Nini tofauti ya Hirizi, Rozali na Tasbihi?

Nini tofauti ya Hirizi, Rozali na Tasbihi?

Usiingize mambo ya kidunia kwenye ukristo maana rozari haipo kibiblia

Biblia unaijua vizuri?
Unaelewa kanuni za kukufikisha Mbinguni?
Rozari unaielewa?
Kama huelewi chochote kati ya hayo uwe tayari kufundishwa maana maneno yote yanayotamkwa wakati wa kusali Rozari yapo katika Biblia Takatifu yenye vitabu 73.
 
sijawahi soma wakristo wa zamani na Yesu mwenyewe walikuwa wanavaa rozari!

Hizo ni irizi kama irizi nyingine, tena chukizo kabisa
 
Rozari inatumika kusali mafungu ya sala ya bikira Maria ikiwa ni maneno malaika aliyomletea Maria kutoka juu mbinguni
Kisha sala ya baba yetu aliyotundisha Yesu na kulitukuza jina la utatu mtakatifu wa Mungu
Hiyo ndio kazi ya rozari
Hirizi sijui wala tasbihi sijui kazi yake

Kwa kazi Hiyo ya rozari basi ni kifaa kitakatifu kwa wakatoliki
 
Tofauti IPO na ni kubwa saana. Mimi nimepitia sehemu mbili kati ya hizo 3.

Hirizi. - hii ni kinga au tochi au king' amuzi inategemeana umepewa kwa ajili gani? na si kila mjuzi anayeweza kukupatia HIRIZI ya kweli.

Kinga kwa maana wabaya watu wanaotaka kukudhuru kwa uchawi au kwa nguvu za mwili kawaida wanashindwa.

Tochi au king'amuzi hiki hutumiwa zaidi na watu waliokatika mamlaka hasa ya ukamataji huweza kung' amua kitu kilichofichwa au mhalifu na hata wahalifu kuweza kuwang'amua walinzi au kuahirisha siku ya uhalifu. Au kutoonekana kwenye eneo la uhalifu. Au kiongozi kuogopwa na kunyenyekewa na wote walio chini yake na wakubwa zake nk.

Rozari - hii ni mahususi kwa ajili ya Wakatoliki pekee, ambao kwa mujibu Wa mfumo Wa kanisa lao,

Imepanga maombi mbalimbali yaliyokatika mpangilio kupitia Msalaba wenyewe uliokatika Rozari na kila punje zilizo katika mpangilio Wa pamoja na iliyo pekee.

Tasbih - hii huwa nawasikia wakirudia neno SUBHUANAH ALLAH, SUBHUANAH ALLAH kila anapoishika punje tofauti kwa mpangilio Wa kusogea mbele.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom