Threesixteen Himself
JF-Expert Member
- Feb 12, 2013
- 8,223
- 7,993
Matatizo yote tunayoyashughulikia mengi hayahusiani na sheria wala mikataba bali ni kutokuwajibika kwa watendaji wetu kama wenye mali.Ndio maana nimekuuliza kwa fikra zako alichokifanya Mkapa kilikuwa sahihi simply because ya kuvutia investors. Sasa kwa nini mnatupigia kelele za Kuibiwa? Yaani mlango mmeacha wazi kwa kigezo cha kuvutia wageni halafu mnaanza kupiga kelele za Wezi? CCM imepitisha Sheria ya madini kwa hati ya dharura in favour of investors, mlikuwa mmehongwa? Mikataba bado ni siri, mmehongwa?
Mkuu Drama za CCM hazikuanza leo. Wakati wa EPA tuliambiwa bilioni 40 zilirejeshwa na watu wasiojulikana. Maana yake wafanyakazi wa mabenki waliokota mabilioni milangoni na askari walinzi hawakujuwa nani kayaweka ila serikali ikayaagiza mabenki yapokee hizo pesa maana ni za EPA. Kwa hawa waliobeba bilioni 300 wakampelekea Mh Rais bila kuonekana na akayakataa ni kweli maana haya maajabu siyo mara ya kwanza kutokea TZ.Ni sawa na kusema majenshi yote yameenda rogue maana yameshindwa kumkamata huyo mtoa rushwa. Raisi ana TISS pale pale magogoni maana msimamizi wake ni waziri wa ofisi ya raisi, ana mkuu wa majeshi, ana mkuu wa polisi, magereza, uhamiaji, ffu,halafu anashindwa kuwakamata hao watu au walimjia kwa njia ya upepo nini?
Mpaka atakaporudi Bwana Yesu hapatatokea kiongozi mwadilifu hata mmoja. Hicho chama kimeoza kabisa. Hata wafanye je, waseme je.Tafsiri ni kuwa siku wakipokea hongo hawaji kututangazia kwenye vyombo ya habari.
Kitendo cha msemaji mkuu wa CCM kuropoka tuhuma kubwa kama hizo bila ushahdi concrete na angalau kuweka wazi solid proof ni jambo la ajabu sana.
Inaonesha ni jinsi gani tunaongozwa na watu wasiopenda kujiridhisha na kuwa thorough.
Sasa padre hivi hujawahi kwenda hosp kupima ukaambiwa huna malaria, lakini kutokana na dalili unazojisikia ukaamua kwenda hosp nyingine kuhakikisha kama ni kweli huna malaria, na unakuta una malaria. Kuna hosp na hosp na pia kuna maabara na maabara! Matokea ya uchunguzi yanadefy common sense na hata logic! Pamoja ba yote hayo tuendelee tu kuiamini ripoti!?Matokeo ya report ile hayakutokana na kupiga ramuli kama wafanyavyo waganga wa kienyeji.Vile vile Kamati ile haikujifungia chumbani na kuanza kufanya maombi kama wafanyavyo vikundi vya kidini vya "mwendokasi" ili ijulishwe na kuonyeshwa mule ndani ya Makontena kuna nini na kwa kiasi gani.Walichukua sampuli na kuelekea maabara.Kupinga matokeo ya Maabara ni kutaka kutuambia kuwa wewe ukiuguaga na kwenda hospitali huwa hukubali matokeo ya maabara yanayoonyesha kuwa uling'atwa na mbu siku kadhaa zilizopita walipokuwa wanatafuta damu ya kustawisha mayai tumboni mwao na hivi umeambukizwa vijududu vya Malaria.
Ni vigumu mbwa wako unayemlisha akung'ate takukuru kuwachunguza ccmTakururu walitakiwa wafanye kazi yao kwa tuuma na pole pole ni mzee wa kula matapishi yako always
Swissme
Sijawahi kusema popote kuwa nchi hii imewahi kuongozwa na watu wengine nje ya CCM.Ninapo-address Lema na CDM siwatizami kama watu pekee maadui Wa CCM bali watu wenye mtizamo tofauti na wale wanaounga mkono hatua zilizopendekezwa na Kamati iliyochunguza Makanikia.Hata wana-CCM wapo wanaopingana na suala hili.Kwa mantiki ya kawaida ukipikiwa chakula kibovu jambo la kwanza ni kuhakikisha unapata mbadala wa chakula ili usife njaa.Huwezi kuendelea kutumia nguvu ulizo nazo ku-blame na kuuliza uliza tu kilichotokea.Fanya fingerpointing baada ya kuwa umekula.Kuhusu mimi kuwa na mawazo ya Ki-CCM nadhani fanya utafiti kidogo.Wanaonijua akina Mnyika, Mdee, Kafulila, Reg, Mbowe wnafahamu vizuri tabia yangu.Hata katika CCM wako watu kama mhe.Mkasa wanafahamu mimi niko zaidi ya kulalamika tu bila kupendekeza suluhisho chanya.
acha kutuongopea. Tuthibitie kama hajawahi kupokea rushwa tangu azaliwe. Na kwani aseme polepole na siyo msigwa? Au ilipitia Lumumba ikapigwa panga?Ni kutujlisha ukweli wa mambo na pia hao... wafahamu nini kimo kwa Awamu ya tano hii...yaani hapokei hongo eeeeeh
Hapa kazi tu
Magufuli 2020
Na kushawishi pia ni kosaNi kweli Pole pole aliombe taifa msamaha kwa kutoa kauli kama hiyo, pia naomba kukuuliza polepole hao watu waliotaka kutoa rushwa ni akina nani? Wewe ulipataje taarifa hizi na alikuambia nani,?? Je hao watu wamechukuliwa hatua gan za kisheria? ? Kwani kutoa na kupokea rushwa ni kosa sasa hatua zipi zimechukuliwa dhidi yao? ?
Polepole naye babu?Ni tuhuma za kujitungia tu hizo, kile kibabu kizushi na kinafiki sana.
Haya bwanaYule ni kijana mwenzenu jamani