
NIMEMALIZA!
Ila Allah ni mungu mwingine na Budha ni mungu mwingine hawana uhusiano wao kwa wao wao wala hawana uhusiano naYesu Kristo.
Unajua kila kitu kina utaratibu wake, na wazazi wanapotoa hayo maoni yao wanawasilisha utaratibu wa dini husika!
Hivi ulijua kibiblia mchina haruhusiwi kuwa na ndoa na mzungu, mwafrika haruhusiwi kuwa na ndoa na mzungu vivyo kwa mhindi, mkorea n.k.
Kama Allah angekuwa Yesu iweje aseme ktk Qurani kuwa, Yesu hakufa msalabani, kwamba ilikuwa ni mtu mwingine?
Kwamba muislamu hapaswi kuwa na rafiki mkristo?
Hao wanaokubali kuwa wanandoa ni hao unaowaita Mkristo/Muislam Jina! Mkristo/Muislam halisi na anayeijua dini yake vizuri hawezi fanya kitu kama hicho!
LoRd JeSuS ChRiSt - The Creator Of All.