Tufikie mahali tuamue kwa usahihi aina ya wabunge tunawachagua
Vigezo ni kutoa VITU MAALUM
Ubinafsi dhambi mbaya sana,huyu mwanamke badala ya kusikitikia watu waliokufa kwa sababu ya
kutumia ARV feki zilizotoka kwenye kiwanda chake na mumewe,anaibuka kulaumu gazeti lililoweka wazi juu
ya uhaini wa kutaka kutorosha sukari iliyoisha muda wake kupelekwa kiwandani kwao Arusha.
Kwamba huyun fisadi aliyenufaika kwa kuwauzia ARV fake watanzania anaweza kusimama mbele ya bunge na kujaribu kujisafisha kwa kashfa ambazo amezitaka mwenyewe.
Hata kama nipashe wasingetoa ufafanuzi wa suala hili lakini watanzania wanafahamu kwamba kiwanda chao cha TPI kimefungwa kwa sababu ya kutengeneza ARV fake na pia wamefunguliwa mashtaka ya kuhifadhi/kutumia sukari mbovu kwa ajili ya kutengenezea madawa kinyume na sheria.