Pretty
::
Kuwa njiapanda ya maamuzi ndio ukomavu wa maisha hivyo,hongera kwa hatua hii.
::
Vikwazo vyote vinavyoyumbisha upendo wako ni sifa za nje ya mtu..MTU hayuko nje,yuko ndani katika akili,mawazo,msimamo na hekima ya kuyatawala maisha yake ktk usafi,uwajibikaji n.k
Yai likichafuka nje si lazima hata ndani ni chafu.KAMA UMPENDAYE ANA HAZINA NJEMA ZA NDANI,endelea mbele ipo siku watakupongeza.
::
Wapo wengi wamevutwa na mwonekano,urefu,ufupi,elimu,mali,kabila au dini.Lakini muda mfupi baada ya ndoa zao wamejikuta yale yaliyowafanya wawapende wenzi wao yamegeuka kuwa chanzo cha huzuni.JIEPUSHE NA HILI,,
::
Naam,kuna staili nyingi za mtu kulazimika kuanza maisha ya ndoa,mf.mimba,upweke,umri n.k LAKINI njia ya kuanza ndoa na mtu ambaye umemkubali tu ili uwafurahishe marafiki,ndugu,wazazi na hata wafanyakazi wenzio,,SI uamuzi bora maana NDOA ni MKE na MUME,,Usiishi kuwafurahisha watu.Kama afanyavyo daktari,,choma sindano mgonjwa aumie ili akipona ashukuru.Chukua uamuzi ambao utaumiza wengine ili baadae wakusifu.
::
MUOMBE MUNGU
::
KILA LA KHERI
=