Nini mtazamo wako baada ya kurudi nyumbani?

Jamani,
Tunaposema Wabeba box haina maana kama mnavyofikiria..Huku majuu kazi zote za kuajiriwa tunaita kubeba box haina maana zaidi ya msemo tu.. sawa na Bongo mnaposema Walalahoi haina maana kila mtu asiye kiongozi ni Mlala hoi na alala hoi kweli!
 
Well, mjadala unaendelea vizuri!! M-shaurini MkamaP aache uhuni wa Nansio na aanze kuongea vitu vya maana!!

Ofkoz wapo watu wanabeba boksi na wame-invest bongo kwa kununua madaladala, nyumba n.k na wanazifaa sana familia zao kupita kama wangelikuwa pale pale bongo!! Lakini pia kuna wabongo huku mtoni ambao ni wajasirimali, kuna watu wana own gas stations, staffing agencies, group homes, restaurants, cleaning services, touring services, e.t.c......pia wapo ma-engineer, accountants, doktas, nurses, walimu kuanzia high school mpaka 'versity, madereva wa treni na mabasi, bila kuwasahau waliojiajiri kwa kuendesha ma-18 wheelers, e.t.c!!! Kama alivyosema BAK, MkamaP acha ku-generalize juu ya watu wanaoishi nje ya Bongo, tengeneza convincing argument ya kwanini watu warudi bongo na sio kukandia juu ya vitu usivyovijua au kuvielewa vizuri!!!

Nyongeza....kuna dada mmoja mbongo hapa ninapoishi, anafanyakazi ya $13 kwa saa ambayo ni equiv na kubeba boksi (ana kazi tatu), lakini ana assets kibao bongo na cash money kwenye account kama $150,000+!! Kwahiyo kazi ni kazi tu, cha muhimu ni kuwa na malengo....cha kusikitisha ni kwamba, lau kama angelikuwa bongo, pengine hata hiyo kazi moja asingekuwa nayo leo hii!!

msilewe sana and don't drive while drunk ktk shamrashamra za mwaka mpya....goodluck ya'll.

Mkuu
Sio uhuni ni ushauri tuu hata hivyo bado nashawishika kuona hujasoma maelezo mengi na bado naamini umejibu kulingana na posts mbili ama moja ambazo nilikuwa wenda najibu hoja fulani.

Hoja yangu hapa toka awali nikuwa kama una kazi nzuri hapo marekani,ujerumani,uingereza n,k si busara kuicha kazi yako na kurudi nyumbani bali ninachosema ni kuwa hizo fedha zako zisaidie kule nyumbani kutengeneza kitu cha maendeleo kusomesha ama kujenga vyuo ama miundo mbinu n.k hii ni kutokana na mkono wako unapokomea.

Lakini kwa wezangu na mimi walio maliza masters Ukraine hawana kitu na uwezekano wa kupata kazi haupo kwanini ang'ang'anie kupigwa baridi huko?

Ukweli tuambiane ukweli na isichukuliwe kama dharau ama nini hata sisi tunaobeba Mabox tuyabebe tukiwa na malengo yalale na mtazamo ulele wa kwamba baada ya miaka kadhaa kazi hii nitastaafu ya kubeba box na nitakuwa nimejikusanyia kiasi kadhaa ili nikafanye kitu fulani nyumbani (labda kama wewe ni raia wa nchi hiyo hapa ni stori nyingine)ni ukweli usiopingika kuwa kazi ya mtulinga hawezi kudumu miaka mingi wewe na mimi ni binadamu itafikia mahala tuta kubali matokeo ya kwamba kazi hii hatuziwezi tena.

Narudia tena wewe kama una kazi hapo ulipo sikushauri kurudi unless unaenda Tz kama mwekezaji.Na wewe mwezangu na mimi kwanini uendelee kupigwa baridi ? Pesa unazitafuta ili zikusaidie sio kutafuta pesa ili uzisaidie.
 
YNIM,Mkandara,MkamaP,B-A-K,....

..nadhani kinachopaswa kufanyika ni MAANDALIZI.

..mtu usirudi kwa haraka na pupa, kama kawaida ya wengi walivyoondoka bongo.

..cha msingi ni kuwa na mahali pa kufikia na kuwa na uhakika wa mlo, na fedha ndogo-ndogo kama ya usafiri, matibabu, etc. baada ya hapo ndiyo unaweza kufikiria kuwa na mradi au biashara kubwa.

..kitu kingine ni kuepuka mashindano na pressure; kwamba wewe umetoka nje hivyo, unapaswa kuishi maisha ya aina fulani, na kuwa juu ya wale uliowaacha bongo.

..mwisho, test 'zali' kwanza. nimeshuhudia wa-Tanzania wanaorudi hatua kwa hatua.
 
Wajamani
Maana ya mbeba box.
Mimi ninavyoelewa na ninavyolitumia neno Mbeba box ni Mtu yeyote asiye Raia wa nchi husika anafanya kazi kiujanja ujanja mfano anajiandikisha yeye ni mwanafunzi ili apate kibali cha kuishi na kufanya kazi and the like ,Mara nyingi lakini si mara zote hatma ya mtu huyu ni tete tena kwa nchi kama uingereza mtu unaogopa hata kwenda kusalimia ndugu zako bongo maana ukienda tu wanaweza kugeuzia uwanja wa ndege.

Mtu mwenye nafasi.
Ni wale waliomaliza shule kwa bahati nzuri akaajiliwa ktk kampuni lamaana kwa kupitia kwake ikampatia haki zote za kufanya kazi.Ama kaajiliwa moja kwa moja kutoka TZ ktk makampuni husika ama ana uraia wa nchi husika.
 
Wewe unaongea vitu gani bana!? kwa taarifa yako mbeba box yupo well off hapa (unyamwezini, sijui huko ulaya) kuliko kama akirudi nyumbani. Kwani nyumbani hata hiyo kazi ya kubeba box yenye benefits kama healthcare, vacation hours, sick leave na mazagazaga mengine hakuna...!! Kama jobless ni 50% or higher (kwa mujibu wa mchangiaji mmoja hapa), sasa watu warudi ma-home kufanya nini? reasoning yako ipo wapi bwana mheshimiwa? au unataka kuingiza watu kingi kwa makusudi!? watu bana, kaaaaaazi kweli...cha muhimu hapa ni kuhamasishana ku-invest bongo (kama kuna haja hiyo), kwani kwa data ninazozifahamu kwa nchi za East Africa na Horn of Africa kama Kenya, Uganda, Ethiopia na Eritrea, sisi wa bongo ni wa mwisho kwa kutuma pesa nyumbani!! Sasa sijui ni kwasababu tupo wachache au ndivyo tulivyo, kwamba "tumekutosa" home kiaina...

Naamini tupo pamoja ila hatuelewani lugha.
 
Lakini Mkuu
mbona hutaki kunielewa mimi sikuelewi nimesema watu wenye nafasi nikiwa na maana yahao waliokwenda shule hawana sababu ya kurudi nyumbani na tunachowaomba watupe sisi fursa huku nyumbani.

Nawale wezangu na mimi wabeba mabox tuangalia namna ya kurudi nyumbani .Mkuu labda sieleweki ama labda tayari umeshaniweka ktk kundi fulani ,mbona narudia sana hayo maneno kipi kisichoeleweka??


Nadhani unafikiri box ni literally kubeba box tu.Kwangu mimi mtu akisema kupiga box ni hata pale anapofanya kazi ambayo si ya taaluma aliyosomea na mara nyingi ni blue color.
Kwa mfano wewe ni Daktari lakini unakosa kazi hospitali kwa kipindi kile wanakwambia ukalee wazee kwenye nursing home.
Na hata hivyo usiwadharau wabeba box na kuwataka warudi nyumbani,wengi wanatengeneza pesa nzuri tu.Inategemea akili yako katika kazi yoyote ile unayofanya na ndiyo mana mnaweza kupokea mshahara sawa kazini au wewe ukapokea kidogo lakini ukafanya mambo ya maana kuliko mwenzako.
Kwa mfano huo wa nursing home niliokupa Jamaa wanakula 12$ per hr huku ukivuta uzoefu na kuchakarika kutafuta kibarua cha taaluma yako.Je ni sawa na kwenda kutupwa hospitali ya wilaya Kigonsera kwenda kupiga mzigo 24/7 na kuambulia kamshahara kiduchu kasikokutoa hata katika matumizi yako mwenyewe kwa mwezi?Kuna wengine kwao kitu cha kwanza ni maslahi.Kama box linalipa kuliko kazi ya ofisini ya taaluma yake anaona bora apige box tu,sasa kwanini huyu naye useme 'wale wenzangu na mimi wabeba box turudi nyumbani'?
Halafu kuna swala la mazingira mazuri ya kazi na nafasi za kujiendeleza zaidi kielimu.Je huyo mbeba box unayemtaka arudi utampatia hizo nafasi na hiyo mikopo yenu ya mizengwe Chukulia kuwa huyo mbeba box ni form 4/6 leaver kwa mfano na pale alipo kama ana nia ya kusoma anaweza ku save 1000$ na kulipa community college na kuendelea kukata msuli huku akipiga box?
 
