Habari wanajamii F.Mimi nimekuwa mtumiaji mzuri wa internet kwa muda mrefu kabla hata mkongo wa mawasiliano haujaanza kuzungumziwa.Ninachoshangaa ni kwa kumekuwa kukitolewa taarifa mbalimbali kuhusu uwepo wa mkongo huo na faida yake.Swali ni je hapa tulipo ndio tumeshaanza kufaidi huo mkongo wa taifa?Mbona gharama ye internet bado ipo juu?Hivi mkulima na mtanzania wa chini atapata elimu inayosemwa kupitia mtandao wa internet?Hebu wanaofahamu gharama halisi watujuze maana haiwezekani wenzetu majuu internet sio anasa lakini sisi inaonekana bado ni huduma ya wachache,nahisi kuna ufisadi hapa