Nipeni kura jamani!

Nipeni kura jamani!

UGONVIMWIKO

Member
Joined
Jan 23, 2012
Posts
7
Reaction score
6
Mheshimiwa mmoja alienda Kijiji cha Lubeho kuomba kura wananchi wakamuwekea Meza ili asimame juu na kumwaga Sera zake,bahati mbaya aliongea mambo mengi sana na kwa muda mrefu sana hadi wananchi wakaboreka na kuanza kuondoka mmoja baada ya mwingine.Kufumba na kufumbua watu wote wakawa wameisha isipokuwa mtu mmoja tu alibaki huku akiwa anamuangalia Mwanasiasa na anatoa Machozi.Yule mwanasihasa akachukia sana watu kuingia Mitini lkn akampenda yule mmoja aliyebaki,akamwambia "Wewe ni mfuasi mzuri sana wa chama chetu maana wenzako wote wameondoka lkn wewe bado upo! Nini kimekukuna ktk hotuba yangu hadi unalia na huondoki? Yule Mwanakijiji akamjibu "Hiyo Meza uliyosimamia ni yangu nasubiri ushuke niipeleke nyumbani!"
 
Hahahahaaaaa ina maana km asingekuwa anangoja meza yake nayeye angeshachapa mwendo eeeh dah
 
Ingekuwa mimi siku hiyo hiyo ningeachana na siasa Haaaaaaaaaaaa.............
 
Na atakuwa anatoka chama cha magamba, wenzie wameshampiga juju kama kawaida yao
 
Mheshimiwa mmoja alienda Kijiji cha Lubeho kuomba kura wananchi wakamuwekea Meza ili asimame juu na kumwaga Sera zake,bahati mbaya aliongea mambo mengi sana na kwa muda mrefu sana hadi wananchi wakaboreka na kuanza kuondoka mmoja baada ya mwingine.Kufumba na kufumbua watu wote wakawa wameisha isipokuwa mtu mmoja tu alibaki huku akiwa anamuangalia Mwanasiasa na anatoa Machozi.Yule mwanasihasa akachukia sana watu kuingia Mitini lkn akampenda yule mmoja aliyebaki,akamwambia "Wewe ni mfuasi mzuri sana wa chama chetu maana wenzako wote wameondoka lkn wewe bado upo! Nini kimekukuna ktk hotuba yangu hadi unalia na huondoki? Yule Mwanakijiji akamjibu "Hiyo Meza uliyosimamia ni yangu nasubiri ushuke niipeleke nyumbani!"

Atakuwa ni Chadema maana kwa kudanganya hao ni no. 1, na mwendo ni huo huo mpaka kieleweke.
 
nadhani hawa ni wanachama wa chadema, na hiyo sehemu ni jimbo la Uzini! Time will tell.
 
Back
Top Bottom