Wajamani
Maana ya mbeba box.
Mimi ninavyoelewa na ninavyolitumia neno Mbeba box ni Mtu yeyote asiye Raia wa nchi husika anafanya kazi kiujanja ujanja mfano anajiandikisha yeye ni mwanafunzi ili apate kibali cha kuishi na kufanya kazi and the like
,Mara nyingi lakini si mara zote hatma ya mtu huyu ni tete tena kwa nchi kama uingereza mtu unaogopa hata kwenda kusalimia ndugu zako bongo maana ukienda tu wanaweza kugeuzia uwanja wa ndege.
Jamani,
Tunaposema Wabeba box haina maana kama mnavyofikiria..Huku majuu kazi zote za kuajiriwa tunaita kubeba box haina maana zaidi ya msemo tu.. sawa na Bongo mnaposema Walalahoi haina maana kila mtu asiye kiongozi ni Mlala hoi na alala hoi kweli!
Wengine wanajua ni hasa kubeba mabox mabegani au zile kazi za kibega.......BTW wabeba box is a kind of Blue collar jobs thats all huitaji ujuzi husika kuweza kuifanya...

Tuendelee.......
 
Acha maneno wewe! Kama huna walau $50,000, kibanda/vibanda vyenye akili, na godfather au washkaji wa kukushika mkono kukuelekeza njia mjini basi usirushe mguu bongo!!! Hiyo "walau 50,000" itakusaidia if and only if una akili ya biashara...vinginevyo uwe fisadi au mmoja ya watoto wao, ama sivyo utajuta kuzaliwa na nyoro itakutoka!!.

Watu wengi "washkaji" ninao wajua mimi waliorudi bongo, kwanza, wengi wao ni 'vilaza' kiasi kwamba wameshindwa ku-compete hapa hivyo wanarudi home ambako kwa mawazo yao wanaweza kupata mambo mazuri juu ya elimu yao ya ughahibuni. Pili, jamaa wengi ni wazushi, aidha ni mashabiki wa ufisadi (wanapenda kona kona, dhulmati na wezi) au wana ndugu zao ambao ni mafisadi na wanakuwa wameshapewa michongo.

Usifuate mkumbo wa kurudi bongo kichwa kichwa.........utaumbuka!!

Wanabodi,

Mimi nimerudi Bongo mara kadhaa na kujaribu kuangalia hali halisi kabla sijafikia maamuzi ya kurudi moja kwa moja lakini kusema kweli Bongo INATISHA...
Sasa nitazungumzia tu experience yangu na pengine kuongezea machache ambayo pia nimeyaona..
Ni makosa makubwa kuondoka Ulaya ukitegemea ajira na pengine nitawashauri wasomi wetu kitu kimoja kwamba unaposoma shule hiyo lengo lako liwe kuwa Mwajiri yaani kwa kiswahili safi TAJIRI...nikiwa na maana nje ya neno RICH isipokuwa mwenye KUTOA AJIRA..
Somo hili ndilo litangulie akilini mwako kwa sababu kama nilivyosema huko mwanzo muhimu sana kutazama WATU na MAZINGIRA kabla hujafikia maamuzi muhimu..Hivyo kwa sababu Tanzania bado ni dunia ya tatu, elimu ya watu wengi ni duchu na ewekeshaji ktk sekta ya ajira ni ndogo sana kiasi kwamba unemployment ni zaidi ya asilimia 50, Taasisi za kutoa huduma na biashara bado ni chache sawa na wilaya moja ya nchi za Ulaya.. bajeti ya nchi nzima ni sawa na bajeti na kitongoji cha mji wa Ulaya wakati Population yetu inashindana sawa na nchi za Ulaya...Tofauti zote hizi za watu na mazingira ndizo zinazoifanya Tanzania kuwa tofauti.
Isipokuwa kitu kimoja tupo pamoja ni kwamba, elimu siku zote ni muhimu sana na huchukua nafasi kubwa ya ufanisi ktk innovation, of which is the key to success..

Sasa unapokwenda Bongo na elimu yako ukifikiria unaweza kubadilisha mwenendo wa taratibu za huduma na biashara nchini kama Ulaya wakuu zangu utadunda na utaonekana unachekesha..Na kibaya zaidi utashindwa hivyo elimu yako itakuwa bure kwa sababu hukuzingatia watu na mazingira mapya ya Tanzania ambyo kinadharia ulitaka kuibadilisha iwe kama Ulaya.

Kwa hiyo kitu cha kwanza unachotakiwa kuingia nacho Tanzania ni idea ya kui nvest na hiyo elimu yako ndio the right key (tool) leading to innovation..wala usitegemee mtaji toka kwa tajiri fulani pale bongo..Utadunda sana sana utaibiwa idea yako na itafanyiwa marekebisho kibongo bongo (watu na Mazingira) kwa sababu Imani kubwa ya biashara na mafaniko Bongo inategemea na muda wa returns za kile unachojaribu ku invest... Hakuna tajiri (rich) ambaye anataka kusubiri matunda ya Uwekeshaji wake miezi sita au mwaka mzima.. Biashara ya nyumbani ni papo kwa hapo yaani idea yako lazima iwe na short term returns, mtaji uliowekeshwa utarudi within few months.

Kikwazo kingine ni Ukiritimba..kwa yule anayetafuta ajira au ku invest ni lazima awe na Mtandao, kama alivyosema FMES kwamba viongozi wetu ni reflection yetu ndivyo maisha ya kila siku navyoendesha..Tusitake sana kuzungumzia Mtandano ndani ya chama tawala CCM, lakini ukweli ni kwamba mtandao upo kila sehemu, siwezi kuamini kwamba vyama vya Upinzani havina makundi ya Mtandao ndani yake nitakuwa najidanganya kwani kama kungekuwa hakuna mtandao basi vyama pinzani vingeweza kuungana. Hakuna sababu ya kutooungana zaidi ya watu kuwa ktk makundi tofauti ya vijiwe...
Pia ukitembelea vitongoji mijini kila eneo lina kijiwe chake na wanachama wa kijiwe hicho..na laa ajabu ni kwamba vijiwe hivi vimejenga hata chuki baina yao out of nothing maadam tu kijiwe cha Kinondoni hakiwezi kula sahani moja na kijiwe cha Magomeni, Temeke, Kariakoo, Sinza na kadhalika..kisha within vitongoji hivyo kuna sub groups ambazo pia haziwezi kupatana hata kama lengo la vijewe hivi ni kuzungumzia matatizo sawa na kundi jingine...
Athari za Ukiritimba zimeingia hadi sehemu za uwekeshaji, hivyo ukiwa na idea, elimu na nondo zote za uwekeshaji toka nje isikupe guarantee kwamba utafanikiwa kwani imani kubwa ya ujenzi wa nchi yetu Tanzania leo hii ni kwamba - FEDHA ndio msingi wa Maendeleo..
Tatu, ni muhimu sana kwa vijana wetu mnaporudi nyumbani kufahamu kwamba Tanzania kama nchi na watu wake inatazama vitu kwa darubini tofauti kabisa..Kwa mfano ukifikira kuwa Kazi ndio kipimo cha Utu wao wanaweza kuamini kwamba - Utu ndio kipimo cha kazi..jambo ambalo linaweza kuwa na results tofauti kabisa..

Nne, Ni lazima ufahamu kwamba Tanzania sawa na nchi zote maskini - Cheo sio dhamana isipokuwa ni Title inayomwezesha mtu kuwa Mungu Mtu ktk sekta aliyokabidhiwa madaraka..kuondolewa madarakani mara nyingi hutafsirika kama mapinduzi ambayo yametokana na chuki na wivu.. hakuna kiongozi hata mmoja anakubali accountability kwa sababu moja - Accountability sio Utamaduni wetu...
Wananchi au kwa lugha nyepesi wateja ndio wanatakiwa kuwa accountable, ni wao wenye shida na maskini hivyo ni jukumu lao kufanya kazi, kuomba, kusubiri na kunyenyekea na kadhalika.. Accountability ni hoja inayotazama mteja ama mwananchi sio kiongozi kwani kwa desturi zetu kiongozi ni Nyapala ambaye husimamia watumwa kufanya kazi kwa ufanisi akilipwa pango kubwa la ile title ya Unyapala. Ni urithi tulioachiwa na mkoloni hivyo leo hii Nyapala atapimwa ufanyaji kazi wake kwa utu anaotumia yeye yaani yule Nyapala poa kabisa!

Kwa hiyo tusishangae kuona Mwanakijiji anapotaka kuongea na waziri mkuu kuhusiana na hali mbaya ya wanafunzi Russia anakujibu - Anakula piga simu baadaye..na hiyo baadaye Mwanakijiji asimpate tena waziri zaidi ya kutamiwa makachero wamtafute huyu Mwanakijiji ni nani!..
Tano na mwisho - ni Ufisadi, huu sina hata la kuongea zaidi ya kusema elimu yako itakuwa na manufaa tu kama inaweza kutumika ktk Ufisadi.. Hiyo ndio elimu inayotakiwa Tanzania, elimu ya kobomoa na sio ya kujenga.

Kwa mtaji huo ndugu zangu kulingana na WATU na MAZINGIRA nimejifunza mengi ambayo inabidi kuyafanyia darasa jipya..Lakini wakati huo huo JK ameweza kufungua baadhi ya ajira nchini pamoja na kwamba ameshindwa kuondoa Ukiritimba, kusimamisha Accountability na kuhakikisha Ufisadi hauna nafasi...
Kwa mara ya kwanza nimeona traffic ya vijana inarudi nyumbani. Wakati wa Mwinyi na hasa Mkapa, tulishudia vijana wengi sana wakiondoka nchini kwenda tafuta Elimu nje..Aidha ilikuwa shida kupata elimu nchini au kwa sababu Mkapa alirudisha hadhi ya elimu ktk kipimo cha ajira...
Kutokana na vijana kurudi nyumbani kwa kasi kubwa inanipa moyo kwamba madirisha yamefunguka kama sio milango kuwa wazi..meaning Opportunities zipo!..

Wazee mmeua!!
 
Mara nyingi sana tunasikia viongozi wetu wakiwa wanazungumza na Watanzania nje ya nchi, Botswana, Afrika Kusini, Canada, UK na kwingineko wanashauri sana vijana warudi nyumbani kusaidia juhudi za kujenga Taifa.
Lakini mimi binafsi nimesikia tofauti kidogo kutoka kwa ndugu na jamaa waliofuata ushauri huu. Kwamba fursa hiyo ya kujenga taifa baada ya kurudi hawaipati !!!! Ndugu mmoja alisoma mambo ya computer nje na kufanya kazi hiyo kwa miaka 7 nje. [ ni mtaalamu wa kutisha wa IT } Akaamua kurudi nyumbani kusukuma gurudumu la maendeleo kama wakubwa walivyosihi, lakini baada ya muda alirudi tena na kusema ameshindwa kufanya kazi nyumbani na kwamba atarudi baada ya kustaafu !!
Mwingine alisoma mambo ya masoko, akapata kazi shirika la umma, lakini bosi wake alimnyanyapaa sana. Jamaa akitoa mawazo mapya bosi anasema anataka kumnyang'anya kazi au anafanya kazi kwa sifa. Sasa yeye hana uwezo wa kurudi nje alikokuwa. Inabidi awe hapohapo huku manung'uniko hayaishi. Na kutusihi sisi " jamani msirudi".
Jamaa mwingine akaniambia kama siku hizi nina lafudhi ya Ki-Kenya basi nirudi nyumbani !!!Maana hao ndio wana kazi zote nzuri.
Tupatie experience yako baada ya kurudi.

Mkuu
Mtazamo wangu ni kuwa, wanaotaka kutorudi wasirudi na zaidi wanaotaka kutoka watoke. Dunia ni kubwa sana, Watanzania wanahaki ya kukaa na kufanya kazi wanakotaka, cha msingi waridhie na wafurahie maisha. So if one decides to come back or opt not to go abroad, he/she is doing that at his/her own risk!
 
Back
Top Bottom