Nipo njia panda

Nipo njia panda

nani mbuzi

Member
Joined
Jan 2, 2014
Posts
79
Reaction score
11
Naingia moja kwa zote kwenye mada. Nina wasichana wawili mmoja ana kipato namaanisha kazi, msichana wa pili yuko kijijini mkulima, niko kwenye wakati mgumu nahutaji kuoa kati yao.

Na mimi sina kazi naunga unga tu kimjini siku zinaenda.Sasa basi huwa napata msaada wa kifedha kwa huyu msichana mwenye kazi. Pili msichana wa kijijini ananitegemea sana japo halipi kivile ila huyu aliye na kipato anaridhisha sasa.

Nimuoe yupi na wote wako tayari kuolewa?

Ushauri wakuu
 
sioni swali apo.....umeuliza na umeshajijibu.
 
Fanya ana - ana -ana do utapata jibu. Or head or tail tossing
 
Naingia moja kwa zote kwenye mada. Nina wasichana wawili mmoja ana kipato namaanisha kazi, msichana wa pili yuko kijijini mkulima, niko kwenye wakati mgumu nahutaji kuoa kati yao.



Nimuoe yupi na wote wako tayari kuolewa?

Ushauri wakuu

Kwa hakika hukuanza nao uhusiano katika siku moja, yupo alietangulia.
Muoe wa pili kwa sababu uliona wa kwanza ana mapungufu yasiyovumilika ndio maana ukamtafuta wa pili.
Ukioa huyo wa kwanza utajikuta unarudi tena njia panda.

NA kama imani yako inaruhusu waoe wote, kila mmoja uanze nae hapo ulipo. Sio utafute na mmoja uje kutumia na wawili, ni UNYONYAJI.
 
nasisitiza. ukitaka kuoa oa wa kijijin ila ukitak olewa olewa na wa mjni
 
kuna kuoa halafu kuna kuolewa

kama unataka kuoa muoe wa kijijini

kama unataka kuolewa olewa na huyo wa mjini japo utajiona umeoa ila kiuhalisia utakua umeolewa

best answer.....mwisho wa mjadala
 
I feel sorry kwa huyo asiyejua kinachoendelea,coz soon atalia
 
Mpigie wa kijijini muulize unapenda kuwa mkia au kichwa na pia muulize huyo wa mjini hivyo hivyo. Majibu yao, ni kwamba moja atakuwa kichwa mwingine mkia, chukua shilingi rusha juu acha ianguke, upande utakaoangukia ndiyo huyo huyo oa.
 
kuna kuoa halafu kuna kuolewa

kama unataka kuoa muoe wa kijijini

kama unataka kuolewa olewa na huyo wa mjini japo utajiona umeoa ila kiuhalisia utakua umeolewa

hahahaha
 
kuna kuoa halafu kuna kuolewa

kama unataka kuoa muoe wa kijijini

kama unataka kuolewa olewa na huyo wa mjini japo utajiona umeoa ila kiuhalisia utakua umeolewa

Leo umeongea la busara.
 
Kwan katika mahusiano yako ulianza na yupi??labda tuanzie hapo
 
Back
Top Bottom