Nipo njia panda nisaidieni

Nipo njia panda nisaidieni

ENC

Member
Joined
Jan 1, 2014
Posts
23
Reaction score
3
Kwanza napenda kuwasukuru wote milionidhauri vizuri ns hata wale walioniponda kwani akili ni nywere kila mtu anazake.
Mimi ni yule niliyeomba ushauri juu ya nilitumia USA dollars za mchumba angu kwasjili ya kujengea makaburi ya ndugu zake. wakat yy akiwa ulaya.
Sasa leo naomben ushauri tena kwani
yule mchumba angu kaja kutoka ulaya na
nilimweleza sababu ya mm kutumia zile dollars zake na nilimwonyesha CD ya movie niliyoishot wakat wa kazi toka mwanzo had mwisho.
kwa kwel alifurahi sana na alinipongeza et mm ndiye mwanaume ninayemfaa kwan nimeweza kusimamia kila kitu alichoniachia vizuri na eti ile hela alituma iliinisaidie kwa kaz hiyo na alijua kuwa kwa mshahara alioniachia hautatosha ndio maana alituma zile dollars ila alinitega kuwa niziweke bank na nisizitumie.
Hivyo bas ameniomba mara nipatapo ajira. maana nasubiria ajira za ualimu. nipeleke mahari walau laki 500,000. ila mama mkwe ndiye aliyebaki mzazi pekee baada ya baba mkwe kufariki kaniambia kuwa mwenz huu febr niende na mwanae akanikabidhi bint yake awe mke wangu harari ndagu zake wote wameafiki nipewe mke bure kwa jinsi nilivyoonesha uungwana na heshima na uaminifu.
kubwa zaidi mchumba angu hataki mm nimuoe bure bila mahari hivyo anapinga juu ya yy kuozwa bila mahari.
je nifanyeje ndugu zangu. kwani amekataa kwenda kwao had watakapo kubali kupokea mahari yangu lakin mm pia nilimwambia kuwa nipo tayar kutoa mahari kwan had sasa anaujauzito wangu wa mwez mmoja. ila ndugu zao wote wamekataa kupokea mahari yangu wsnataka mm nimuoe binti yao bure.
 
Umesema upo njia panda unaenda ulaya??? Au mi sijaelewa???
 
Njia panda gani hiyo? kwani hujui kuwa ni wajibu mwanaume kulipa mahari kwa ajiri ya mke wake? kama uko taryari peleka hiyo laki tano tena ndogoo hiyo ni sawa nabure kabisa wewe kwa nini unataka upewe mke bure? hayo ulikuwa ukifanya kwa sabab ya mapenzi uliyonayo kwa mchumba wako wala hayapaswi kuwa kama compasation je, ungefanya hayo halafu mkaachana ingekuwaje? mwanamke anaogopa ndoa itakaposhika kasi mkawa mnatofautiana mdomo huwa hauchelewi kutoa maneno kama haya "kwanza wewe nimepewa bure tu na wazazi wako" tafuta laki tano mwanamke aridhike na roho yake
 
Mkuu kalipe mahari wewe uliona wapi mtu akapewa mke wa bure si baadae utamtukana .
 
Tatizo nn hauna hela au nn...wazazi wanakupa bint yao bure kwa kujua kwamba hela ulizotumia kujengea makuburi ni zako. Hawajui kama niza mtoto wao jitahidi toa mahari tena lak 5 ndogo sana
 
Unapswa kulipa mahari! Uoe buree! Nampongeza binti anajitambua! Tafuta wazee wa heshima waeleze, then uwaombe wabembeleze (wawasihi) wakwe zako wapokee mahari japo kidogo. Haiswihi kupewa mke kama "lijamanda"
 
Unapswa kulipa mahari! Uoe buree! Nampongeza binti anajitambua! Tafuta wazee wa heshima waeleze, then uwaombe wabembeleze (wawasihi) wakwe zako wapokee mahari japo kidogo. Haiswihi kupewa mke kama "lijamanda"



ok poa bro nimekupata nitafanyia kaz ushauri wako
 
Kwanza tulia aafu jitambue kisha fahamu kuwa KUPEWA BINTI BURE ni DHARAU NA FEDHEHA kwa binti, sio utaratibu mzuri wakujenga mahusiano mazuri yakifamilia, ukiyajua hayo ni jukumu lako kuwashawishi na kuwafafanulia umuhimu wa MAHALI tena ikiwezekana zidisha LAKI MOJA acha uzembe mwalimu.
NB: UKIPANGIWA KIJIJINI HAUJAYAKAMILISHA HAYO KWA KUKOSA NETWORK NA LAKI TANO UTAMKOSA NA MKE.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom