Mindi
JF-Expert Member
- Apr 5, 2008
- 3,523
- 4,998
Ukitafakari yanayoendelea dhidi ya CAG, juu juu inaonekana kwamba ni Bunge ndiyo lina mgogoro na CAG. lakini ukiangalia vizuri, mwenye mgogoro na CAG hasa ni Rais Magufuli.
Ukimwangalia Spika Ndugai siku ile alipotoa kwa mara ya kwanza agizo la CAG kutakiwa kufika mbele ya kamati ya Bunge, akatoa vitisho kwamba ataletwa hata kwa pingu, unaona kwamba hapa kuna kitu nyuma ya pazia. Ndugai aligeuza jambo la kanuni za bunge kuwa jambo la kisiasa. Tena siasa za CHUKI, zinazohatarisha misingi ya taifa letu. Vitisho vya Ndugai viliashiria kwamba tayari "kesi" ya CAG imeshasikilizwa na kutolewa hukumu na Spika mwenyewe. Hukumu ni kwamba CAG ametiwa hatiani tayari toka siku hiyo. kwa hiyo vile vikao vya kamati ya Bunge vilikuwa geresha tu, na pengine ndiyo maana iliamuliwa ripoti ya kamati hiyo iwasilishwe sasa hivi ili kuzuia watanzania wasione huo muunganiko wa "hukumu" ya Ndugai na hukumu ya kamati.
Lakini kubwa zaidi ni swali: Ni nani yuko nyuma ya Spika Ndugai? Maana siyo rahisi Mhimili mmoja uanze kubwata kuhusu mhimili mwingine, pasina "mkuu" wa "MIHIMILI" kujua. Na tulipata mwanga pale mkuu huyu, Rais Magufuli, alipotoa neno kuhusu "kesi" hiyo, kwamba mbona inacheleweshwa? ni siku ile alipoongelea kushangazwa na "upelelezi kesi ya MO". Ni kama alikuwa anataka hukumu itangazwe haraka. Lakini pia ni kama alitaka kujifanya yuko pembeni na jambo hili, wakati ndio hasa stelingi mwenyewe. ni kama alitaka kuonekana anapenda haki itendeke, kama alivyokusudia katika suala la MO. Katika suala la MO, najua mahakama ya wananchi ilishatoa maamuzi na hapo Rais alishachelewa.
Tunapata mwanga zaidi pale Rais alipoamua kupokea Ripoti ya CAG KIMYAKIMYA, wakati alipokea ripoti ya TAKUKURU kwa MBWEMBWE. na akatamba kwamba huyu bosi wa TAKUKURU ni TISS!!! sasa hapa kuna jambo kubwa sana. Tunaweza kuona kwamba ni Rais ambaye kamsusia CAG, na siyo hasa kwa sababu ya alichosema kule UN, siyo hicho tu, bali msimamo wa CAG kutotaka UJINGAUJINGA katika mambo ya matumizi ya Fedha za Serikali. Kwa hio hicho tunachokiona kama "hatua" za Bunge letu, ni hasa mkakati wa Rais Magufuli "kumkata miguu" CAG, akitafuta njia za "kumdhoofisha" CAG ili kukwepa vifungu vya katiba vinavyomlinda, lakini pengine kumfanya awe USELESS, kama ilivyo useless ile TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA. Maana kama ripoti ya CAG haijadiliwi Bungeni, na Rais ndiyo kazisusa, nguvu ya ripoti hizo itatoka wapi?
Lakini, kama katiba inamtaka Rais kuwasilisha bungeni Ripoti yake ndani ya siku 7 tangu kuipokea, ataiwasilisha? na bunge je, litafanya nini kwa ripoti hiyo? Je, uamuzi wa Bunge kumsusia CAG, UMEVUNJA KATIBA? Maana Katiba ndiyo inalielekeza bunge kufanyia kazi ripoti ya CAG. Bunge lina hiari ya kuacha kushirikiana na CAG? Mimi nadhani Bunge halina ubavu wa kumsusia CAG. Linaweza kufanya hivyo kwa KUVUNJA KATIBA, KWA KUSIMAMIWA NA RAIS AMBAYE HAOGOPI KUVUNJA KATIBA, KAMA AMBAVYO AMEFANYA MARA KADHAA.
Kitendo cha Bunge kumhoji CAG kwa kutumia haki yake ya kikatiba ya kutoa maoni, ni cha kuvunja katiba. kama ni hiyo kauli yake CAG, alishafafanua kwamba ni lugha ya kawaida ya kihasibu. NA NI UKWELI.
Sasa Bunge limefanya uamuzi, Magufui amefanya uamuzi, CAG naye kaamua kusimamia aliyoyasema. MAHAKAMA YA WANANCHI INASEMAJE? hilo ndio swali kubwa na muhimu kwa sasa.
Ukimwangalia Spika Ndugai siku ile alipotoa kwa mara ya kwanza agizo la CAG kutakiwa kufika mbele ya kamati ya Bunge, akatoa vitisho kwamba ataletwa hata kwa pingu, unaona kwamba hapa kuna kitu nyuma ya pazia. Ndugai aligeuza jambo la kanuni za bunge kuwa jambo la kisiasa. Tena siasa za CHUKI, zinazohatarisha misingi ya taifa letu. Vitisho vya Ndugai viliashiria kwamba tayari "kesi" ya CAG imeshasikilizwa na kutolewa hukumu na Spika mwenyewe. Hukumu ni kwamba CAG ametiwa hatiani tayari toka siku hiyo. kwa hiyo vile vikao vya kamati ya Bunge vilikuwa geresha tu, na pengine ndiyo maana iliamuliwa ripoti ya kamati hiyo iwasilishwe sasa hivi ili kuzuia watanzania wasione huo muunganiko wa "hukumu" ya Ndugai na hukumu ya kamati.
Lakini kubwa zaidi ni swali: Ni nani yuko nyuma ya Spika Ndugai? Maana siyo rahisi Mhimili mmoja uanze kubwata kuhusu mhimili mwingine, pasina "mkuu" wa "MIHIMILI" kujua. Na tulipata mwanga pale mkuu huyu, Rais Magufuli, alipotoa neno kuhusu "kesi" hiyo, kwamba mbona inacheleweshwa? ni siku ile alipoongelea kushangazwa na "upelelezi kesi ya MO". Ni kama alikuwa anataka hukumu itangazwe haraka. Lakini pia ni kama alitaka kujifanya yuko pembeni na jambo hili, wakati ndio hasa stelingi mwenyewe. ni kama alitaka kuonekana anapenda haki itendeke, kama alivyokusudia katika suala la MO. Katika suala la MO, najua mahakama ya wananchi ilishatoa maamuzi na hapo Rais alishachelewa.
Tunapata mwanga zaidi pale Rais alipoamua kupokea Ripoti ya CAG KIMYAKIMYA, wakati alipokea ripoti ya TAKUKURU kwa MBWEMBWE. na akatamba kwamba huyu bosi wa TAKUKURU ni TISS!!! sasa hapa kuna jambo kubwa sana. Tunaweza kuona kwamba ni Rais ambaye kamsusia CAG, na siyo hasa kwa sababu ya alichosema kule UN, siyo hicho tu, bali msimamo wa CAG kutotaka UJINGAUJINGA katika mambo ya matumizi ya Fedha za Serikali. Kwa hio hicho tunachokiona kama "hatua" za Bunge letu, ni hasa mkakati wa Rais Magufuli "kumkata miguu" CAG, akitafuta njia za "kumdhoofisha" CAG ili kukwepa vifungu vya katiba vinavyomlinda, lakini pengine kumfanya awe USELESS, kama ilivyo useless ile TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA. Maana kama ripoti ya CAG haijadiliwi Bungeni, na Rais ndiyo kazisusa, nguvu ya ripoti hizo itatoka wapi?
Lakini, kama katiba inamtaka Rais kuwasilisha bungeni Ripoti yake ndani ya siku 7 tangu kuipokea, ataiwasilisha? na bunge je, litafanya nini kwa ripoti hiyo? Je, uamuzi wa Bunge kumsusia CAG, UMEVUNJA KATIBA? Maana Katiba ndiyo inalielekeza bunge kufanyia kazi ripoti ya CAG. Bunge lina hiari ya kuacha kushirikiana na CAG? Mimi nadhani Bunge halina ubavu wa kumsusia CAG. Linaweza kufanya hivyo kwa KUVUNJA KATIBA, KWA KUSIMAMIWA NA RAIS AMBAYE HAOGOPI KUVUNJA KATIBA, KAMA AMBAVYO AMEFANYA MARA KADHAA.
Kitendo cha Bunge kumhoji CAG kwa kutumia haki yake ya kikatiba ya kutoa maoni, ni cha kuvunja katiba. kama ni hiyo kauli yake CAG, alishafafanua kwamba ni lugha ya kawaida ya kihasibu. NA NI UKWELI.
Sasa Bunge limefanya uamuzi, Magufui amefanya uamuzi, CAG naye kaamua kusimamia aliyoyasema. MAHAKAMA YA WANANCHI INASEMAJE? hilo ndio swali kubwa na muhimu kwa sasa.